Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utusikie Kristo utusikilize
Baba wa mbinguni Mungu Utuhurumie
Mwana, Mkombozi wa dunia Mungu Utuhurumie
Roho Mtakatifu Mungu Utuhurumie
Utatu Mtakatifu Mungu mmoja Utuhurumie
Moyo wa Yesu Mwana wa Baba wa Milele Utuhurumie
Moyo wa Yesu uliotungwa na Roho Mtakatifu mwilini mwa Mama Bikira Maria Utuhurumie
Moyo wa Yesu ulioungana na Neno wa Mungu Utuhurumie
Moyo wa Yesu ulio na utukufu pasipo mfano Utuhurumie
Moyo wa Yesu, hekalu takatifu la Mungu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, hema la Yule aliye juu Utuhurumie
Moyo wa Yesu tanuru lenye kuwaka mapendo Utuhurumie
Moyo wa Yesu, nyumba ya Mungu na mlango wa Mbingu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, tanuru yenye kuwaka mapendo Utuhurumie
Moyo wa Yesu, chombo cha haki na upendo Utuhurumie
Moyo wa Yesu, unaojaa upendo na wema Utuhurumie
Moyo wa Yesu, kilindi cha fadhila zote Utuhurumie
Moyo wa Yesu, unaostahili sifa zote Utuhurumie
Moyo wa Yesu, unaotawala mioyo yote Utuhurumie
Moyo wa Yesu, zinamokaa hazina za hekima na elimu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uliopendelewa na Mungu Baba Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uliotuenezea maziada yake Utuhurumie
Moyo wa Yesu, mtamaniwa wa vilima vya milele Utuhurumie
Moyo wa Yesu, wenye uvumilivu na huruma nyingi Utuhurumie
Moyo wa Yesu, tajiri kwa wote wenye kukuomba Utuhurumie
Moyo wa Yesu, chemchemi ya uzima na utakatifu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, malipo kwa dhambi zetu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, ulioshibishwa matusi Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uliovunjika kwa sababu ya ubaya wetu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uliotii mpaka kufa Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uliochomwa kwa mkuki Utuhurumie
Moyo wa Yesu, chemchemi ya faraja zote Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uzima na ufufuo wetu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, amani na upatanisho wetu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, sadaka ya wakosefu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, unamokaa wokovu wao wenye kukutumaini Utuhurumie
Moyo wa Yesu, matumaini yao wenye kuzimia kwako Utuhurumie
Moyo wa Yesu, sababu ya furaha ya watakatifu wote Utuhurumie
Mwanakondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za dunia Utusamehe Bwana
Mwanakondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za dunia Utusikilize Bwana
Mwanakondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za dunia Utuhurumie
Kiongozi: Yesu mwenye Moyo mpole na mnyenyekevu,
Wote: Ufanye mioyo yetu ifanane na Moyo wako
TUOMBE: (W) Ee Mungu Mwenyezi milele, uuangalie Moyo wa mwanao mpendelevu, pia na heshima na malipo aliyokutolea kwa ajili ya wenye dhambi, uridhike, uwaondolee wenye kuomba toba kwako kwa njia ya huyo Mwanao Yesu Kristo anayeishi na kutawala nawe pamoja na Roho Mtakatifu, Mungu milele. Amina.
Mary Kidata (Guest) on February 17, 2017
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Margaret Mahiga (Guest) on December 15, 2016
πβ¨ Mungu asikie maombi yetu
Francis Njeru (Guest) on September 22, 2016
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Lucy Wangui (Guest) on August 11, 2016
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Mariam Kawawa (Guest) on July 8, 2016
Rehema hushinda hukumu
Stephen Amollo (Guest) on June 19, 2016
ππ Mungu wetu asifiwe
Mariam Kawawa (Guest) on April 23, 2016
πβ¨ Mungu atakuinua
John Lissu (Guest) on March 21, 2016
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Irene Akoth (Guest) on March 18, 2016
πππ Mungu akufunike na upendo
Patrick Kidata (Guest) on March 11, 2016
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Jackson Makori (Guest) on February 18, 2016
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Joseph Mallya (Guest) on December 23, 2015
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
John Kamande (Guest) on December 22, 2015
ππ Nakushukuru Mungu
Lucy Kimotho (Guest) on December 7, 2015
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Alice Mrema (Guest) on October 27, 2015
Mwamini Bwana; anajua njia
Robert Okello (Guest) on October 9, 2015
ππ Namuomba Mungu akupiganie
Mary Sokoine (Guest) on October 9, 2015
Endelea kuwa na imani!
Rose Lowassa (Guest) on July 26, 2015
πππ
James Malima (Guest) on July 25, 2015
Mungu ni mwema, wakati wote!
Rose Amukowa (Guest) on July 25, 2015
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Jane Muthui (Guest) on June 26, 2015
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
John Mwangi (Guest) on June 16, 2015
πβ€οΈβ¨ Mungu akujalie furaha
Alex Nyamweya (Guest) on April 12, 2015
πβ€οΈβ¨ Asante Mungu kwa kila kitu