SALA YA ASUBUHI
Tuusifu Utatu Mtakatifu wa Mungu Mwenyezi, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, milele na milele, Amina.
Ee Utatu Mtakatifu wa Mwenyezi Mungu, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, nasadiki kuwa upo hapa na mahali pote. Ee Mungu wangu, umeniumba, umenikomboa, umenifanya mkristo, umenizidishia neema zako hapa duniani, umenitayarishia makao yangu mbinguni, umenijalia na siku hii nikutumikie. Ee Mungu wangu! Nakuabudu, nakushukuru, nakuomba toba, nakupenda! Ee Mungu wangu, nakutolea roho yangu, na mawazo, na maneno, na kazi, na furaha, na mateso yangu: uyapokee unipe neema yako nisikutende leo dhambi!
Majitoleo ya Asubuhi
Ee Baba yetu Mungu Mkuu, Umenilinda usiku huu, Ninakushukuru kwa moyo, Ee Baba, Mwana na Roho, Nilinde tena siku hii, Niache dhambi nikutii, Naomba sana Baba wee, Baraka yako nipokee, Bikira safi ee Maria, Nisipotee unisimamie, Mlinzi Mkuu Malaika wee, Kwa Mungu wetu niombee, Nitake nitende mema tu, Na mwisho nije kwake juu, Amina.
Kuweka nia njema
Kumheshimu Mungu wangu, Namtolea roho yangu, Nifanye kazi nipumzike, Amri zake tu nishike, Wazo neno tendo lote, Namtolea Mungu pote, Roho, mwili chote changu, pendo na uzima wangu, Mungu wangu nitampenda, Wala dhambi sitatenda, Jina lako nasifia, Utakalo hutimia, Kwa utii navumilia, Teso na matata pia, Nipe Bwana neema zako, Niongezee sifa yako, Amina.
Majitoleo
Ee Yesu, kupitia mikono safi ya Bikira Maria, na kwa maungano na sadaka yako kuu, ninakutolea sala, matendo, kazi, masumbuko, na furaha zangu zote za siku hii ya leo, kwa ajili ya nia za Moyo wako Mtakatifu, Ee Yesu ufalme wako utufikie!
Baba Yetuβ¦.
Salamu Maria, β¦..
Nasadiki β¦β¦.
Amri za Mungu β¦β¦
Amri za Kanisa β¦β¦
Sala ya Malaika wa Bwana
Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria, naye akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Salamu Maria,β¦.
Ndimi Mtumishi wa Bwana, nitendewe ulivyonena. Salamu Maria, β¦β¦
Neno wa Bwana akatwaa Mwili, akakaa kwetu. Salamu Maria, β¦..
Utuombee, ee Mzazi Mtakatifu wa Mungu, tujaliwe ahadi za Kristo.
Tuombe:
Tunakuomba ee Bwana, utie neema yako mioyoni mwetu, ili sisi tuliojua kwa maelezo ya Malaika, kwamba, Kristo Mwanao amejifanya mtu: kwa mateso na Msalaba wake, utufikishe kwenye utukufu wa ufufuko. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu, Amina.
Sala kwa Malaika Mlinzi
Ee Malaika wangu, uliyewekwa na Mungu mwema unilinde, naomba uniongoze leo, unitunze, unisimamie, unishauri. Amina.
Sala kwa wenye kuzimia
Ee Yesu mwenye huruma, mpenda roho za watu, nakuomba kwa ajili ya kuzimia kwa Moyo wako Mtakatifu, na kwa ajili ya Mama Yako asiye na doa, uwatakase kwa damu yako, watu wote wenye dhambi wanaokufa sasa, na watakaokufa leo.
Moyo wa Yesu uliozomia, uwahurumie watu wanaokufa X3.
Sala kwa Mtakatifu Yosef
Ee Yosef mwenye heri, tunakimbilia kwako, katika masumbuko yetu, na kishaomba shime ya Mchumba wako Mtakatifu, tunaomba pia kwa matumaini usimamizi wako. Kwa ajili ya mapendo uliyompenda nayo Bikira Mtakatifu, Mzazi wa Mungu, na kwa ajili ya tunza ya Baba, uliyomtunza nayo Mtoto Yesu, tunakuomba sana, utuangalie kwa wema, sisi tuliokuwa fungu lake Yesu Kristo, tuliokombolewa kwa damu yake, utusimamie katika masumbuko yetu, kwa enzi na shime yako.
