Author name: SW - Melkisedeck Shine

Stori inayogusa!!

Habari ya mama aliyeuguliwa ghafla na mtoto wake majira ya SAA 2 usiku, mtoto alibanwa na kifua(asthma), hali ilikuwa mbaya na mama akaenda kuomba msaada kwa jirani yake aliyekuwa na gari, akamjibu gari haina mafuta, akaenda kwa mchungaji ili amsaidie, akamjibu nina wachungaji toka USA, hivyo sitaweza kuwaacha peke yao, mama hakuwa na jinsi aliamua kumbeba mtoto ili amuwahishe hospitali akiwa na hofu asije kufa kama baba yake aliyefariki miaka michache kwa ugonjwa huo.

 

Huyo mama alikuwa na tatizo la mguu na mtoto alikuwa mzito, mama alianguka Mara kadhaa na akainuka kuendelea na safari. Njiani alikutana na watu waliotoka kazini aliomba wamsaidie walimpuuza na alijaribu kusimamisha magari hayakusimama. Kichaa mmoja mchafu aliyekuwa akizungukazunguka mitaani na jalalani alipomuona yule mama anavyohangaika na mtoto akamwendea na kumchukua mtoto, kisha akamweka begani, mama hakuwa na la kusema ila kumwelekeza Hospitali, yule kichaa alielewa akaenda haraka hadi Hospitali. Ma doctor walipomuona yule kichaa na mtoto wakajua kuna dharura, wakamchukua mtoto na kumhudumia haraka, baada ya dk.10, mama wa mtoto akawasili, kisha ma doctor wakatoa taarifa kuwa, mtoto angecheleweshwa dk 5 angekufa. Mungu alimtumia yule kichaa mchafu kuokoa maisha ya mtoto. Hivyo usimteegemee Mch, jirani, wenye magari, matajiri nk. Mungu huweza kuinua MTU usiyemdhania kukubariki. Mwamini Mungu atakubariki. Usitumainie wanadamu hakuna baraka kwao. Mungu huinua vinyonge ilI kuangusha vyenye nguvu. Tuma ujumbe huu wa BARAKA kwa watu japo wanne ili kushiriki BARAKA hizi za Mungu, ujumbe huu waweza tena nitumia nami ktk kutakiana BARAKA za MUNGU WETU.

Kisa kilichombadilisha mume tabia

Mume alirejea nyumbani na kukuta ujumbe juu ya meza umeandikwa “NIMEONDOKA” ilikuwa jioni, alienda jikoni na kukuta kukavu, aliwaita watoto na kuwauliza wakasema walimuona Mama akiondoka na begi lakini hakuwaambia anaenda wapi. Mume alichanganyikiwa, alijaribu kuchukua simu kumpigia lakini ilikuwa haipatikani, kabla hajafanya chochote mtoto wao wa mwaka mmoja alikuja akilia na kusema ana njaaa.

Ilibidi kuingia jikono na kutaka kupika huku akitukana matusi yote, kila kitu kilikuwa hakuna, hapo ndipo alipokumbuka kua asubuhi mkewe alimuomba pesa ya kununua chakula akamuambia hana afanye maarifa. “Ataondokaje ghafla namna hii, huyu mwanamke mshenzi kabisa..” Aliwaza lakini alikumbuka kuwa asubuhi hiyo hiyo baada ya kumnyima mkewe pesa ya chakula mke alilalamika kua amechoka maisha yale na yeye akamjibu “Kama umkechoka si uondoke, wanawake wako wengi ukiondoa kitu na weka kitu…”

Akili yake iliwaza sana akakumbuka mchepuko wake, aliupigia simu uje nyumbani, lakini ulistuka kuhusu Mama watoto, akamuambia ameondoka na kamuachia watoto wote wa nne. Mchepuko ulijifanya hausikii vizuri na baada ya muda ukazima simu. Sasa alikuwa amechanganyikiwa, alitaka kupiga simu Kijijini ndipo alikumbuka kuwa hata namba ya Mama mkwe wake alikuwa hana, hakuwa na kawaida ya kuongea nao na mara chache alipoongea ni pale ambapo mkewe alipiga simu na kumuambia kuwa aongea na familia.

Alikumbuka ana namba ya rafiki wa mke wake, akampigia kumuuliza mkewe yuko wapi akasema hajui lakini mara ya mwisho alipompigia alimuambia kuwa “ANAENDA KUPUMZIKA”. Alizidi tena kutukana, alitoka jikoni nakuwachukua watoto kwenda kwenye mgahawa alizunguka nao mpaka kupata sehmu ya kula, watoto walifurahi sana siku hiyo kutoka na Baba yao, waliongea na kucheka kula nnje ya nyumbani, kidogo alipata faraja na kutabasmau lakini bado alikuwa akiwaza kuhusu mkewe.

