Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

SALA YA KUANGUKA MIGUUNI PA BWANA YESU KATIKA EKARISTI

Featured Image

Ee Yesu Mfungwa wa Upendo wa Mungu,/ ninapofikiri Upendo wako na jinsi ulivyojitolea kwa ajili yangu,/ nashindwa kuelewa./ Unaficha Ukuu wako usiofahamika/ na kujidhihirisha kwa ajili yangu mimi mnyonge./ Ee Mfalme wa utukufu,/ unaficha uzuri wako,/ lakini jicho la moyo wangu/ linapenya pazia na kuona Majeshi ya Malaika/ wakikuimbia kwa heshima bila kukoma/ na nguvu zote mbinguni zikikusifu bila mwisho zikisema:/ β€œMtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu..”/

Ni nani awezaye kufahamu Upendo wako/ na huruma yako isiyo na kipimo kwa ajili yetu!/ Ee Mfungwa wa Upendo,/ nafungia moyo wangu masikini/ kwenye Tabarnakulo hii/ ili niweze kukuabudu usiku na mchana bila mwisho./ Najua hakuna kizuizi/ na hata kama naonekana kukaa mbali,/ lakini moyo wangu u pamoja nawe/ katika ibada hii./ Hakuna kinachoweza kuzuia upendo wangu kwako./ Kwangu hakuna kizuizi chochote./

Ee Utatu Mtakatifu,/ Mungu Mmoja usiyegawanyika,/ utukuzwe kwa zawadi yako hii kuu/ na agano hili la huruma!/

Nakuabudu,/ Bwana na Muumba uliyefichika katika Sakramenti Takatifu!/ Ee Bwana,/ nakuabudu kwa kazi zote za mikono yako/ zinazonifunulia Hekima yako kuu,/ Wema wako na Huruma yako kuu./ Uzuri uliousambaza hapa/ Uzuri ulio nao Wewe mwenyewe/ ambaye U Uzuri usioelezeka;/ na ingawaje umejificha na kusitiri uzuri wako,/ jicho langu,/ kwa mwanga wa imani linafika kwako,/ na roho yangu inapata kumtambua Muumba wake/ aliye Uzuri usiopimika,/ ulio juu ya kila uzuri,/ na moyo wangu unazama kabisa katika sala ya kukuabudu./

Bwana wangu na Muumba wangu,/ wema wako wanitia moyo wa kuongea nawe,/ Huruma yako huondoa kiambaza/ kitenganishacho Muumba na kiumbe./ Furaha ya moyo wangu,/ ee Mungu, ni kuongea na Wewe./ Yote ambayo moyo wangu unayatamni nayapata kwako./ Hapa ndipo mwanga wako unaponiangaza akili yangu/ na kuiwezesha kukujua Wewe zaidi na zaidi/ – ndipo mikondo ya neema inapoutiririkia moyo wangu,/ ndipo roho yangu inapochota uzima wa milele./ Ee Bwana na Muumba wangu,/ licha ya mapaji yote haya,/ unajitoa mwenyewe kwangu,/ ili uweze kujiunganisha na kiumbe dhaifu na maskini./

Ee Kristu,/ nafurahi sana nionapo kwamba unapendwa/ na kwamba sifa na utukufu wako vinaongezwa/ hasa ya Huruma yako./ Ee Kristu,/ sitaacha kamwe kuutukuza wema wako na huruma yako,/ hadi dakika ya mwisho ya maisha yangu./ Kwa kila tone la damu yangu/ na kwa kila pigo la moyo wangu/ naitukuza Huruma yako./ Natamani kugeuzwa kabisa/ na kuwa utenzi wa utukufu wako./ Naomba siku ya kufa kwangu/ popote nitakapokuwa nimelala,/ pigo la mwisho la moyo wangu/ liwe utenzi mpendevu/ usifuo Huruma yako isiyo na kipimo./ Amina

(Na Mt. Faustina Kowalska).

