Author name: SW - Melkisedeck Shine

Kisa cha mama na mwanae na mkwe wake

Kuna kijana mmoja daktari alikwenda kuposa. Binti aliyemposa akamuwekea masharti mazito. Akamwambia chagua mawili imma kunioa mimi au kukaa na mama yako, kwa sababu ukinioa mimi sitokubali mama yako aje hata harusini kwangu! Yule kijana aliemewa. Hakujua la kufanya. Mke anamtaka, lakini mama yake pia anampenda. Hivyo aliamua kuomba ushauri kwa mwalimu wake wa chuo kikuu. Alimwambia: moyo wangu unampenda mno binti niliyekwenda kumposa, lakini pia siwezi kuishi mbali na mama yangu. Nifanye nini?

Yule mwalimu mwenye hekima ambaye alikuwa anajua tabu alizopitia mama wa kijana yule, alimjibu kwa kumwambia: Kabla ya kukueleza uchague yupi kati ya wawili hao, rudi nyumbani, na leo usifanye chochote, ila kuikosha mikono ya mama yako. Yule kijana alifanya kama alivyotakiwa na mwalimu wake. Alipofika nyumbani aliomba idhini kwa mama yake amruhusu kuikosha mikono yake, na yule mama alimkubalia bila ya ajizi yoyote. Yule kijana alipoanza kuikosha mikono ya mama yake na kuona jinsi ilivyogugutaa kwa kazi za sulubu, alilia sana. Muda wote huu alikuwa hajawahi kuangalia viganja vya mama yake. *Je, na wewe umewahi kukaa na kuangalia viganja vya mama au baba yako kuona tabu walizopitia kukulea?* Kumbe baba wa yule kijana alifariki dunia yeye akiwa bado mdogo, yule mama aliamua kusamehe kila kitu kwa ajili ya mustakbali wa mwanawe. Alijitolea kufanya kazi za sulubu.

Alikubali kuwa mtumishi wa ndani, kukosha nguo, kupiga deki na kila kazi ambayo alihisi ingelimletea chumo la halali bila ya kujali ugumu wa jkazu hiyo. Juhudi zake zilizaa matunda na kufanikiwa kumlea na kumsomesha mwanawe hadi chuo kikuu na sasa ni daktari ambaye ana mustakbali mzuri. Baada ya yule kijana kukumbuka yote hayo, alifanya haraka kumpigia simu mwalimu wake huku macho yakiendelea kububujikwa na machozi akimwambia, siwezi kusubiri hadi kesho. Jibu nimeshalipata. Siwezi kumtupa mama yangu kwa ajili ya mtu asiyejua thamani ya mama. Ahsante sana kwa kunionesha njia sahihi! Kamwe siwezi kumuuza mama yangu kwa ajili ya leo yangu wakati yeye ameuza maisha yake yote kwa ajili ya mustakbali wangu.
NANI KAMA MAMA?!? Maa! Tabasamu lako ni ufunguo wangu wa ufanisi.
Kama umeipenda, itume kwa wengine ili nao wazinduke.

Majuto ni mjukuu. Angalia kisa cha huyu dada

Dada mmoja aliyejulikana kwa jina
la Angel, alikuwa anafanya
biashara ya kujiuza ili aweze
kuweka kitu tumboni mwake.
dada huyo alikuwa na wateja
wamaana na mapedeshee wengi
sana kwa hiyo kwa siku yeye
kuondoka na laki 4 au 5
ilikuwa ni kawaida sana.

Siku moja dada Angel aliamua aende
hospitali ili akatoe mimba
aliyokuwa nayo tumboni mwake,
alifanikiwa na kutoa mimba ile
lakini baada ya kumaliza utoaji wa
miamba alimuomba daktari atoe
kizazi kabisa ili asipate tabu ya
kuja kutoa mimba kila mara!

Daktari alifanya kama
alivyoambiwa.
Dada Angel alirudi mtaani na
kuendelea na biashara ya kujiuza.

