Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

SALA MUHIMU ZA MKRISTO ZA KILA SIKU ASUBUHI

Featured Image

SALA YA ASUBUHI

Tuusifu Utatu Mtakatifu wa Mungu Mwenyezi, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, milele na milele, Amina.

Ee Utatu Mtakatifu wa Mwenyezi Mungu, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, nasadiki kuwa upo hapa na mahali pote. Ee Mungu wangu, umeniumba, umenikomboa, umenifanya mkristo, umenizidishia neema zako hapa duniani, umenitayarishia makao yangu mbinguni, umenijalia na siku hii nikutumikie. Ee Mungu wangu! Nakuabudu, nakushukuru, nakuomba toba, nakupenda! Ee Mungu wangu, nakutolea roho yangu, na mawazo, na maneno, na kazi, na furaha, na mateso yangu: uyapokee unipe neema yako nisikutende leo dhambi!

Majitoleo ya Asubuhi

Ee Baba yetu Mungu Mkuu, Umenilinda usiku huu, Ninakushukuru kwa moyo, Ee Baba, Mwana na Roho, Nilinde tena siku hii, Niache dhambi nikutii, Naomba sana Baba wee, Baraka yako nipokee, Bikira safi ee Maria, Nisipotee unisimamie, Mlinzi Mkuu Malaika wee, Kwa Mungu wetu niombee, Nitake nitende mema tu, Na mwisho nije kwake juu, Amina.

Kuweka nia njema

Kumheshimu Mungu wangu, Namtolea roho yangu, Nifanye kazi nipumzike, Amri zake tu nishike, Wazo neno tendo lote, Namtolea Mungu pote, Roho, mwili chote changu, pendo na uzima wangu, Mungu wangu nitampenda, Wala dhambi sitatenda, Jina lako nasifia, Utakalo hutimia, Kwa utii navumilia, Teso na matata pia, Nipe Bwana neema zako, Niongezee sifa yako, Amina.

Majitoleo

Ee Yesu, kupitia mikono safi ya Bikira Maria, na kwa maungano na sadaka yako kuu, ninakutolea sala, matendo, kazi, masumbuko, na furaha zangu zote za siku hii ya leo, kwa ajili ya nia za Moyo wako Mtakatifu, Ee Yesu ufalme wako utufikie!

Baba Yetu….
Salamu Maria, …..
Nasadiki …….
Amri za Mungu ……
Amri za Kanisa ……

Sala ya Malaika wa Bwana

Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria, naye akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Salamu Maria,….

Ndimi Mtumishi wa Bwana, nitendewe ulivyonena. Salamu Maria, ……
Neno wa Bwana akatwaa Mwili, akakaa kwetu. Salamu Maria, …..

Utuombee, ee Mzazi Mtakatifu wa Mungu, tujaliwe ahadi za Kristo.

Tuombe:

Tunakuomba ee Bwana, utie neema yako mioyoni mwetu, ili sisi tuliojua kwa maelezo ya Malaika, kwamba, Kristo Mwanao amejifanya mtu: kwa mateso na Msalaba wake, utufikishe kwenye utukufu wa ufufuko. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu, Amina.

Sala kwa Malaika Mlinzi

Ee Malaika wangu, uliyewekwa na Mungu mwema unilinde, naomba uniongoze leo, unitunze, unisimamie, unishauri. Amina.

Sala kwa wenye kuzimia

Ee Yesu mwenye huruma, mpenda roho za watu, nakuomba kwa ajili ya kuzimia kwa Moyo wako Mtakatifu, na kwa ajili ya Mama Yako asiye na doa, uwatakase kwa damu yako, watu wote wenye dhambi wanaokufa sasa, na watakaokufa leo.
Moyo wa Yesu uliozomia, uwahurumie watu wanaokufa X3.

Sala kwa Mtakatifu Yosef

Ee Yosef mwenye heri, tunakimbilia kwako, katika masumbuko yetu, na kishaomba shime ya Mchumba wako Mtakatifu, tunaomba pia kwa matumaini usimamizi wako. Kwa ajili ya mapendo uliyompenda nayo Bikira Mtakatifu, Mzazi wa Mungu, na kwa ajili ya tunza ya Baba, uliyomtunza nayo Mtoto Yesu, tunakuomba sana, utuangalie kwa wema, sisi tuliokuwa fungu lake Yesu Kristo, tuliokombolewa kwa damu yake, utusimamie katika masumbuko yetu, kwa enzi na shime yako.
Ee Mlinzi amini wa Jamaa Takatifu, uwakinge watoto wateule wa Yesu Kristo, ee Baba uliyetupenda mno, utuepusha na kilema chochote cha madanganyo na upotevu. Ee kinga yetu mwezaji,utusimamie huko juu mbinguni ulipo, tunaposhindana na wenye nguvu wakaao gizani. Kama vile siku za kale ukamwokoa Mtoto Yesu katika hatari ya kuuawa, na leo hivi, ulikinge Kanisa Takatifu la Mungu katika mitego ya adui, na katika shida yote, mtunze daima kila mmoja wetu, tupate mfano wako, tusaidie kwa msaada wako, kukaa na utakatifu maisha, kufa kifo chema, na kupokelewa mbinguni makao ya raha milele. Amina