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

John Mwangi (Guest) on June 10, 2024

πŸ™β€οΈπŸ’– Bwana akujalie baraka

Peter Tibaijuka (Guest) on April 13, 2024

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Robert Okello (Guest) on March 17, 2024

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Samson Mahiga (Guest) on February 12, 2024

Baraka kwako na familia yako.

Stephen Kikwete (Guest) on January 23, 2024

πŸ™β€οΈ Mungu akubariki

Alice Mwikali (Guest) on December 28, 2023

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Bernard Oduor (Guest) on September 13, 2023

Mwamini Bwana; anajua njia

Christopher Oloo (Guest) on September 9, 2023

πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha

Margaret Mahiga (Guest) on August 12, 2023

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Nancy Akumu (Guest) on April 29, 2023

Rehema hushinda hukumu

Rose Lowassa (Guest) on March 3, 2023

Tumaini ni nanga ya roho

Nora Kidata (Guest) on February 9, 2023

Dumu katika Bwana.

Edward Chepkoech (Guest) on January 17, 2023

Imani inaweza kusogeza milima

Christopher Oloo (Guest) on January 6, 2023

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Ann Awino (Guest) on December 11, 2022

Neema na amani iwe nawe.

Catherine Mkumbo (Guest) on November 14, 2022

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Chris Okello (Guest) on October 20, 2022

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Mariam Hassan (Guest) on October 14, 2022

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Alex Nakitare (Guest) on July 28, 2022

πŸ™βœ¨ Mungu atakuinua

Lucy Mushi (Guest) on July 14, 2022

πŸ™πŸ’– Nakusihi Mungu

Elijah Mutua (Guest) on July 10, 2022

πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani

Margaret Mahiga (Guest) on March 11, 2022

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Stephen Amollo (Guest) on February 11, 2022

πŸ™β€οΈ Mungu ni mlinzi wetu

Joy Wacera (Guest) on February 7, 2022

Mungu ni mwema, wakati wote!

Lucy Mushi (Guest) on January 29, 2022

Mungu akubariki!

Anna Mchome (Guest) on January 25, 2022

πŸ™πŸ™πŸ™

Lucy Mushi (Guest) on December 8, 2021

πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu

Philip Nyaga (Guest) on September 18, 2021

πŸ™βœ¨ Mungu atupe nguvu

John Kamande (Guest) on August 28, 2021

Rehema zake hudumu milele

Mercy Atieno (Guest) on August 24, 2021

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Tabitha Okumu (Guest) on August 18, 2021

πŸ™πŸ’–πŸ’« Mungu ni mwema

Frank Sokoine (Guest) on July 31, 2021

Amina

Patrick Mutua (Guest) on May 5, 2021

πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani

Irene Makena (Guest) on April 30, 2021

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Stephen Amollo (Guest) on April 29, 2021

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

David Musyoka (Guest) on March 22, 2021

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Mariam Kawawa (Guest) on March 22, 2021

πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo

Faith Kariuki (Guest) on November 23, 2020

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Edith Cherotich (Guest) on November 15, 2020

Katika imani, yote yanawezekana

Samuel Omondi (Guest) on September 29, 2020

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Paul Kamau (Guest) on August 14, 2020

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Mary Kidata (Guest) on August 9, 2020

Nguvu hutoka kwa Bwana

Violet Mumo (Guest) on August 2, 2020

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Betty Cheruiyot (Guest) on July 11, 2020

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Benjamin Masanja (Guest) on June 12, 2020

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Edith Cherotich (Guest) on May 16, 2020

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Francis Mtangi (Guest) on May 16, 2020

πŸ™πŸ’–βœ¨ Neema yako ni ya kutosha

Alex Nakitare (Guest) on April 3, 2020

πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu

Stephen Amollo (Guest) on March 7, 2020

πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu

Patrick Akech (Guest) on March 1, 2020

πŸ™βœ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku

Ruth Kibona (Guest) on January 18, 2020

πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri

Rose Amukowa (Guest) on December 26, 2019

πŸ™πŸŒŸ Mbarikiwe sana

Mercy Atieno (Guest) on December 22, 2019

πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai

Richard Mulwa (Guest) on December 17, 2019

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Monica Nyalandu (Guest) on August 30, 2019

πŸ™βœ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike

Janet Wambura (Guest) on March 23, 2019

πŸ™β€οΈ Mungu ni mwaminifu

Alice Mrema (Guest) on February 16, 2019

Endelea kuwa na imani!