Baada ya kumaliza chakula aliwarudisha watoto nyumbani alitaka kwenda kuwalaza lakini walikataa na kutaka kuogeshwa. Kimbembe kilianza katika kuwaogesha wale wadogo. walihtaji kuoga kwa maji ya moto, alienda moja kwa moja kuwasha jiko la umeme akakuta haliwaki. Akaanza kutukana ndipo alipokumbuka miezi mitatu iliyopita liliharibika na mkewe alipomuambia alisema watumie mkaa, akaenda kwenye jiko la gesi, hata hakuwasha kwani alikumbuka kuwa siku tatu zilizopita mkewe alimuomba hela ya gesi akamtukana mwanamke gani mvivu kuwasha mkaa, anatumia tu hela wakati hana chakufanya.

Alichanganyikiwa zaidi, akaenda kuwalaza watoto kwa lazima lakini ile na yeye anapanda kitandani mtoto mdogo akaanza kulia kwa sauti ya juu, joto, alitaka kuoga, ilibidi kunyanyuka kutaka kuwasha mkaa, atauwashaje hata mafuta ya taa hajui yako wapi labda angeweka ili uwake. Ilibidi kunyanyuka kuwasha TV watoto waliangalia mpaka walipopitiwa na usingizi, hata hakuwanyanyua yeye na watoto walilala, pale pale kwenye kochi mpaka asubuhi. Wote walipitiwa, asubuhi alistuka ameichelewa kazini na watoto walitakiwa kuandaliwa kwaajili ya shule.

Kichwa kilizidi kumuuma, hakujua aanzie wapi aishie wapi, akanunue vitafunwa au apike chai lakini atapika na nini? Akawaambia siku hiyo hakuna kwenda shule, akawasha gari kwenda kununua gesi na vitu vya nyumbani. Bado mkewe alikuwa hapatikani. alinunua jiko na kuja kupika chai akawapa watoto, akaanza kumtumia meseji mkewe za kumuomba msamaha, kumuomba arejee nyumbani kwani peke yake asingeweza kuwale watoto lakini meseji hasikupokelewa.

Simu ilianza kuita, ilikuwa namba ya bosi wake, alikuwa akimhitaji kupeleka taarifa ofisini, aliamua kumtafuta mdogo wake aje akae na wanae lakini naye alikuwa bize na kazi zake. Ili bidi kuwaacha watoto nyumbani na kwenda ofisini hivyo hivyo. Alifika ofisini na kukabidhi taarifa, baada ya muda meseji simu ilipiga kelele kuashiria kuwa meseji alizomtumia mkewe ziliingia, simu ilikuwa imewashwa.

Harakaharaka alinyanyua simu na kupiga, ilipopokelewa alianza kuomba msamaha aliongea maneno mengi ya kujilaumu na kumtaka mkewe kurejea nyumbani. “Wewe ndiyo mume wake?” Upande wapili uliuliza. “Ndiyo! Ndiyo Mimi! Kuna nini kimetokea! Mke wangu kafanya nini?” Aliuliza maswali mfululizo lakini kwa utaratibu upande wapili ulisikika unasema “MImi ni nesi nipo hapa Temeke Hospital mwenye hii simu ame…”

Hakusubiri wala amalizie alianza kupiga kelele kulia kwa uchungu, nguvu zilimuishia na kukaa juu ya kochi la mapokezi. Wafanyakazi wenzake walimsogelea kutaka kujua ni nini, bado alikuwa ameshikilia simu, walichukua na kuongea na mtu wa upende wapili. Baada ya muda alisikia wakimuambia “Unalia nini sasa yaani baada ya ufurahi unalia, Hongera mke wako amejifungua mtoto wa kiume..” Alishtuka sana kwani alihisi ni kitu kibaya, hapo ndipo alipokumbuka kuwa mke wake alikuwa mjamzito.

Alikuwa akimuona kila siku lakini kwakuwa alikua hajali hata alikuwa hajui kuwa ujauzito wa mkewe ulikuwa na muda gani? Akili yake ilishatekwa na mchepuko kiasi cha kuisahau familia yake. Aliendelea kulia kwa uchungu uliokuwa umechanganyika na furaha, alifurahia kuwa mkewe yuko salama lakini alipata uchungu kwa ukatili wake kiasi kwamba ameshaau hata kua mkewe alikuwa amekaribia kujifungua.

Haraka haraka aliingia kwenye gari, akaenda hospitallini kumuomba mkewe msamaha,. watuwa lishangaa kumuona amepiga magoti analia kama mtoto mdogo. mkewe alimuambia nilishjakusamehe muda mrefu, naamini sasa unafahamu thamani ya familia. Alinyanyuka na kukuabli kweli sasa anafahamu maana ya familia, siku ile amejifunza mengi kuliko mambo aliyokuwa amejifunza kwa maisha yake yote. Wlikumbatiana na baada ya kuruhusiwa alirejea nyumbani kwake na mkewe, alibadili tabia na kuwa Mume na baba bora.

MWISHO

Shopping Cart