Tumia Rozari ya Mateso Saba ya Bikira Maria iliyo na mafungu 7 yaani mateso 7 yenye Salamu Maria saba kwa kila teso.
TESO LA KWANZA
Mzee Simeoni aliagua kuwa Moyo wa Mama Maria utachomwa kwa upanga.
Tuombe neema ya kuvumilia mateso.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu β¦β¦β¦ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba β¦β¦
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA PILI
Maria na Yosefu walikimbilia Misri usiku ili kumficha Mtoto Yesu asiuawe na Herodi.
Tuombe neema ili miili yetu iwe kimbilio lake Yesu.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu β¦β¦β¦ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba β¦β¦
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA TATU
Mama Maria aliona uchungu sana Mtoto Yesu alipopotea kwa siku tatu.
Tuombe neema ya kudumu na Yesu mioyoni mwetu.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu β¦β¦β¦ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba β¦β¦
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA NNE
Mama Maria aliona uchungu sana alipokutana na Mwanae Yesu katika njia ya Msalaba.
Tuombe neema ya kudumu na Yesu siku zote.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu β¦β¦β¦ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba β¦β¦
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA TANO
Mama Maria aliona uchungu sana alipomwona Mwanae Yesu akisulibiwa Msalabani.
Tuombe neema ya kufa mikononi mwa Yesu na Maria.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu β¦β¦β¦ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba β¦β¦
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA SITA
Mama Maria aliona uchungu sana alipopakata maiti ya Mwanae Yesu baada ya kushushwa Msalabani.
Tuombe neema ya kutotenda dhambi.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu β¦β¦β¦ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba β¦β¦
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA SABA
Mama Maria aliona uchungu sana aliporudi nyumbani baada ya kumzika Mwanae Yesu
Tuombe neema ya kitulizo kwa Mama Maria.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu β¦β¦β¦ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba β¦β¦
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
Stephen Malecela (Guest) on April 9, 2019
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Stephen Mushi (Guest) on October 13, 2018
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Farida (Guest) on July 28, 2018
πππ
Robert Ndunguru (Guest) on June 13, 2018
ππ Neema za Mungu zisikose
Nora Lowassa (Guest) on March 16, 2018
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Victor Kimario (Guest) on February 11, 2018
Neema na amani iwe nawe.
Jane Muthoni (Guest) on October 5, 2017
ππ Mungu alete amani
Betty Akinyi (Guest) on August 18, 2017
Sifa kwa Bwana!
Elizabeth Mrope (Guest) on April 10, 2017
ππ Mbarikiwe sana
Joseph Kiwanga (Guest) on March 18, 2017
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Lydia Mahiga (Guest) on March 12, 2017
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
George Wanjala (Guest) on March 6, 2017
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Grace Mligo (Guest) on February 21, 2017
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Samson Mahiga (Guest) on December 22, 2016
ππ Nakusihi Mungu
Paul Ndomba (Guest) on September 11, 2016
Rehema zake hudumu milele
Lucy Wangui (Guest) on August 23, 2016
ππβ€οΈ Nakuombea heri
Frank Macha (Guest) on August 4, 2016
πβ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku
David Kawawa (Guest) on April 10, 2016
Rehema hushinda hukumu
Jane Muthoni (Guest) on January 28, 2016
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
David Sokoine (Guest) on December 11, 2015
πβ€οΈ Mungu akubariki
Stephen Kikwete (Guest) on August 5, 2015
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Patrick Akech (Guest) on June 6, 2015
ππ Mungu akujalie amani
Elizabeth Mrope (Guest) on May 22, 2015
πβ¨ Mungu atupe nguvu
Sarah Karani (Guest) on April 20, 2015
πππ