Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utusikie – Kristo utusikilize
Mungu Baba wa Mbinguni, Utuhurumie
Mungu Mwana, Mkombozi wa dunia Utuhurumie
Mungu Roho Mtakatifu Utuhurumie
Utatu Mtakatifu Mungu MMoja Utuhurumie
Maria Mtakatifu Utuombee (iwe kiitikio)
Mama wa Mkombozi wetu,
Mama mwenye mateso,
Malkia wa mashahidi,
Mama wa wenye uchungu,
Mfariji wa wenye taabu,
Msaada wa wenye shida,
Mlinzi wa wenye upweke,
Nguvu ya dhaifu moyoni,
Makimbilio ya wakosefu,
Afya ya wagonjwa,
Matumaini ya wanaozimia,
Kwa ajili ya ufukara wako ulioona pangoni Bethlehemu, – Utusaidie ee Mama wa mateso (iwe kiitikio)
Kwa ajili ya mateso yako uliyoona katika uaguzi wa Simeoni,
Kwa ajili ya taabu zako ulizopata katika safari ya Misri,
Kwa uchungu wako, Mwanao alipopotea,
Kwa ajili ya huzuni yako Mwanao alipodhulumiwa,
Kwa ajili ya hofu yako Yesu alipokamatwa,
Kwa ajili ya uchungu wako ulipokutana na Yesu katika njia ya Msalaba,
Kwa ajili ya mateso ya Moyo wako aliposulibiwa,
Kwa ajili ya mateso yako makali Yesu alipokufa,
Kwa ajili ya kilio chako juu ya Mwanao mpenzi,
Kwa ajili ya uchungu wako penye kaburi la Mwanao,
Kwa ajili ya upweke wako baada ya maziko ya Mwanao,
Kwa ajili ya uvumilivu wako katika shida zote,
Katika uchungu wetu wote,
Katika ugonjwa na mateso,
Katika huzuni na shida,
Katika umaskini na upweke,
Katika mahangaiko na hatari,
Katika vishawisho vyote,
Katika saa ya kifo chetu,
Katika hukumu ya mwisho,
Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utusamehe ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utusikilize ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utuhurumie.
Kristo utusikie – Kristo utusikilize
Bwana utuhurumie – Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie.
Baba Yetu ….
Utuombee, ee Mama wa Mateso
Tujaliwe kupewa ahadi za Kristo.
TUOMBE: Ee Bwana Yesu Kristo, utusaidie sasa na saa ya kifo chetu msaada wa Bikira Maria Mama yako, ambaye moyo wake mtakatifu ulichomwa na upanga wa mateso ulipoteswa na kufa msalabani. Unayeishi na kutawala milele na milele. Amina.
🙏💖🙏 Mungu akufunike na upendo
🙏💖 Asante kwa neema zako Mungu
Amina
Wakati wa Mungu ni kamilifu
🙏❤️ Mungu ni mlinzi wetu
🙏✨💖 Mungu atajibu maombi yako
🙏✨ Mungu asikie maombi yetu
🙏❤️💖 Baraka za Mungu ziwe nawe
🙏🙏🙏
🙏❤️✨ Asante Mungu kwa kila kitu
🙏🙏🙏
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
🙏✨ Mungu atakuinua
🙏💖 Mungu wetu asifiwe
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
🙏❤️ Mungu ni mwaminifu
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
🙏🌟 Namuomba Mungu akupiganie
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
🙏🌟 Mungu alete amani
Mungu ni mwema, wakati wote!
🙏✨ Mungu atupe nguvu
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Dumu katika Bwana.
🙏✨❤️ Neema za Mungu zikufunike
Mungu akubariki!
Imani inaweza kusogeza milima
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
🙏❤️ Mungu akubariki
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
🙏❤️🌟 Asante Mungu kwa uhai
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Neema ya Mungu inatosha kwako
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Nguvu hutoka kwa Bwana
Nakuombea 🙏
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
🙏💖 Nakusihi Mungu
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
🙏❤️💖 Tumshukuru Mungu kwa yote
🙏💖💫 Mungu ni mwema
🙏❤️💖 Bwana akujalie baraka
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
🙏❤️ Mungu ni mkombozi
🙏🌟 Neema za Mungu zisikose
Baraka kwako na familia yako.
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Neema na amani iwe nawe.
Mwamini Bwana; anajua njia
Endelea kuwa na imani!
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Mwamini katika mpango wake.
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
🙏🌟❤️ Nakuombea heri
Katika imani, yote yanawezekana
🙏✨❤️ Tumwombe Mungu kila siku
🙏💖 Nakushukuru Mungu
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
🙏✨ Neema ya Mungu iwe nawe
Rehema zake hudumu milele
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Tumaini ni nanga ya roho
🙏🌟 Mungu akujalie amani
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
🙏❤️✨ Mungu akujalie furaha
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Sifa kwa Bwana!
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
🙏🌟 Mbarikiwe sana
Rehema hushinda hukumu
🙏💖✨ Neema yako ni ya kutosha