Ee Yesu Mfungwa wa Upendo wa Mungu,/ ninapofikiri Upendo wako na jinsi ulivyojitolea kwa ajili yangu,/ nashindwa kuelewa./ Unaficha Ukuu wako usiofahamika/ na kujidhihirisha kwa ajili yangu mimi mnyonge./ Ee Mfalme wa utukufu,/ unaficha uzuri wako,/ lakini jicho la moyo wangu/ linapenya pazia na kuona Majeshi ya Malaika/ wakikuimbia kwa heshima bila kukoma/ na nguvu zote mbinguni zikikusifu bila mwisho zikisema:/ βMtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu..β/
Ni nani awezaye kufahamu Upendo wako/ na huruma yako isiyo na kipimo kwa ajili yetu!/ Ee Mfungwa wa Upendo,/ nafungia moyo wangu masikini/ kwenye Tabarnakulo hii/ ili niweze kukuabudu usiku na mchana bila mwisho./ Najua hakuna kizuizi/ na hata kama naonekana kukaa mbali,/ lakini moyo wangu u pamoja nawe/ katika ibada hii./ Hakuna kinachoweza kuzuia upendo wangu kwako./ Kwangu hakuna kizuizi chochote./
Ee Utatu Mtakatifu,/ Mungu Mmoja usiyegawanyika,/ utukuzwe kwa zawadi yako hii kuu/ na agano hili la huruma!/
Nakuabudu,/ Bwana na Muumba uliyefichika katika Sakramenti Takatifu!/ Ee Bwana,/ nakuabudu kwa kazi zote za mikono yako/ zinazonifunulia Hekima yako kuu,/ Wema wako na Huruma yako kuu./ Uzuri uliousambaza hapa/ Uzuri ulio nao Wewe mwenyewe/ ambaye U Uzuri usioelezeka;/ na ingawaje umejificha na kusitiri uzuri wako,/ jicho langu,/ kwa mwanga wa imani linafika kwako,/ na roho yangu inapata kumtambua Muumba wake/ aliye Uzuri usiopimika,/ ulio juu ya kila uzuri,/ na moyo wangu unazama kabisa katika sala ya kukuabudu./
Bwana wangu na Muumba wangu,/ wema wako wanitia moyo wa kuongea nawe,/ Huruma yako huondoa kiambaza/ kitenganishacho Muumba na kiumbe./ Furaha ya moyo wangu,/ ee Mungu, ni kuongea na Wewe./ Yote ambayo moyo wangu unayatamni nayapata kwako./ Hapa ndipo mwanga wako unaponiangaza akili yangu/ na kuiwezesha kukujua Wewe zaidi na zaidi/ β ndipo mikondo ya neema inapoutiririkia moyo wangu,/ ndipo roho yangu inapochota uzima wa milele./ Ee Bwana na Muumba wangu,/ licha ya mapaji yote haya,/ unajitoa mwenyewe kwangu,/ ili uweze kujiunganisha na kiumbe dhaifu na maskini./
Ee Kristu,/ nafurahi sana nionapo kwamba unapendwa/ na kwamba sifa na utukufu wako vinaongezwa/ hasa ya Huruma yako./ Ee Kristu,/ sitaacha kamwe kuutukuza wema wako na huruma yako,/ hadi dakika ya mwisho ya maisha yangu./ Kwa kila tone la damu yangu/ na kwa kila pigo la moyo wangu/ naitukuza Huruma yako./ Natamani kugeuzwa kabisa/ na kuwa utenzi wa utukufu wako./ Naomba siku ya kufa kwangu/ popote nitakapokuwa nimelala,/ pigo la mwisho la moyo wangu/ liwe utenzi mpendevu/ usifuo Huruma yako isiyo na kipimo./ Amina
(Na Mt. Faustina Kowalska).
John Mwangi (Guest) on June 10, 2024
πβ€οΈπ Bwana akujalie baraka
Peter Tibaijuka (Guest) on April 13, 2024
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Robert Okello (Guest) on March 17, 2024
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Samson Mahiga (Guest) on February 12, 2024
Baraka kwako na familia yako.
Stephen Kikwete (Guest) on January 23, 2024
πβ€οΈ Mungu akubariki
Alice Mwikali (Guest) on December 28, 2023
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Bernard Oduor (Guest) on September 13, 2023
Mwamini Bwana; anajua njia
Christopher Oloo (Guest) on September 9, 2023
πβ€οΈβ¨ Mungu akujalie furaha
Margaret Mahiga (Guest) on August 12, 2023
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Nancy Akumu (Guest) on April 29, 2023
Rehema hushinda hukumu
Rose Lowassa (Guest) on March 3, 2023
Tumaini ni nanga ya roho
Nora Kidata (Guest) on February 9, 2023
Dumu katika Bwana.
Edward Chepkoech (Guest) on January 17, 2023
Imani inaweza kusogeza milima
Christopher Oloo (Guest) on January 6, 2023
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Ann Awino (Guest) on December 11, 2022
Neema na amani iwe nawe.
Catherine Mkumbo (Guest) on November 14, 2022
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Chris Okello (Guest) on October 20, 2022
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Mariam Hassan (Guest) on October 14, 2022
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Alex Nakitare (Guest) on July 28, 2022
πβ¨ Mungu atakuinua
Lucy Mushi (Guest) on July 14, 2022
ππ Nakusihi Mungu
Elijah Mutua (Guest) on July 10, 2022
ππ Mungu akujalie amani
Margaret Mahiga (Guest) on March 11, 2022
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Stephen Amollo (Guest) on February 11, 2022
πβ€οΈ Mungu ni mlinzi wetu
Joy Wacera (Guest) on February 7, 2022
Mungu ni mwema, wakati wote!
Lucy Mushi (Guest) on January 29, 2022
Mungu akubariki!
Anna Mchome (Guest) on January 25, 2022
πππ
Lucy Mushi (Guest) on December 8, 2021
ππ Nakushukuru Mungu
Philip Nyaga (Guest) on September 18, 2021
πβ¨ Mungu atupe nguvu
John Kamande (Guest) on August 28, 2021
Rehema zake hudumu milele
Mercy Atieno (Guest) on August 24, 2021
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Tabitha Okumu (Guest) on August 18, 2021
πππ« Mungu ni mwema
Frank Sokoine (Guest) on July 31, 2021
Amina
Patrick Mutua (Guest) on May 5, 2021
ππ Mungu alete amani
Irene Makena (Guest) on April 30, 2021
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Stephen Amollo (Guest) on April 29, 2021
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
David Musyoka (Guest) on March 22, 2021
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Mariam Kawawa (Guest) on March 22, 2021
πππ Mungu akufunike na upendo
Faith Kariuki (Guest) on November 23, 2020
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Edith Cherotich (Guest) on November 15, 2020
Katika imani, yote yanawezekana
Samuel Omondi (Guest) on September 29, 2020
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Paul Kamau (Guest) on August 14, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mary Kidata (Guest) on August 9, 2020
Nguvu hutoka kwa Bwana
Violet Mumo (Guest) on August 2, 2020
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Betty Cheruiyot (Guest) on July 11, 2020
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Benjamin Masanja (Guest) on June 12, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Edith Cherotich (Guest) on May 16, 2020
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Francis Mtangi (Guest) on May 16, 2020
ππβ¨ Neema yako ni ya kutosha
Alex Nakitare (Guest) on April 3, 2020
πβ¨ Mungu asikie maombi yetu
Stephen Amollo (Guest) on March 7, 2020
ππ Asante kwa neema zako Mungu
Patrick Akech (Guest) on March 1, 2020
πβ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku
Ruth Kibona (Guest) on January 18, 2020
ππβ€οΈ Nakuombea heri
Rose Amukowa (Guest) on December 26, 2019
ππ Mbarikiwe sana
Mercy Atieno (Guest) on December 22, 2019
πβ€οΈπ Asante Mungu kwa uhai
Richard Mulwa (Guest) on December 17, 2019
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Monica Nyalandu (Guest) on August 30, 2019
πβ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike
Janet Wambura (Guest) on March 23, 2019
πβ€οΈ Mungu ni mwaminifu
Alice Mrema (Guest) on February 16, 2019
Endelea kuwa na imani!
Rose Lowassa (Guest) on December 31, 2018
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Grace Majaliwa (Guest) on December 2, 2018
πβ¨ Neema ya Mungu iwe nawe
Frank Macha (Guest) on October 8, 2018
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe