ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA
Tumia Rozari ya Mateso Saba ya Bikira Maria iliyo na mafungu 7 yaani mateso 7 yenye Salamu Maria saba kwa kila teso.
TESO LA KWANZA
Mzee Simeoni aliagua kuwa Moyo wa Mama Maria utachomwa kwa upanga.
Tuombe neema ya kuvumilia mateso.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu ……… Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba ……
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA PILI
Maria na Yosefu walikimbilia Misri usiku ili kumficha Mtoto Yesu asiuawe na Herodi.
Tuombe neema ili miili yetu iwe kimbilio lake Yesu.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu ……… Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba ……
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA TATU
Mama Maria aliona uchungu sana Mtoto Yesu alipopotea kwa siku tatu.
Tuombe neema ya kudumu na Yesu mioyoni mwetu.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu ……… Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba ……
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA NNE
Mama Maria aliona uchungu sana alipokutana na Mwanae Yesu katika njia ya Msalaba.
Tuombe neema ya kudumu na Yesu siku zote.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu ……… Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba ……
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA TANO
Mama Maria aliona uchungu sana alipomwona Mwanae Yesu akisulibiwa Msalabani.
Tuombe neema ya kufa mikononi mwa Yesu na Maria.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu ……… Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba ……
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA SITA
Mama Maria aliona uchungu sana alipopakata maiti ya Mwanae Yesu baada ya kushushwa Msalabani.
Tuombe neema ya kutotenda dhambi.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu ……… Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba ……
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA SABA
Mama Maria aliona uchungu sana aliporudi nyumbani baada ya kumzika Mwanae Yesu
Tuombe neema ya kitulizo kwa Mama Maria.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu ……… Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba ……
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
LITANIA YA MAMA WA MATESO
Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utusikie – Kristo utusikilize
Mungu Baba wa Mbinguni, Utuhurumie
Mungu Mwana, Mkombozi wa dunia Utuhurumie
Mungu Roho Mtakatifu Utuhurumie
Utatu Mtakatifu Mungu MMoja Utuhurumie
Maria Mtakatifu Utuombee (iwe kiitikio)
Mama wa Mkombozi wetu,
Mama mwenye mateso,
Malkia wa mashahidi,
Mama wa wenye uchungu,
Mfariji wa wenye taabu,
Msaada wa wenye shida,
Mlinzi wa wenye upweke,
Nguvu ya dhaifu moyoni,
Makimbilio ya wakosefu,
Afya ya wagonjwa,
Matumaini ya wanaozimia,
Kwa ajili ya ufukara wako ulioona pangoni Bethlehemu, – Utusaidie ee Mama wa mateso (iwe kiitikio)
Kwa ajili ya mateso yako uliyoona katika uaguzi wa Simeoni,
Kwa ajili ya taabu zako ulizopata katika safari ya Misri,
Kwa uchungu wako, Mwanao alipopotea,
Kwa ajili ya huzuni yako Mwanao alipodhulumiwa,
Kwa ajili ya hofu yako Yesu alipokamatwa,
Kwa ajili ya uchungu wako ulipokutana na Yesu katika njia ya Msalaba,
Kwa ajili ya mateso ya Moyo wako aliposulibiwa,
Kwa ajili ya mateso yako makali Yesu alipokufa,
Kwa ajili ya kilio chako juu ya Mwanao mpenzi,
Kwa ajili ya uchungu wako penye kaburi la Mwanao,
Kwa ajili ya upweke wako baada ya maziko ya Mwanao,
Kwa ajili ya uvumilivu wako katika shida zote,
Katika uchungu wetu wote,
Katika ugonjwa na mateso,
Katika huzuni na shida,
Katika umaskini na upweke,
Katika mahangaiko na hatari,
Katika vishawisho vyote,
Katika saa ya kifo chetu,
Katika hukumu ya mwisho,
Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utusamehe ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utusikilize ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utuhurumie.
Kristo utusikie – Kristo utusikilize
Bwana utuhurumie – Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie.
Baba Yetu ….
Utuombee, ee Mama wa Mateso
Tujaliwe kupewa ahadi za Kristo.
TUOMBE: Ee Bwana Yesu Kristo, utusaidie sasa na saa ya kifo chetu msaada wa Bikira Maria Mama yako, ambaye moyo wake mtakatifu ulichomwa na upanga wa mateso ulipoteswa na kufa msalabani. Unayeishi na kutawala milele na milele. Amina.
SALA KWA BIKIRA MARIA KATIKA UKIWA WAKE
Nakusikitikia sana Mama Mtakatifu Maria kwa sababu ya ukiwa wako mkuu. Uchungu wako ulikuwa mkubwa sana ulipotazama mateso na kifo cha Mwana wako mpenzi. Muda ule uliweza kutuliz kidogo kwa sababu ya kumwona angali hai. Lakini je, baada ya kufa na kumzika? Sasa wewe ni mkiwa mkubwa mno! Uh, ukiwa wa pekee, uniombee mimi ninayempoteza mara nyingi kwa dhambi zangu. Unijalie nisimpoteze tena Yesu wangu kwa ubaya wa uvivu wangu, bali nimtumikie kiaminifu duniani hapa ili nimwone na kumfurahia milele mbinguni. Amina.
