1.Kuwaimbia binadamu.Yaani tupo kwa ajili ya kuimba ili tusifiwe na watu.
2.Kuimba bila tafakari.Mara nyingi tunaimba tu bila kuzingatia ujumbe Wa ule wimbo
3.Kuimba bila kusali!Yasemekana Kuimba ni kusali Mara mbili.Waimbaji wengi hukariri wimbo na nyimbo nyingi zimetungwa kwa njia ya sala lakini wanakwaya wengi huimba tu wala hali ya sala haimo ndani yao!
4.Walimu wenye hasira na ubinafsi.Mkufunzi Wa kwaya ni nguzo muhimu kwa maendeleo ya uimbaji.Iwapo choirmaster ni mwenye vurugu, mchochezi na mpenda fitina, bila shaka itakuwa vigumu kwa kwaya kupiga hatua kiuimbaji!
5.Sheria Kali zisizoenda na maadili ya kanisa.Kila jamii INA sheria zake na sheria ni nzuri.lakini tukiwa na sheria zinazowakandamiza wengine, tutapoteza kondoo wengi badala ya kuwaleta kwa Mungu!
6.Utoaji Wa albamu au kurekodi nyimbo kwa nia ya kutafuta pesa au kigezo kwa kwaya.Kwaya nyingi zimeanguka pindi tu wanapotoa albamu ya kwanza!Maana tunakosa kufahamu kuwa sisi ni wainjilisiti na tunawasaidia mapadri wetu kuhubiri injili.
7.Kutotii viongozi Wa kanisa.Wanakwaya wanaokosa kufahamu kuwa wapo chini ya viongozi na kanisa husika Mara nyingi hujipata wakiwa kwa makosa bila kunuia!
8.Kutoishi kwa hali ya sakramenti!Kama kuna jambo kubwa ambalo ibilisi hufurahia, ni yule MTU anayeishi katika maisha ya ndoa isiyo halali mbele za Mungu.Yaani Maana yake unaishi na mke au Mme bila ndoa ya kanisa na huna kizuizi chochote kinachokufanya usipate sakramenti hiyo.
9.Kitubio.Wengi tunapokea sakramenti ya ekaristi katika hali ya dhambi na hatushughuliki kabisaa kwenda kitubio.Hii inachochea zaidi kuwepo kwa dhambi za mazoea katika maisha yetu!
10.Kutosali kila siku.Inakuwa rahisi kwetu sisi kujaribiwa tukiwa hatusali.Kuimba kwako kunawasha hasira za shetani kwa hivo usiposali, bila shaka atarudi kulipiza kisasi.
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Nakuombea 🙏
Mwamini Bwana; anajua njia
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Neema ya Mungu inatosha kwako
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Nguvu hutoka kwa Bwana
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Endelea kuwa na imani!
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Rehema hushinda hukumu
Sifa kwa Bwana!
Katika imani, yote yanawezekana
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Mungu ni mwema, wakati wote!
Mwamini katika mpango wake.
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Rehema zake hudumu milele
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Imani inaweza kusogeza milima
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Baraka kwako na familia yako.
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Neema na amani iwe nawe.
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Dumu katika Bwana.
Mungu akubariki!
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Tumaini ni nanga ya roho