Ujana na Makuzi | Mapenzi na Ngono Salama

Ni katika umri gani vijana wana haki ya kujihusisha na mambo ya kujamiiana?

Kujamiiana ni uamuzi wa mtu binafsi. Ni uamuzi wako na hakuna
mtu yeyote mwenye haki ya kukuamulia. Lakini unapoamua
kujamiiana hakikisha kwamba ni maamuzi uliojulishwa na kwamba
unaelewa matokeo ya kujamiiana. Usisahau kuchukua hadhari
muhimu. kumbuka kutumia kondomu kujikinga wewe na mwenzi
wako kutokana na mimba usizotarajia na magonjwa kama vile
Virusi vya UKIMWI. Madhari mwili wako unaendelea kukua,
kujamiiana bila ya kondomu ni hatari zaidi kuliko mtu mzima,
kwa sababu maambukizo mengine haswa kwa vijana yanaweza
kukuletea matatizo kama vile ugumba baadaye katika maisha.
Pia jiulize mwenyewe kwa uangalifu kama kweli unataka
kujamiiana. Ni muhimu pia kujadiliana na mwenzi wako na kuwa
na hakika kama wote wawili mnataka kujamiiana. Usijamiiane
kwa sababu tu unafikiria kwamba watu wengine wanajamiiana
au unajitosa kwa kuwa unashawishiwa na marafiki au watu
wazima.

Ni umri gani ambapo vijana wanapaswa kuelezwa juu ya afya ya uzazi na njia za uzazi wa mpango?

Vijana balehe wote wana haki ya kupata habari juu ya mambo yote
wanayoyapenda. Watoto wanavyokuwa, wanapitia mabadiliko ya
kimwili, hisia na ya kisaikolojia katika maisha yao. Watu wazima,
hasa wale wanaowasimamia watoto wanapaswa kuwapa habari
juu ya mabadiliko na jinsi yanavyoshawishi ukuaji wa kimwili na
hisia. Hii ni muhimu ifanyike muda wote na katika kila rika.
Vijana wana mahitaji mbalimbali kutegemea umri wao, katika
hatua ya ukuaji na mazingira, mvulana wa umri wa miaka 11 au
kijana wa miaka 18 watakuwa na shauku tofauti. Pi wavulana au
wasichana wana haja tofauti na hata vijana wawili wenye umri
na jinsia moja wanaweza kukua kwa kasi na njia tofauti.
Tofauti hizi zinahitaji
kutambuliwa na kushughulikiwa.
Ni muhimu
pia kutambua
kwamba mahitaji
haya yatabadilika
kadiri ya muda unavyoenda
na pia kuweza
kubadilika kwa
haraka sana. Kwa
mfano mtu anapokuwa
na mhemuko wa
kujisikia kujamiiana.
Kwa njia yoyote, watoto
wana haja ya
kupata habari juu ya
uzazi kabla au mara
tu wapaoingia katika
ujana. Pia mada juu ya wajibu wa wavulana na wasichana katika
jamii, uhusiano na marafiki, na wazazi, uhusiano wa kijinsia na
matatizo yanayotokana na unyanyasaji wa kijinsia / ujinsia ni
muhimu yajadiliwe.
Iwapo vijana hawapati habari za kutosha juu ya mabadiliko ya
miili yao wanaweza kuingizwa katika matatizo ya kimaisha, ya
kijinsia na mimba yasiyotarajiwa au magonjwa yatokanayo na
kujamiiana pamoja na Virusi vya UKIMWI. Kwa hiyo wasichana
na wavulana wanahitaji kupata elimu ya ujinsia wanapokuwa vijana
wadogo. Hii ni pamoja na habari ya jinsi ya kujilinda wenyewe.
Siyo kweli kwamba elimu ya ujinsia inahimiza vijana wajamiiane.
Kinyume chake, wale vijana waliopata habari sahihi wanakuwa
na mwelekeo mzuri na wana uwezo wa kufanya maamuzi sahihi
. kama vile kuamua kuahirisha kujamiiana mpaka baadaye na
pia wanajilinda mara wanapoanza kujamiiana. Elimu ya Afya ya
Uzazi na Ujinsia ina habari juu ya uzuiaji wa mimba na kondomu.
Kabla ya kuanza kujamiiana inatakiwa vijana waelezwe kuhusu
njia za uzazi wa mpango na hasa jinsi ya kutumia kondomu kwa
sababu kondomu huzuia maambukizo ya Virusi vya UKIMWI
na magonjwa yatokanayo na kujamiiana. Jambo la busara ni
kwenda kliniki kwa ushauri katika suala zima la njia za uzazi wa
mpango mara tu ukiamua kuanza kujamiiana.