SALA YA MAJITOLEO KWA MAMA WA HUZUNI
Mama Mtakatifu, Mama wa Mungu na Malkia wa Mashahidi, leo nakuchagua Wewe uwe mfano wangu, mkingaji na mteteaji wangu. Naweka roho fukara katika moyo wako uliotobolewa na panga nyingi za mateso. Unipokee mimi niwe mtumishi wako wa pekee na mshiriki wa mateso yako. Nijalie nguvu niwe daima karibu na msalaba ule alikosulibiwa Yesu. Nakutolea nafsi yangu na mali yangu yote. Pokea kila tendo langu jema ukalisindikize kwa Mwanao, Mama, nifanye nistahili kuitwa mtumishi wa Maria, Simama karibu yangu katika matendo yangu yote ili yafanwe kwa sifa ya Mungu. Ulivyosimama karibu kabisa ya Mwanao alipokufa msalabani uwe karibu nami saa ya kufa kwangu. Nijalie niweze kutaja jina lako na la Mwana wako nikisema: “Yesu, Maria na Yosef mnisaidie saa ya kufa kwangu. Yesu, maria na Yosef, naomba nife kwa amani kati yenu!” . Amina.
SALA KWA MAMA WA UCHUNGU KUOMBA NEEMA YA PEKEE
Ee Mama mbarikiwa na Bikira mwenye uchungu, Malkia wa Mashahidi, uliyesimama chini ya msalaba na uliyemtazama Mwana wako akifa, unitazame kwa huruma ya kimama ninayekusikitikia. Kwa sababu ya upanga uliochoma moyo wako, kwa mateso ya maisha yako nakuomba uniangalie kwa wema ukasikilize maombi yangu. Nakuomba, ee Mama, uniombee daima kwa Mwana wako, najua hawezi kukuvyima wewe kitu chochote. Basi, ufanye, Moyo wa Mwanao ukubali kunijalia ombi langu hili …………………(taja ombi lako).
Maana nitamkimbilia nani katika mahitaji na misiba yangu isipokuwa kwako, ee Mama wa huruma? Wewe hasa unaweza kutusaidia sisi tulio bado katika bonde la machozi kwa sababu ulishiriki mateso ya Mwanao kutukomboa. Umtolee Yesu tone moja la Damu yake takatifu. Umkumbushe ya kuwa wewe ni matumaini, furaha na maisha yetu ukanipatie jambo ninalokuomba kwa Yesu Kristo, bwana wetu. Amina.
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
🙏❤️💖 Bwana akujalie baraka
🙏🌟 Namuomba Mungu akupiganie
🙏❤️ Mungu ni mwaminifu
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
🙏❤️💖 Baraka za Mungu ziwe nawe
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Nguvu hutoka kwa Bwana
🙏🌟 Neema za Mungu zisikose
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Mungu akubariki!
Mwamini Bwana; anajua njia
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Endelea kuwa na imani!
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
🙏❤️ Mungu akubariki
Baraka kwako na familia yako.
Nakuombea 🙏
🙏❤️🌟 Asante Mungu kwa uhai
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
🙏❤️✨ Mungu akujalie furaha
🙏❤️💖 Tumshukuru Mungu kwa yote
🙏🌟 Mungu alete amani
Amina
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
🙏💖 Nakushukuru Mungu
🙏✨❤️ Neema za Mungu zikufunike
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Neema ya Mungu inatosha kwako
🙏💖✨ Neema yako ni ya kutosha
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Rehema hushinda hukumu
Dumu katika Bwana.
🙏💖 Asante kwa neema zako Mungu
Sifa kwa Bwana!
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Imani inaweza kusogeza milima
Neema na amani iwe nawe.
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
🙏✨ Mungu atakuinua
🙏🌟 Mbarikiwe sana
Mwamini katika mpango wake.
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
🙏🙏🙏
🙏💖💫 Mungu ni mwema
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
🙏💖 Nakusihi Mungu
🙏🙏🙏
🙏🌟❤️ Nakuombea heri
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
🙏🌟 Mungu akujalie amani
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Rehema zake hudumu milele
🙏✨💖 Mungu atajibu maombi yako
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Tumaini ni nanga ya roho
🙏💖🙏 Mungu akufunike na upendo
🙏❤️ Mungu ni mkombozi
🙏✨ Mungu asikie maombi yetu
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
🙏✨❤️ Tumwombe Mungu kila siku
Katika imani, yote yanawezekana
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
🙏✨ Mungu atupe nguvu
🙏❤️✨ Asante Mungu kwa kila kitu
Kwa Mungu, yote yanawezekana
🙏❤️ Mungu ni mlinzi wetu
Mungu ni mwema, wakati wote!
🙏💖 Mungu wetu asifiwe
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
🙏✨ Neema ya Mungu iwe nawe
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni