Author name: DIN - Melkisedeck Leon Shine

MASOMO YA MISA, MEI 21, 2023:
DOMINIKA YA 7 YA PASAKA
SHEREHE YA KUPAA BWANA

MWANZO:
Mdo. 1:11

Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Atakuja vivyo hivyo mlivyomwona akienda zake mbinguni, Aleluya.

SOMO 1

Mdo. 1:1-11

Kitabu kile cha kwanza nalikiandika, Theofilo, katika habari ya mambo yote aliyoanza Yesu kufanya na kufundisha, hata siku ile alipochukuliwa juu, alipokuwa amekwisha kuwaagiza kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua; wale aliowadhihirishia nafsi yake, kwa dalili nyingi, baada ya kuteswa kwake, ya kwamba yu hai, akiwatokea muda wa siku arobaini, na kuyanena mambo yaliyouhusu ufalme wa Mungu. Hata alipokuwa amekutana nao aliwaagiza wasitoke Yerusalemu, bali waingoje ahadi ya Baba, ambayo mlisikia habari zake kwangu; ya kwamba Yohane alibatiza kwa maji, bali ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu baada ya siku hizi chache.

Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli ufalme? Akawaambia, Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe. Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.

Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, akainuliwa, wingu likampokea kutoka machoni pao. Walipokuwa wakikaza macho mbinguni, yeye alipokuwa akienda zake, tazama, watu wawili wakasimama karibu nao, wenye nguo nyeupe, wakasema, Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 47 : 1-2, 5-6, 7-8, (K) 5

(K) Mungu amepaa kwa kelele za shangwe, Bwana kwa sauti ya baragumu. au: Aleluya

Enyi watu wote, pigeni makofi,
Mpigieni Mungu kelele kwa sauti ya shangwe,
Kwa kuwa Bwana Aliye juu, mwenye kuogofya,
Ndiye mfalme mkuu juu ya dunia yote. (K)

Mungu amepaa kwa kelele za shangwe,
Bwana kwa sauti ya baragumu.
Mwimbieni Mungu, naam, imbeni;
Mwimbieni mfalme wetu, naam, imbeni. (K)

Maana Mungu ndiye mfalme wa dunia yote,
Imbeni kwa akili.
Mungu awamiliki mataifa,
Mungu ameketi katika kiti chake kitakatifu. (K)

SOMO 2

Efe 1 : 17-23

Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu, awape ninyi roho ya hekima na ya ufunuo katika kumjua yeye; macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo; na ubora wa ukuu wa uweza wake ndani yetu tuaminio jinsi ulivyo; kwa kadiri ya utendaji wa nguvu za uweza wake; aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia; akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

SHANGILIO

Mt. 28:19-20

Aleluya, aleluya,
Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, na tazama, mimi nipo pamoja nanyi sikuzote.
Aleluya.

INJILI

Mt. 28:16-20

Wale wanafunzi kumi na mmoja walikwenda Galilaya mpaka mlima ule aliowaagiza Yesu. Nao walipomwona, walimsujudia; lakini baadhi yao waliona shaka. Yesu akaja kwao, akasema nao, akawambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi sikuzote, hata ukamilifu wa dahari.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

MASOMO YA MISA, APRILI 2, 2023: DOMINIKA YA MATAWI

SOMO 1

Isa. 50:4 – 7

Bwana Mungu amenipa ulimi wa hao wafundishwao, nipate kujua jinsi ya kumtegemeza kwa maneno yeye aliyechoka, huniamsha asubuhi baada ya asubuhi; huniamsha, sikio langu lipate kusikia kama watu wafundishwao. Bwana Mungu amenizibua sikio langu, wala sikuwa mkaidi, wala sikurudi nyuma. Naliwatolea wapigao mgongo wangu, na wang’oao ndevu mashavu yangu; sikuficha uso wangu usipate fedheha na kutemewa mate. Maana Bwana Mungu atanisaidia; kwa sababu hiyo sikutahayari, kwa sababu hiyo nimekaza uso wangu kama gumegume, nami najua ya kuwa sitaona haya.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 22:7 – 8; 16 – 17a; 18 – 19; 22 – 23 (K)22:1

(K) Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?

Wote wanionao hunicheka sana

Hinifyonya, wakitikisa vichwa vyao;

Husema: Umtegemee Bwana; na amponye;

Na amwokoe sasa, maana apendezwa naye. (K)

Kwa maana mbwa wamenizunguka;

Kusanyiko la waovu wamenisonga;

Yamenizua mikono na miguu.

Naweza kuihesabu mifupa yangu yote. (K)

Wanagawanya nguo zangu,

Na vazi langu wanalipigia kura.

Nawe, Bwana, usiwe mbali,

Ee Mungu wangu, fanya haraka kunisaidia. (K)

Nitalihubiri jina lako kwa ndugu zangu,

Katikati ya kusanyiko nitakusifu.

Ninyi mnaomcha Bwana msifuni

Enyi nyote mlio wazao wa Yakobo, mtukuzeni. (K)

SOMO 2

Flp. 2:6 – 11

Ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.

Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa Yesu Kristo ni Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.

SHANGILIO

Flp. 2:8 – 9

Kristu alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba. Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina.

INJILI

Mt. 26: 14 – 27: 66

Wakati huo mmoja wa wale Thenashara, jina lake Yuda Iskariote, aliwaendea wakuu wa makuhani, akasema, Ni nini mtakachonipa, nami nitamsaliti kwenu? Wakampimia vipande thelathini vya fedha. Tokea wakati huo akawa akitafuta nafasi apate kumsaliti.

Hata siku ya kwanza ya mikate isiyotiwa chachu, wanafunzi wake wakamwendea Yesu, wakamwambia, Ni wapi utakapo tukuandalie uile Pasaka? Akasema, Enendeni mjini kwa mtu fulani, mkamwambie, Mwalimu asema, Majira yangu ni karibu; kwako nitafanya Pasaka pamoja na wanafunzi wangu. Wanafunzi wakafanya kama Yesu alivyowaagiza, wakaiandaa Pasaka.

Basi kulipokuwa jioni aliketi chakulani pamoja na wale Thenashara. Nao walipokuwa wakila, alisema, Amin, nawaambia, Mmoja wenu atanisaliti. Wakahuzunika sana, wakaanza kumwuliza mmoja mmoja, Ni mimi, Bwana? Akajibu akasema, Yeye aliyetia mkono wake pamoja nami katika kombe, ndiye atakayenisaliti. Mwana wa Adamu aenda zake, kama alivyoandikiwa; lakini ole wake mtu yule ambaye amsaliti Mwana wa Adamu! Ingekuwa heri kwake mtu yule kama asingalizaliwa. Yuda, yule mwenye kumsaliti, akajibu, akasema, Ni mimi, Rabi? Akamwambia, Wewe umesema.

Nao walipokuwa wakila Yesu alitwaa mkate, akabariki, akaumega, akawapa wanafunzi wake, akasema, Twaeni, mle; huu ndio mwili wangu Akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, akisema, Nyweni nyote katika hiki; kwa maana hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi. Lakini nawaambieni, Sitakunywa kabisa tangu sasa uzao huu wa mzabibu, hata siku ile nitakapokunywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu. Nao walipokwisha kuimba, wakatoka nje kwenda mlima wa Mizeituni.

Ndipo Yesu akawaambia, Ninyi nyote mtachukizwa kwa ajili yangu usiku huu kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika. Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya. Petro akajibu, akamwambia, Wajapochukizwa wote kwa ajili yako, mimi sitachukizwa kamwe. Yesu akamwambia, Amin, nakuambia wewe, usiku huu kabla ya kuwika jogoo, utanikana mara tatu. Petro akamwambia, Ijaponipasa kufa nawe, sitakukana kamwe. Na wanafunzi wote wakasema vivyo hivyo.

Kisha Yesu akaenda pamoja nao mpaka bustani iitwayo Gethsemane, akawaambia wanafunzi wake, Ketini hapa, hata niende kule nikaombe. Akamchukua Petro na wale wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuhuzunika na kusononeka. Ndipo akawaambia, Roho yangu ina huzuni nyingi kiasi cha kufa; kaeni hapa, mkeshe pamoja nami.

Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifulifuli, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke; walakini si kama nitakavyo mimi, bali kama utakavyo wewe. Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja? Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu. Akaenda tena mara ya pili, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwa haiwezekani kikombe hiki kiniepuke nisipokunywa, mapenzi yako yatimizwe. Akaja tena, akawakuta wamelala; maana macho yao yamekuwa mazito. Akawaacha tena, akaenda, akaomba mara ya tatu, akisema maneno yale yale.

Kisha akawajia wanafunzi wake, akawaambia, Laleni sasa, mpumzike tazama, saa imekaribia, na Mwana wa Adamu anatiwa katika mikono ya wenye dhambi. Ondokeni, twende zetuni! Tazama, yule anayenisaliti amekaribia. Basi alipokuwa katika kusema, tazama, Yuda, mmoja wa wale Thenashara akaja, na pamoja naye kundi kubwa wenye panga na marungu, wametoka kwa wakuu wa makuhani na wazee wa watu.

Na yule mwenye kumsaliti alikuwa amewapa ishara, akisema, Nitakayembusu, huyo ndiye; mkamateni. Mara akamwendea Yesu, akasema, Salamu, Rabi, akambusu. Yesu akamwambia, Rafiki, fanya ulilolijia. Wakaenda, wakanyosha mikono yao wakamkamata Yesu. Na tazama, mmoja wao waliokuwa pamoja na Yesu akanyosha mkono wake, akaufuta upanga wake, akampiga mtumwa wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio. Ndipo Yesu akamwambia, Rudisha upanga wako mahali pake, maana wote waushikao upanga, wataangamia kwa upanga. Ama wadhani ya kuwa mimi siwezi kumsihi Baba yangu, naye ataniletea sasa hivi zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika? Yatatimizwaje basi maandiko, ya kwamba hivyo ndivyo vilivyopasa kujiri? Saa ile Yesu akawaambia makutano, Je, mmetoka kama kumkamata mnyang’anyi, wenye panga na marungu, ili kunishika? Kila siku naliketi hekaluni nikifundisha, msinikamate. Lakini haya yote yamekuwa, ili maandiko ya manabii yatimizwe.

Ndipo wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia. Nao waliomkamata Yesu wakampeleka kwa Kayafa, Kuhani Mkuu, walikokuwa wamekutanika waandishi na wazee. Na Petro akamfuata kwa mbali mpaka behewa ya Kuhani Mkuu, akaingia ndani, akaketi pamoja na watumishi, auone mwisho.

Basi wakuu wa makuhani na baraza yote wakatafuta ushuhuda wa uongo juu ya Yesu, wapate kumwua; wasiuone wangawa walitokea mashahidi wa uongo wengi. Hata baadaye wawili wakatokea, wakasema, Huyu alisema, Naweza kulivunja hekalu la Mungu, na kulijenga kwa siku tatu. Kisha Kuhani Mkuu akasimama akamwambia, Hujibu neno? Hawa wanakushuhudia nini? Lakini, Yesu akanyamaza. Kuhani Mkuu akamwambia, Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, utuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu. Yesu akamwambia, Wewe umesema; lakini nawaambieni, Tangu sasa mtamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kuume wa nguvu, akija juu ya mawingu ya mbinguni.

Ndipo Kuhani Mkuu akararua mavazi yake, akisema, Amekufuru; mna haja gani tena ya mashahidi? Tazameni, sasa mmesikia hiyo kufuru yake; mwaonaje ninyi? Wakajibu, wakasema, Imempasa kuuawa. Ndipo wakamtemea mate ya uso, wakampiga makonde; wengine wakampiga makofi, wakisema, Ewe Kristo, tufumbulie; ni nani aliyekupiga? Na Petro alikuwa ameketi nje behewani; kijakazi mmoja akamwendea, akasema, Wewe nawe ulikuwapo pamoja na Yesu wa Galilaya. Akakana mbele ya wote, akisema, Sijui usemalo.

Naye alipotoka nje hata ukumbini, mwanamke mwingine alimwona, akawaambia watu waliokuwako huko, Huyu alikuwapo pamoja na Yesu Mnazareti. Akakana tena kwa kiapo, Simjui mtu huyu. Punde kidogo, wale waliohudhuria wakamwendea, wakamwambia Petro, Hakika wewe nawe u mmoja wao; kwa sababu hata usemi wako wakutambulisha. Ndipo akaanza kulaani na kuapa akisema, Simjui mtu huyu. Na mara akawika jogoo. Petro akalikumbuka lile neno la Yesu alilolisema, Kabla ya kuwika jogoo, utanikana mara tatu. Akatoka nje, akalia kwa majonzi. Na ilipokuwa asubuhi, wakuu wa makuhani wote na wazee wa watu wakafanya shauri juu ya Yesu, wapate kumwua; wakamfunga, wakamchukua, wakampeleka kwa Pilato aliyekuwa liwali.

Kisha Yuda, yule mwenye kumsaliti, alipoona ya kuwa amekwisha kuhukumiwa, alijuta, akawarudishia wakuu wa makuhani na wazee vile vipande thelathini vya fedha, akasema, Nalikosa nilipoisaliti damu isiyo na hatia. Wakasema, Basi, haya yatupasani sisi? Yaangalie haya wewe mwenyewe. Akavitupa vile vipande vya fedha katika hekalu, akaondoka; akaenda, akajinyonga. Wakuu wa makuhani wakavitwaa vile vipande vya fedha, wakasema, Si halali kuviweka katika sanduku ya sadaka, kwa kuwa ni kima cha damu.

Wakafanya shauri, wakavitumia kwa kununua konde la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni. Kwa hiyo konde lile huitwa konde la damu hata leo. Ndipo likatimia neno lililonenwa na nabii Yeremia, akisema, Wakavitwaa vipande thelathini vya fedha, kima chake aliyetiwa kima, ambaye baadhi ya Waisraeli walimtia kima; wakavitumia kwa kununua konde la mfinyanzi, kama Bwana alivyoniagiza.

Naye Yesu akasimama mbele ya liwali; liwali akamwuliza, akasema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Yesu akamwambia, Wewe wasema. Lakini aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu hata neno. Ndipo Pilato akamwambia, Husikii ni mambo mangapi wanayokushuhudia? Asimjibu hata neno moja, hata liwali akastaajabu sana. Basi wakati wa siku kuu, liwali desturi yake huwafungulia mkutano mfungwa mmoja waliyemtaka. Basi palikuwa na mfungwa mashuhuri siku zile, aitwaye Baraba. Basi walipokutanika, Pilato akawaambia, Mnataka niwafungulie yupi? Yule Baraba, au Yesu aitwaye Kristo? Kwa maana alijua ya kuwa wamemtoa kwa husuda.

Na alipokuwa ameketi juu ya kiti cha hukumu, mkewe alimpelekea mjumbe, kumwambia, Usiwe na neno na yule mwenye haki; kwa sababu nimeteswa mengi leo katika ndoto kwa ajili yake. Nao wakuu wa makuhani na wazee wakawashawishi makutano ili wamtake Baraba, na kumwangamiza Yesu. Basi liwali akajibu, akawaambia, Mnataka niwafungulie yupi katika hawa wawili? Wakasema, Baraba. Pilato akawaambia, Basi, nimtendeje Yesu aitwaye Kristo? Wakasema wote, Asulibiwe. Akasema, Kwani? Ni ubaya gani alioutenda? Wakazidi sana kupiga kelele, wakisema, Na asulibiwe. Basi Pilato alipoona ya kuwa hafai lo lote, bali ghasia inazidi tu, akatwaa maji, akanawa mikono yake mbele ya mkutano, akasema, Mimi sina hatia katika damu ya mtu huyu mwenye haki; yaangalieni haya ninyi wenyewe. Watu wote wakajibu wakasema, Damu yake na iwe juu yetu, na juu ya watoto wetu.

Ndipo akawafungulia Baraba; na baada ya kumpiga Yesu mijeledi, akamtoa ili asulibiwe. Ndipo askari wa liwali wakamchukua Yesu ndani ya Praitorio, wakamkusanyikia kikosi kizima. Wakamvua nguo, wakamvika vazi jekundu. Wakasokota taji ya miiba, wakaiweka juu ya kichwa chake, na mwanzi katika mkono wake wa kuume; wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki, wakisema, Salamu, Mfalme wa Wayahudi! Kisha wakamtemea mate, wakautwaa ule mwanzi, wakampiga-piga kichwani. Walipokwisha kumdhihaki, wakalivua lile vazi, wakamvika mavazi yake, wakamchukua kumsulibisha.

Hata walipokuwa wakitoka, wakamwona mtu Mkirene, jina lake Simoni; huyu wakamshurutisha auchukue msalaba wake. Na walipofika mahali paitwapo Golgotha, yaani, Fuvu la kichwa, wakampa kunywa divai iliyochanganyika na nyongo; lakini yeye alipoionja hakutaka kunywa. Walipokwisha kumsulibisha, waligawa mavazi yake, wakipiga kura; [ili litimie neno lililonenwa na nabii, Waligawa nguo zangu kati yao, na juu ya vazi langu walipiga kura.] Wakaketi, wakamlinda huko.

Wakaweka juu ya kichwa chake mashitaka yake, yaliyoandikwa HUYU NI YESU, MFALME WA WAYAHUDI. Wakati uo huo wanyang’anyi wawili wakasulibiwa pamoja naye, mmoja mkono wake wa kuume, na mmoja mkono wake wa kushoto. Nao waliokuwa wakipita njiani wakamtukana, wakitikisa-tikisa vichwa vyao, wakisema, Ewe mwenye kulivunja hekalu na kulijenga kwa siku tatu, jiokoe nafsi yako; ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, shuka msalabani. Kadhalika na wale wakuu wa makuhani wakamdhihaki pamoja na waandishi na wazee, wakisema, Aliokoa wengine, hawezi kujiokoa mwenyewe. Yeye ni mfalme wa Israeli; na ashuke sasa msalabani, nasi tutamwamini. Amemtegemea Mungu; na amwokoe sasa, kama anamtaka; kwa maana alisema, Mimi ni Mwana wa Mungu. Pia wale wanyang’anyi waliosulibiwa pamoja naye walimshutumu vile vile.