Rose Lowassa (Guest) on December 31, 2018

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Grace Majaliwa (Guest) on December 2, 2018

πŸ™βœ¨ Neema ya Mungu iwe nawe

Frank Macha (Guest) on October 8, 2018

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Related Posts

Rozari ya Malaika Mkuu Mikaeli

Rozari ya Malaika Mkuu Mikaeli

Rozari ya Malaika Mkuu Mikaeli ni sala nzuri sana ya kumheshimu huyu Malaika Mkuu pamoja na makun... Read More

Litani ya Bikira Maria

Litani ya Bikira Maria

  • Bwana utuhurumie
  • Bwana utuhurumie
  • Kristo utuhurumie
  • Bwana utuhurumie... Read More
SALA YA MTU ALIYEKABILIWA NA MATATIZO MBALIMBALI

SALA YA MTU ALIYEKABILIWA NA MATATIZO MBALIMBALI

Ewe Mtakatifu Yuda Tadei,/ mtume mtukufu na shahidi wa Kristo,/ umesifika pote kwa wepesi wako wa... Read More

SALA YA KUMWOMBA MT. YOSEFU MSAADA (SALA KUU KWA MTAKATIFU YOSEFU)

SALA YA KUMWOMBA MT. YOSEFU MSAADA (SALA KUU KWA MTAKATIFU YOSEFU)

Ee Mt. Yosefu mwenye heri, tunakimbilia kwako katika masumbuko yetu, na kisha omba shime ya Mchum... Read More

SALA MBELE YA KITI CHA ENZI CHA MUNGU

SALA MBELE YA KITI CHA ENZI CHA MUNGU

Sali Atukuzwe 7 kwa heshima ya Malaika 7 wateule ujipatie neema ya kuepa dhambi mbaya saba na kut... Read More

Novena ya Siku tisa kwa Mtakatifu Agustino wa Hippo: Sala zote na Litania

Novena ya Siku tisa kwa Mtakatifu Agustino wa Hippo: Sala zote na Litania

Anza Novena hii tarehe 19 Agosti ili kumalizia tarehe 27 Agosti na kush... Read More

SALAMU MARIA

SALAMU MARIA

Salamu Maria
Umejaa neema
Bwana yu nawe
Umebarikiwa kuliko wanawake wote
Na Y... Read More

SALA YA BWANA: SALA YA BABA YETU

SALA YA BWANA: SALA YA BABA YETU

Baba yetu uliye mbinguni
Jina lako litukuzwe
Ufalme wako ufike
Utakalo lifanyikeRead More

SALA YA NOVENA YA SIKU TISA KWA MT. YOSEFU, YA ZAMANI, MIAKA 1900 ILIYOPITA

SALA YA NOVENA YA SIKU TISA KWA MT. YOSEFU, YA ZAMANI, MIAKA 1900 ILIYOPITA

Ee Mt. Yosefu, ambaye ulinzi wako ni mkubwa, wenye nguvu na wa haraka mbele ya Kiti cha Enzi cha ... Read More

AMRI ZA KANISA

AMRI ZA KANISA

1. HUDHURIA MISA TAKATIFU DOMINIKA NA SIKUKUU ZILZOAMRIWA

2. FUNGA SIKU YA JUMATANO YA MAJI... Read More

ROZARI YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

ROZARI YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Tumia tasbihi ya kawaida yenye chembe ndogo 53.

Kwenye Msalaba Sali:

... Read More
ROZARI, MATENDO NA LITANI YA MAMA BIKIRA MARIA

ROZARI, MATENDO NA LITANI YA MAMA BIKIRA MARIA

Read More