Haki za uzazi ni zipi?

Haki za binadamu ni haki zinazohusiana na mambo ya msingi na
asili ya uhuru na heshima ya ubinadamu ambapo watu wote wamepewa
haki ya kupata heshima kama
binadamu. Mara mtu azaliwapo
mume au mke hupata
haki hizi. Haki hizi
zinatambuliwa kimataifa
na zina usawa kwa watu
wote. Nchi mbalimbali
zimetia saini na kuidhinisha
haki hizi za kimataifa
na kufanya ni sehemu
ya sheria zao
pamoja na kuweka sera
zinazolinda haki hizi.

Haki za uzazi zina misingi yake katika haki za binadamu na pia
zinahusiana na haki za mtu mmojammoja.

Kupata habari juu ya ujinsia na mada zinazohusu afya
ya uzazi.

Mwanamke au mwanaume kuamua kwa uhuru na
kuwajibika, kama unataka kujamiaana lini na nani.
Uhuru wa maamuzi.

Kuamua kwa hiari na kuwajibika juu ya idadi na muda wa
kupishana katika kupata watoto.

Kupata huduma za afya ya uzazi kwa urahisi.

Haki za kufanya maamuzi kuhusu afya ya uzazi, kwa
uhuru, bila kunyanyaswa, kulazimishwa, bila kutumia
nguvu pamoja na maamuzi nani wa kufunga naye ndoa.

Kujilinda kutokana na mila zenye madhara kama vile
ukeketaji wa wanawake.

Haki hizi zimerekebishwa tangu mkutano uliofanyika Cairo mwaka
19941.

Afya ya uzazi ni nini?

Afya ya uzazi inahusiana na mfumo wa uzazi wa mtu, na via
vya uzazi kwa watu. Kwa hali hiyo basi inahusiana na mambo
yote yanayojumuisha uzazi na ujinsia. Ina maana kuwa watu
wana uwezo wa kukidhi mapenzi na usalama katika maisha
yao, kwamba watu wana uwezo wa kuwa na watoto na pia wana
uhuru wa kuamua, kama lini na kwa muda gani wapate watoto.
Yaliyomo humu yanampa haki mwanamume na mwanamke kupewa
habari au kuelekezwa na kufikiwa na njia za uzazi wa mpango
ambazo ni salama, zinazofanya kazi, anazomudu kulipia na njia
zinazokubalika za uzazi wa mpango alizochagua na haki ya kuwa
na huduma za afya zinazofaa ambazo zitawawezesha wanawake
kuwa salama wakati wa ujazito na kujifungua.

Ukweli kuhusu albino

  1. Je, ualbino unaambukiza? ……….. Hapana
  2. Ualbino ni ugonjwa? ………..Hapana
  3. Ualbino ni laana? ………..Hapana
  4. Ualbino ni kitu cha kawaida? ………..Hapana
  5. Ualbino unawapata tu watu weusi?……….. Hapana
  6. Watu wanaoishi na ualbino wana macho mekundu?……….. Hapana
  7. Albino ni watu wenye imani za ushirikina? ………..Hapana
  8. Albino wana nguvu za giza? ………..Hapana
  9. Je, Albino hawana akili? ………..Hapana
  10. Je, ni kosa la mwanamke anayezaa mtoto Albino? ………..Hapana
  11. Je, jamii ibadili mtazamo hasi iliyo nao kuhusu Albino?……….. NDIYO
Shopping Cart