Sala kwa Mtakatifu Yuda Thadei

(Sala hii inaweza kusaliwa kila siku au kama Novena ya siku tisa mfululizo kuomba kitu kilekile)
Mtakatifu Yuda Tadei,/ Mtume Mtakatifu,/ Mtumishi mwaminifu na rafiki wa Yesu./ Jina la yule msaliti aliyemwuza Yesu/ limewafanya wengi wakusahau./ Walakini Kanisa zima linakuheshimu/ na kukuomba kama Msaidizi katika mashaka makubwa,/ na katika mambo yasiyo na matumaini tena./
Uniombee mimi mnyonge./ Ninaomba utumie uwezo ule uliojaliwa/ wa kuleta upesi msaada kwa watu walioukosa./ Unisaidie sasa katika mahitaji yangu,/ ili nipate kitulizo na msaada wa mbinguni/ katika lazima zangu,/ masumbuko na mateso,/ hasa/ (taja shida yako)./ Pia ili niweze kumsifu Mungu nawe na wateule wote milele./
Mtakatifu Yuda Tadei,/ utuombee,/ na uwaombee watu wote wanaokuheshimu na kukuomba msaada./
Baba yetu……. Salamu Maria ……… Atukuzwe ……….

Sala ya Medali ya Mwujiza

Ee Bikira Maria uliyekingiwa dhambi ya asili, utuombee sisi wenye kukimbilia kwako, uwaombee na wale wasioukimbilia kwako, hasa maadui wa Kanisa Takatifu, na wale waliokabidhiwa kwako. Amina.

Majitoleo kwa Bikira Maria

(Sala iliyotungwa na Mtk. Aloisi)
Bibi yangu mtukufu Maria, nakuwekea amana ya roho yangu na mwili wangu, nikikuomba uipokee amana yangu, kuitunzia ulinzi mwema ulinzi bora, ninakuaminia na kila neno langu, matumaini na kitulizo na kisongo chote, na masumbuko na uzima na ukomo wa uzima wangu: nitakayo ndiyo unifanyizie kwa maombezi na stahili zako, ili mambo yangu yote yapate kuongoka, yakiwa na kufuata mapenzi yako, pamoja na mapenzi ya Mwanao. Amina.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Grace Mligo (Guest) on June 21, 2024

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Lucy Wangui (Guest) on May 2, 2024

πŸ™β€οΈ Mungu akubariki

Peter Otieno (Guest) on February 2, 2024

πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai

Thomas Mwakalindile (Guest) on January 8, 2024

πŸ™πŸŒŸ Mbarikiwe sana

Irene Makena (Guest) on November 14, 2023

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Nancy Kawawa (Guest) on October 30, 2023

Mungu akubariki!

Miriam Mchome (Guest) on October 20, 2023

Baraka kwako na familia yako.

Victor Kimario (Guest) on October 8, 2023

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Carol Nyakio (Guest) on September 17, 2023

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Samuel Omondi (Guest) on August 23, 2023

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Wilson Ombati (Guest) on July 24, 2023

πŸ™πŸ’– Nakusihi Mungu

Frank Sokoine (Guest) on July 21, 2023

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Charles Mchome (Guest) on July 6, 2023

πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie

George Mallya (Guest) on May 28, 2023

Mwamini katika mpango wake.

Elizabeth Malima (Guest) on April 3, 2023

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Samson Mahiga (Guest) on March 8, 2023

πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani

Charles Wafula (Guest) on January 20, 2023

πŸ™βœ¨ Mungu atupe nguvu

Esther Cheruiyot (Guest) on November 27, 2022

Nguvu hutoka kwa Bwana

Henry Mollel (Guest) on August 21, 2022

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Victor Malima (Guest) on June 29, 2022

Endelea kuwa na imani!

Elijah Mutua (Guest) on May 15, 2022

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Andrew Mchome (Guest) on March 11, 2022

πŸ™β€οΈ Mungu ni mlinzi wetu

Nancy Kabura (Guest) on March 6, 2022

πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani

David Chacha (Guest) on February 19, 2022

Nakuombea πŸ™

Michael Mboya (Guest) on January 28, 2022

Sifa kwa Bwana!