Siku moja ilikuwa jumapili Angel
alikutana na rafiki yake wa muda
mrefu waliyekuwa wanaishi wote
enzi za utoto wao, rafiki yake
huyo alimwambia Angel waende
kanisani, ili kuficha aibu ya
biashara aliyokuwa anafanya;
dada Angel alikubari na
wakaamua kwenda wote
kanisani.

Siku hiyo Angel alilielewa sana neno la Mungu kutoka kwa mchungaji na akaahidi
kuwa jumapili ijayo ataenda, basi
ikawa tabia mpya ya dada Angel
akawa kila siku anafanya biashara
zake za kujiuza na jumapili
anaenda kanisani..

Kadri siku
zinavyozidi kwenda dada Angel
akaanza kupunguza biashara ya
kujiuza na kumgeukia Muumba
mpaka akaacha kabisa tabia ya
kujiuza na kuanza kufanya
shughuli nyingine zilizokuwa
zinamuingizia kipato.

Siku moja Angel alienda kanisani
na alipokuwa ameketi mchungaji
alimfuata na kumwambia
“nimeoteshwa kuwa ww ndiyo
utakuwa mke wangu wa kufa na
kuzikana” dada Angel alishtuka
na alimtazama mchungaji na
kumwambia “mchungaji
umekurupuka mimi kamwe
siwezi kuwa mke wa mtu na
kamwe siwezi kuzaa” alimaliza
Angel na kuondoka kanisani.

Kila wiki aliyokuwa anaenda kanisani
dada Angel alikutana na maneno
yale yale kwa mchungaji na
mchungaji alimwambia “nimeota
umepata ujauzito na umenizalia
watoto wanne” Angel
alimuangalia mchungaji na
kusimama na msimamo wake
ulele ule.

Siku zilizidi kwenda lakini
kutokana na mchungaji
kuendelea kusema maneno yale
yale basi ilibidi dada Angel
akubali na akakubali kuolewa na
mchungaji na wakafunga ndoa na
ndoa yao ilikuwa ya furaha sana.

Kadri siku zilivyozidi kwenda dada
angel alianza kuona mabadiliko
mwilini mwake na kuamua
kwenda katika ile hospitali
aliyowahi kwenda mwanzo kutoa
mimba na kumkuta daktari
aliyemfanyanyia utoaji wa
mimba siku za nyuma, baada ya
daktari kumona Angel akajua
amekuja kwa shida nyingine
ikabidi amuulize “Dada Angel
nikusaidie nini tena dada yangu”
Angel alijibu kuwa anahisi
anadalili za ujauzito, Daktari
alicheka sana baada ya kuambiwa
hayo majibu kutoka kwa angel
na daktari alimwambia “Dada
Angel naona umechanganyikiwa enh dada yangu?? mimi ndiye
nilitoa kizazi chako leo iweje uwe
na mimba acha kuchekesha
walionuna”

Angel alimwambia daktari
chukua vipimo kapime, kweli
daktari alifanya hivyo na baadae
akarudi mikono inamtetemeka na
kumwambia angel “Dada
angel nipeleke na mimi kwa
huyo uneyebuabudu nami niweze
kumuabudu maana ni mkweli na
anasaidia wanyonge,

Dada
Angel wewe ni mjamzito wa miezi
miwili”. Angel alilia huku
akiamini kuwa Mungu ashindwi
na kitu chochote Duniani.
Daktari wiki ilifata naye alienda
kanisani na kuanza kumtukuza
Mungu…

Ndugu yangu hata kama upo
katika wakati mgumu kiasi gani
lakini kumbuka yupo anaweza
kufanya ugumu wa mambo yako
kuwa mepesi kama unatafuna
karanga.
hakuna kinachoshindikana kwa
Mungu,comment AMINA kama unaamini
hakuna kinachoshindika na kwa
jina lake yeye muumba na kama
unaamini magumu yako yote
yenaweza kuwa mepesi
kupindukia

Shopping Cart