Basi tangu saa sita palikuwa na giza juu ya nchi yote hata saa tisa. Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Na baadhi yao waliohudhuria, waliposikia, walisema, Huyu anamwita Eliya. Mara mmoja wao akaenda mbio, akatwaa sifongo, akaijaza siki, akaitia juu ya mwanzi, akamnywesha. Wale wengine wakasema, Acha; na tuone kama Eliya anakuja kumwokoa. Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake.

Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka; makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala; nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, wakauingia mji mtakatifu, wakawatokea wengi. Basi yule akida, na hao waliokuwa pamoja naye wakimlinda Yesu, walipoliona tetemeko la nchi na mambo yaliyofanyika, wakaogopa sana, wakisema, Hakika huyu alikuwa Mwana wa Mungu.

Palikuwa na wanawake wengi pale wakitazama kwa mbali, hao ndio waliomfuata Yesu toka Galilaya, na kumtumikia. Miongoni mwao alikuwamo Mariamu Magdalene, na Mariamu mama yao Yakobo na Yusufu, na mama yao wana wa Zebedayo. Hata ilipokuwa jioni akafika mtu tajiri wa Arimathaya, jina lake Yusufu, naye mwenyewe alikuwa mwanafunzi wa Yesu; mtu huyu alimwendea Pilato akauomba mwili wa Yesu. Ndipo Pilato akaamuru apewe. Yusufu akautwaa mwili, akauzonga-zonga katika sanda ya kitani safi, akauweka katika kaburi lake jipya, alilokuwa amelichonga mwambani; akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango wa kaburi, akaenda zake. Na pale walikuwapo Mariamu Magdalene, na Mariamu yule wa pili, wameketi kulielekea kaburi.

Hata siku ya pili, ndiyo iliyo baada ya Maandalio, wakuu wa makuhani, na Mafarisayo wakamkusanyikia Pilato, wakasema, Bwana, tumekumbuka kwamba yule mjanja alisema, alipokuwa akali hai, Baada ya siku tatu nitafufuka. Basi amuru kwamba kaburi lilindwe salama hata siku ya tatu; wasije wanafunzi wake wakamwiba, na kuwaambia watu, Amefufuka katika wafu; na udanganyifu wa mwisho utapita ule wa kwanza. Pilato akawaambia, Mna askari; nendeni mkalilinde salama kadiri mjuavyo. Wakaenda, wakalilinda kaburi salama, kwa kulitia lile jiwe muhuri, pamoja na wale askari walinzi.

MASOMO YA MISA, APRILI 1, 2023: JUMAMOSI, JUMA LA 5 LA KWARESIMA

SOMO 1

Eze. 37:21 – 28

Bwana Mungu asema hivi: Tazama, nitawatwaa wana wa Israeli toka kati ya mataifa walikokwenda, nami nitawakusanya pande zote, na kuwaleta katika nchi yao wenyewe; nami nitawafanya kuwa taifa moja katika nchi hiyo, juu ya milima ya Israeli; na mfalme mmoja atakuwa mfalme wao wote; wala hawatakuwa tena mataifa mawili, wala hawatagawanyikana kuwa falme mbili tena, hata milele. Wala hawatajitia uchafu tena kwa vinyago vyao, wala kwa vitu vyao vichukizavyo, wala kwa makosa yao mmojawapo; lakini nitawaokoa, na kuwatoa katika makao yao yote, ambayo wamefanya dhambi ndani yake, nami nitawatakasa; basi watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao. Na mtumishi wangu, Daudi, atakuwa mfalme juu yao, nao wote watakuwa na mchungaji mmoja; nao wataenenda katika hukumu zangu, na kuzishika amri zangu, na kuzitenda. Nao watakaa katika nchi niliyompa Yakobo, mtumishi wangu, walimokaa baba zenu; nao watakaa humo, wao na watoto wao, na watoto wa watoto wao, milele; na Daudi, mtumishi wangu, atakuwa mkuu wao milele. Tena nitafanya agano la Amani pamoja nao; litakuwa agano la milele pamoja nao; naami nitaweka na kuwazidisha, na patakatifu pangu nitapaweka katikati yao milele. Tena maskani yangu itakuwa pamoja nao; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. Na mataifa watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, mimi niwatakasaye Israeli, patakatifu pangu patakapokuwa katikati yao milele.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI

Yer. 31:10 – 13 (K) 10

(K) Bwana anatulinda kama mchungaji alindavyo kundi lake.

Lisikieni neno la Bwana, enyi mataifa,

Litangazeni visiwani mbali;

Mkaseme: Aliyemtawanya Israeli atamkusanya,

Na kumlinda kama mchungaji alindavyo kundi lake.

Kwa maana Bwana amemweka huru Yakobo,

Amemkomboa mkononi mwake aliyekuwa hodari kuliko yeye. (K)

Watakuja na kuimba katika mlima Sayuni.