Ee Mlinzi amini wa Jamaa Takatifu, uwakinge watoto wateule wa Yesu Kristo, ee Baba uliyetupenda mno, utuepusha na kilema chochote cha madanganyo na upotevu. Ee kinga yetu mwezaji,utusimamie huko juu mbinguni ulipo, tunaposhindana na wenye nguvu wakaao gizani. Kama vile siku za kale ukamwokoa Mtoto Yesu katika hatari ya kuuawa, na leo hivi, ulikinge Kanisa Takatifu la Mungu katika mitego ya adui, na katika shida yote, mtunze daima kila mmoja wetu, tupate mfano wako, tusaidie kwa msaada wako, kukaa na utakatifu maisha, kufa kifo chema, na kupokelewa mbinguni makao ya raha milele. Amina
Sala kwa Mtakatifu Yuda Thadei
(Sala hii inaweza kusaliwa kila siku au kama Novena ya siku tisa mfululizo kuomba kitu kilekile)
Mtakatifu Yuda Tadei,/ Mtume Mtakatifu,/ Mtumishi mwaminifu na rafiki wa Yesu./ Jina la yule msaliti aliyemwuza Yesu/ limewafanya wengi wakusahau./ Walakini Kanisa zima linakuheshimu/ na kukuomba kama Msaidizi katika mashaka makubwa,/ na katika mambo yasiyo na matumaini tena./
Uniombee mimi mnyonge./ Ninaomba utumie uwezo ule uliojaliwa/ wa kuleta upesi msaada kwa watu walioukosa./ Unisaidie sasa katika mahitaji yangu,/ ili nipate kitulizo na msaada wa mbinguni/ katika lazima zangu,/ masumbuko na mateso,/ hasa/ (taja shida yako)./ Pia ili niweze kumsifu Mungu nawe na wateule wote milele./
Mtakatifu Yuda Tadei,/ utuombee,/ na uwaombee watu wote wanaokuheshimu na kukuomba msaada./
Baba yetuβ¦β¦. Salamu Maria β¦β¦β¦ Atukuzwe β¦β¦β¦.
Sala ya Medali ya Mwujiza
Ee Bikira Maria uliyekingiwa dhambi ya asili, utuombee sisi wenye kukimbilia kwako, uwaombee na wale wasioukimbilia kwako, hasa maadui wa Kanisa Takatifu, na wale waliokabidhiwa kwako. Amina.
Majitoleo kwa Bikira Maria
(Sala iliyotungwa na Mtk. Aloisi)
Bibi yangu mtukufu Maria, nakuwekea amana ya roho yangu na mwili wangu, nikikuomba uipokee amana yangu, kuitunzia ulinzi mwema ulinzi bora, ninakuaminia na kila neno langu, matumaini na kitulizo na kisongo chote, na masumbuko na uzima na ukomo wa uzima wangu: nitakayo ndiyo unifanyizie kwa maombezi na stahili zako, ili mambo yangu yote yapate kuongoka, yakiwa na kufuata mapenzi yako, pamoja na mapenzi ya Mwanao. Amina.
Grace Mligo (Guest) on June 21, 2024
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Lucy Wangui (Guest) on May 2, 2024
πβ€οΈ Mungu akubariki
Peter Otieno (Guest) on February 2, 2024
πβ€οΈπ Asante Mungu kwa uhai
Thomas Mwakalindile (Guest) on January 8, 2024
ππ Mbarikiwe sana
Irene Makena (Guest) on November 14, 2023
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Nancy Kawawa (Guest) on October 30, 2023
Mungu akubariki!
Miriam Mchome (Guest) on October 20, 2023
Baraka kwako na familia yako.