Frank Macha (Guest) on December 4, 2021

πŸ™πŸ’–βœ¨ Neema yako ni ya kutosha

Joyce Nkya (Guest) on December 3, 2021

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Edwin Ndambuki (Guest) on August 30, 2021

Rehema zake hudumu milele

Edward Lowassa (Guest) on March 31, 2021

πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha

Janet Sumari (Guest) on March 18, 2021

πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu

Samuel Were (Guest) on January 7, 2021

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

John Lissu (Guest) on December 7, 2020

πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo

Anthony Kariuki (Guest) on November 5, 2020

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Joy Wacera (Guest) on October 24, 2020

Rehema hushinda hukumu

Alice Wanjiru (Guest) on August 21, 2020

πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe

Andrew Mahiga (Guest) on August 5, 2020

πŸ™β€οΈ Mungu ni mwaminifu

Janet Mbithe (Guest) on April 21, 2020

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Victor Kimario (Guest) on March 24, 2020

πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu

Joy Wacera (Guest) on February 26, 2020

Amina

Samson Mahiga (Guest) on January 21, 2020

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Betty Cheruiyot (Guest) on December 11, 2019

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Edith Cherotich (Guest) on October 12, 2019

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Nancy Kabura (Guest) on August 8, 2019

πŸ™β€οΈ Mungu ni mkombozi

Sarah Mbise (Guest) on June 11, 2019

πŸ™βœ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike

Betty Akinyi (Guest) on June 5, 2019

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Stephen Kangethe (Guest) on May 13, 2019

Tumaini ni nanga ya roho

Rose Lowassa (Guest) on May 3, 2019

πŸ™βœ¨πŸ’– Mungu atajibu maombi yako

James Kimani (Guest) on April 28, 2019

Dumu katika Bwana.

Lucy Wangui (Guest) on March 21, 2019

πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri

Josephine (Guest) on February 23, 2019

πŸ™πŸ™πŸ™

Edwin Ndambuki (Guest) on January 19, 2019

πŸ™πŸ’–πŸ’« Mungu ni mwema

Joseph Mallya (Guest) on January 10, 2019

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Joyce Mussa (Guest) on November 2, 2018

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Samson Tibaijuka (Guest) on October 20, 2018

πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu

Edwin Ndambuki (Guest) on October 4, 2018

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Jane Malecela (Guest) on October 2, 2018

πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu

Agnes Njeri (Guest) on September 7, 2018

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Robert Ndunguru (Guest) on July 29, 2018

Neema ya Mungu inatosha kwako

Anna Mchome (Guest) on July 8, 2018

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Charles Mrope (Guest) on December 15, 2017

πŸ™β€οΈπŸ’– Tumshukuru Mungu kwa yote

Related Posts

SALA WAKATI WA KUJIBARIKI NA MAJI YA BARAKA

SALA WAKATI WA KUJIBARIKI NA MAJI YA BARAKA

Kwa njia ya Maji haya ya Baraka,

na kwa njia ya Damu yako azizi,

na kwa maombezi ya M... Read More

SALA KWA MT. YOSEFU KWA WASIO NA AJIRA WAPATE AJIRA

SALA KWA MT. YOSEFU KWA WASIO NA AJIRA WAPATE AJIRA

Ee Mt. Yosefu, tunakuomba kwa ajili ya wale asio na ajira, kwa ajili ya wale wanaotaka kujipatia ... Read More

SALA YA KUANGUKA MIGUUNI PA BWANA YESU KATIKA EKARISTI

SALA YA KUANGUKA MIGUUNI PA BWANA YESU KATIKA EKARISTI

Ee Yesu Mfungwa wa Upendo wa Mungu,/ ninapofikiri Upendo wako na jinsi ulivyojitolea kwa ajili ya... Read More

SALA YA UHAI KWA MT. YOSEFU

SALA YA UHAI KWA MT. YOSEFU

(Sala hii inafaa sana kwa ajili ya kutetea uhai wa watoto wachanga wakiwa tumboni mwa mama za... Read More

SALA YA JIONI

SALA YA JIONI

TUNAKUSHUKURU, EE MUNGU KWA MAPAJI YOTE ULIYOTUJALIA LEO AMINA


BABA YETU…………β... Read More

LITANIA YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

LITANIA YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie ... Read More

Majitoleo kwa Bikira Maria

Majitoleo kwa Bikira Maria

(Sala iliyotungwa na Mtk. Aloisi)
Bibi yangu mtukufu Maria, nakuwekea amana ya roho yangu na... Read More

ATUKUZWE BABA

ATUKUZWE BABA

Atukuzwe Baba
na Mwana
na Roho Mtakatifu
Kama mwanzo
na sasa,
na siku zo... Read More

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE 1

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE 1

Kwa ajili ya Baba Mtakatifu wetu ..(N); Bwana, umpe moyo wako wa uchungaji ... Read More

SALA KWA MTAKATIFU MIKAELI MALAIKA MKUU

SALA KWA MTAKATIFU MIKAELI MALAIKA MKUU

Mtakatifu Mikaeli Malaika Mkuu, utulinde katika vita, uwe kinga yetu katika maovu na maoteo ya sh... Read More

SALA YA BWANA: SALA YA BABA YETU

SALA YA BWANA: SALA YA BABA YETU

Baba yetu uliye mbinguni
Jina lako litukuzwe
Ufalme wako ufike
Utakalo lifanyikeRead More

SALA YA KUUABUDU MOYO MTAKATIFU WA YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA YA KUUABUDU MOYO MTAKATIFU WA YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

Kwa nguvu zangu zote za moyo wangu/ ninakuabudu ee Moyo Mtakatifu/ na Mwabudiwa sana,/ Moyo Mtaka... Read More