Wataukimbilia wema wa Bwana,

Nafaka, na divai, na mafuta,

Na wachanga wa kondoo na wa ng’ombe. (K)

Ndipo bikira atafurahi katika kucheza,

Na vijana na wazee pamoja;

Maana nitageuza masikitiko yao kuwa furaha,

Nami nitawafariji, na kuwafurahisha waache huzuni zao. (K)

SHANGILIO

Zab. 95:8 , 9

Leo msifanye migumu mioyo yenu, lakini msikie sauti yake Bwana.

INJILI

Yn. 11:45 – 57

Wengi katika Wayahudi waliokuja kwa Maria, na kuyaona yale aliyoyafanya Yesu, wakamwamini. Lakini wengine wakaenda zao kwa Mafarisayo, wakawaambia aliyoyafanya.

Basi wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakakusanya baraza, wakasema, Tunafanya nini? Maana mtu huyu afanya ishara nyingi. Tukimwacha hivi, watu wote watamwamini; na Warumi watakuja watamuondolea mahali petu na taifa letu. Mtu mmoja miongoni mwao, Kayafa, aliyekuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, akawaambia, Ninyi hamjui neno lolote; wala hamfikiri ya kwamba yafaa mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, wala lisiangamie taifa zima. Na neno hilo yeye hakulisema kwa nafsi yake; bali kwa kuwa alikuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, alitabiri ya kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa hilo, wala si kwa ajili ya taifa hilo tu; lakini pamoja na hayo awakusanye watoto wa Mungu waliotawanyika, ili waawe wamoja. Basi tangu siku ile walifanya shauri la kumwua.

Kwa hiyo Yesu hakutembea tena kwa wazi katikati ya Wayahudi; bali alitoka huko, akaenda mahali karibu na jangwa, mpaka mji uitwao Efraimu; akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.

Na Pasaka ya Wayahudi ilikuwa karibu; na wengi wakakwea toka mashambani kwenda Yerusalemu kabla ya Pasaka, ili wajitakase. Basi wao wakamtafuta Yesu, wakasemezana hali wamesimama hekaluni, Mwaonaje? Haji kabisa sikukuu hii? Na wakuu wa makuhani wa Mafarisayo walikuwa wametoa amri ya kwamba mtu akijua alipo, alete habari, ili wapate kumkamata.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo

Thamani ya Neno “Nimekusamehe”

Ni jambo jema kusamehe wale waliotukosea. Neno “Nimekusamehe” ni zuri kusikia masikioni kuliko neno “Ninakupenda”. Maana kusamehewa ni zaidi ya kupendwa kwani Msamaha ni matokeo ya Upendo.

Melkisedeck Leon Shine

Neno “Nimekusamehe”

Neno “Nimekusamehe” ni moja ya maneno yenye nguvu kubwa sana katika lugha yoyote ile. Ni neno ambalo linabeba uzito wa moyo mzito uliojaa maumivu na hatimaye kuachilia mzigo huo. Ni jambo jema kusamehe wale waliotukosea, kwani msamaha unafungua milango ya amani na upatanisho.

“Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi.” (Mathayo 6:14)
“Basi, vaeni kama wateule wa Mungu, watakatifu na wapendwao, moyo wa rehema, utu wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu; mkichukuliana na kusameheana, mtu akiwa na neno juu ya mwenzake. Kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi.” (Wakolosai 3:12-13)
“Msameheane, na kwa maana hiyo msisahau jinsi Yesu Kristo alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi msameheane.” (Waefeso 4:32)

Uzuri wa Kusamehewa

Neno “Nimekusamehe” ni zuri kusikia masikioni kuliko neno “Ninakupenda”. Maana yake ni kwamba, msamaha unaleta uzima wa moyo na uhuru wa ndani. Kila mtu anahitaji kusamehewa, na wakati mwingine msamaha una nguvu zaidi ya upendo wenyewe. Kwa maana kusamehewa ni zaidi ya kupendwa kwani msamaha ni matokeo ya upendo. Ni kupitia msamaha tunapata nafasi ya kuanza upya na kujenga mahusiano mapya yaliyojaa matumaini.