Victor Kimario (Guest) on October 8, 2023
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Carol Nyakio (Guest) on September 17, 2023
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Samuel Omondi (Guest) on August 23, 2023
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Wilson Ombati (Guest) on July 24, 2023
ππ Nakusihi Mungu
Frank Sokoine (Guest) on July 21, 2023
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Charles Mchome (Guest) on July 6, 2023
ππ Namuomba Mungu akupiganie
George Mallya (Guest) on May 28, 2023
Mwamini katika mpango wake.
Elizabeth Malima (Guest) on April 3, 2023
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Samson Mahiga (Guest) on March 8, 2023
ππ Mungu akujalie amani
Charles Wafula (Guest) on January 20, 2023
πβ¨ Mungu atupe nguvu
Esther Cheruiyot (Guest) on November 27, 2022
Nguvu hutoka kwa Bwana
Henry Mollel (Guest) on August 21, 2022
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Victor Malima (Guest) on June 29, 2022
Endelea kuwa na imani!
Elijah Mutua (Guest) on May 15, 2022
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Andrew Mchome (Guest) on March 11, 2022
πβ€οΈ Mungu ni mlinzi wetu
Nancy Kabura (Guest) on March 6, 2022
ππ Mungu alete amani
David Chacha (Guest) on February 19, 2022
Nakuombea π
Michael Mboya (Guest) on January 28, 2022
Sifa kwa Bwana!
Frank Macha (Guest) on December 4, 2021
ππβ¨ Neema yako ni ya kutosha
Joyce Nkya (Guest) on December 3, 2021
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Edwin Ndambuki (Guest) on August 30, 2021
Rehema zake hudumu milele
Edward Lowassa (Guest) on March 31, 2021
πβ€οΈβ¨ Mungu akujalie furaha
Janet Sumari (Guest) on March 18, 2021
πβ¨ Mungu asikie maombi yetu
Samuel Were (Guest) on January 7, 2021
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
John Lissu (Guest) on December 7, 2020
πππ Mungu akufunike na upendo
Anthony Kariuki (Guest) on November 5, 2020
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Joy Wacera (Guest) on October 24, 2020
Rehema hushinda hukumu
Alice Wanjiru (Guest) on August 21, 2020
πβ€οΈπ Baraka za Mungu ziwe nawe
Andrew Mahiga (Guest) on August 5, 2020
πβ€οΈ Mungu ni mwaminifu
Janet Mbithe (Guest) on April 21, 2020
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Victor Kimario (Guest) on March 24, 2020
ππ Nakushukuru Mungu
Joy Wacera (Guest) on February 26, 2020
Amina
Samson Mahiga (Guest) on January 21, 2020
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Betty Cheruiyot (Guest) on December 11, 2019
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Edith Cherotich (Guest) on October 12, 2019
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Nancy Kabura (Guest) on August 8, 2019
πβ€οΈ Mungu ni mkombozi
Sarah Mbise (Guest) on June 11, 2019
πβ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike
Betty Akinyi (Guest) on June 5, 2019
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Stephen Kangethe (Guest) on May 13, 2019
Tumaini ni nanga ya roho
Rose Lowassa (Guest) on May 3, 2019
πβ¨π Mungu atajibu maombi yako
James Kimani (Guest) on April 28, 2019
Dumu katika Bwana.
Lucy Wangui (Guest) on March 21, 2019
ππβ€οΈ Nakuombea heri
Josephine (Guest) on February 23, 2019
πππ
Edwin Ndambuki (Guest) on January 19, 2019
πππ« Mungu ni mwema
Joseph Mallya (Guest) on January 10, 2019
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Joyce Mussa (Guest) on November 2, 2018
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Samson Tibaijuka (Guest) on October 20, 2018
ππ Asante kwa neema zako Mungu
Edwin Ndambuki (Guest) on October 4, 2018
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Jane Malecela (Guest) on October 2, 2018
πβ€οΈβ¨ Asante Mungu kwa kila kitu
Agnes Njeri (Guest) on September 7, 2018
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Robert Ndunguru (Guest) on July 29, 2018
Neema ya Mungu inatosha kwako
Anna Mchome (Guest) on July 8, 2018
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Charles Mrope (Guest) on December 15, 2017
πβ€οΈπ Tumshukuru Mungu kwa yote