“Kwa maana nitatubia uovu wao, na dhambi yao sitaikumbuka tena.” (Yeremia 31:34)
“Naye asema, ‘Dhambi zao na uovu wao sitaukumbuka tena.'” (Waebrania 8:12) “Nanyi msifanye mambo ambayo mimi nimewaambia msifanye, bali ninyi pia msisahau kwamba, ikiwa ninyi mna uovu na msamaha, mimi pia ninasamehe na kuponya.”_ (Zaburi 103:3)

Msamaha: Daraja ya Upendo wa Kweli

Msamaha ni daraja inayoelekea kwenye upendo wa kweli. Bila msamaha, upendo hawezi kuwa kamili. Wakati tunapowapenda wengine, tunahitaji pia kujifunza kusamehe. Upendo usio na msamaha ni kama mti usio na mizizi, hauwezi kustawi na kuzaa matunda mazuri. Msamaha hufungua milango ya mawasiliano na kurejesha amani kati ya watu. Ni ishara ya kukubali udhaifu wa kibinadamu na kutambua kuwa sisi sote tunahitaji neema na rehema ya Mungu.

“Upendo hufunika wingi wa dhambi.” (1 Petro 4:8)
“Mwenye upendo huvumilia yote, huamini yote, hutumaini yote, hustahimili yote.” (1 Wakorintho 13:7)
“Kwa maana nimekasirika kiasi gani, kwamba nilipotaka huruma, ndipo nilipokasirika; lakini nikaachilia mbali upendo wangu, na hivyo nimesamehe.” (Mika 7:18)

Ukomavu Katika Imani na Msamaha

Kusamehe ni ishara ya ukomavu katika imani. Ni kuonyesha kwamba tumeelewa maana ya kweli ya upendo wa Kristo. Yesu alitufundisha umuhimu wa kusamehe kupitia maisha yake na kifo chake msalabani. Alisema, “Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui walitendalo.” (Luka 23:34). Huu ni mfano wa hali ya juu kabisa ya msamaha na upendo. Tunapomwiga Kristo kwa kusamehe wengine, tunaonyesha kwamba tumezama katika upendo wake na tumeamua kufuata njia yake.

“Wakati Petro alipomwambia Yesu, ‘Bwana, nikisamehe ndugu yangu mara ngapi? Hata mara saba?’ Yesu akamjibu, ‘Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.'” (Mathayo 18:21-22) “Nanyi mtasameheani bure kama Bwana alivyosameheani ninyi, pia nanyi msameheani kwa bure.”_ (Wakolosai 3:13)
“Tafuteni amani na kila mtu, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao.” (Waebrania 12:14)

Kusamehe ni zawadi ya kipekee ambayo tunaweza kupeana sisi kwa sisi. Inahitaji unyenyekevu, uvumilivu, na upendo wa kweli. Tukumbuke kila siku kuwa na moyo wa kusamehe na kujenga mahusiano yenye msingi wa upendo na msamaha. Kwa kufanya hivyo, tunaweza kuishi maisha yenye amani na furaha, tukifuata nyayo za Kristo ambaye alitufundisha maana ya kweli ya msamaha na upendo.

Kumtafuta Mungu ni Jukumu lako Binafsi

Kumtafuta Mungu ni jukumu la mtu binafsi na nafsi yake. Huwezi kumfuata Mungu kwa kufwata njia ya wengine. Njia yako ya kukuwezesha kumfikia Mungu ni tofauti na wengine, Kwa maana Mungu amemwita kila mtu kwa namna ya kipekee.

Melkisedeck Leon Shine

Kumtafuta Mungu: Jukumu la Mtu Binafsi

Kumtafuta Mungu ni jukumu la mtu binafsi na nafsi yake. Kila mmoja wetu ana safari ya kiroho inayomwita kumtafuta Mungu kwa njia yake mwenyewe. Safari hii ni ya kipekee na haifanani na ya mwingine yeyote. Mungu anatuita kila mmoja wetu kwa namna ya kipekee, akitufundisha na kutuongoza kupitia maisha yetu binafsi. Kumtafuta Mungu si jambo la jumuia au kanisa, bali ni uamuzi wa kibinafsi unaohitaji moyo wa kujitolea na utayari wa kipekee.

“Nitajitokeza kwenu, nanyi mtaniona; nanyi mtakaponiomba, nitasikiliza.” (Yeremia 29:12-13)
“Wakati unapotaka kujua mambo ya Mungu, basi mpe nafasi, naye atakujulisha siri zake.” (Amosi 3:7)
“Ee Mungu, Mungu wangu, nakutafuta asubuhi; roho yangu inakuonea kiu, mwili wangu unakutamani, katika nchi kame na yenye kuia, isiyo na maji.” (Zaburi 63:1)

Njia ya Kipekee ya Kumtafuta Mungu

Huwezi kumfuata Mungu kwa kufuata njia ya wengine. Ingawa tunaweza kupata mwongozo na msaada kutoka kwa wale walio karibu nasi katika jumuia au kanisa, ni muhimu kutambua kuwa kila mtu ana njia yake ya kumfikia Mungu. Njia yako ya kukuwezesha kumfikia Mungu ni tofauti na wengine. Hii ni kwa sababu Mungu amemwita kila mtu kwa namna ya kipekee. Katika ulimwengu huu wa tofauti na utofauti, Mungu anazungumza nasi kwa njia ambazo zinaendana na maisha yetu binafsi na hali zetu za kipekee. Hili ni jambo la kibinafsi na si suala la jumuia au kanisa.

“Kwa maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu, asema Bwana.” (Isaya 55:8)
“Pendo la Mungu limemiminwa mioyoni mwetu na Roho Mtakatifu tuliyekirimiwa.” (Warumi 5:5)
“Mmoja na mmoja wenu, ajaribu sana kutafuta kibali mbele za Bwana, kwa moyo wote, maana hatuwezi kumpendeza Mungu bila imani.” (Waebrania 11:6)

Kutembea Katika Wito Wako

Mungu anatuita kila mmoja wetu kwa namna ya kipekee. Kila wito unaambatana na vipawa, changamoto, na fursa ambazo ni za kipekee kwa kila mmoja wetu. Kwa hivyo, ni muhimu kumsikiliza Mungu katika maisha yako na kutembea katika wito wako binafsi. Hii inamaanisha kujifunza kusikiliza sauti ya Mungu katika maombi, kusoma Neno lake, na kutafakari juu ya maisha yako. Kutembea katika wito wako ni hatua ya kibinafsi inayohitaji kujitolea na uwazi wa moyo.

“Bali nyote mtakuja kwa njia ya utulivu na kunyamaza; na mtafakari kwa utulivu wa moyo, ndipo mtakapoona nuru ya Bwana.” (Isaya 30:15)
“Jitoe kwa Bwana, na umetulie mbele zake; nawe atakupatia maombi ya moyo wako.” (Zaburi 37:4)
“Naye atatenda katika njia zako, atakuongoza kwa haki na njia zake zote.” (Mithali 3:6)

Umuhimu wa Maombi na Tafakari

Kumtafuta Mungu kunahitaji muda wa maombi na tafakari. Huu ni wakati wa kuwa kimya mbele za Mungu, kumwambia mahitaji yako, na kumsikiliza. Maombi ni mazungumzo na Mungu, na ni katika mazungumzo haya tunapopata mwongozo wa kiroho. Tafakari juu ya Neno la Mungu na jinsi linavyohusiana na maisha yako binafsi ni muhimu katika safari hii ya kiroho. Hili ni jukumu la kibinafsi, ambalo linaweza kufanyika vyema wakati unapotenga muda maalumu kuwa peke yako na Mungu.

“Basi, kesheni, mkiomba kila wakati, ili mweze kuokoka mambo haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.” (Luka 21:36)
“Kwa maana mkimtafuta kwa bidii mtampata, mkimtafuta kwa moyo wenu wote.” (Yeremia 29:13)
“Jilindeni, ninyi wenyewe, na usiache moyo wako upotee, bali mwombe Mungu kwa bidii, naye atakujulisha mapenzi yake.” (Yakobo 1:5)

Kusikiliza Sauti ya Mungu

Mungu anaweza kuzungumza nasi kwa njia nyingi tofauti. Anaweza kuzungumza kupitia Neno lake, kupitia watu wengine, au kupitia matukio katika maisha yetu. Ni muhimu kuwa na moyo wazi na kusikiliza kwa makini sauti ya Mungu. Unapokuwa na utayari wa kusikiliza na kufuata mwongozo wake, utaona njia zako zikifunguka na kupata mwanga mpya wa kiroho. Hii ni safari ya kibinafsi inayohitaji kujitoa na kuwa na moyo wa kusikiliza.

“Kwa maana Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara mbili, lakini mwanadamu hajali.” (Ayubu 33:14)
“Ee Bwana, unayenifundisha na kuniongoza kwa njia ya haki, unayenipenda kwa upendo wa milele.” (Zaburi 32:8)
“Ee Mungu, unayejua kila kitu, unayejua kwamba nakupenda. Unayejua kwamba nakutafuta kwa moyo wote.” (Yohana 21:17)

Kumtafuta Mungu ni Jukumu la Kibinafsi

Kumtafuta Mungu ni jukumu la mtu binafsi na si suala la jumuia au kanisa. Mwisho wa siku, kila mmoja wetu atahitajika kusimama peke yake mbele za Mungu na kutoa hesabu ya maisha yake. Hatutaweza kutumia njia za wengine kama kigezo cha safari yetu ya kiroho. Ni muhimu kuchukua jukumu la kumtafuta Mungu kwa bidii na moyo wote, kwa kuwa hatimaye, ni uhusiano wetu binafsi na Mungu ndio utakaotupa uzima wa milele.

“Kwa maana kila mmoja wetu atatoa habari zake mwenyewe mbele za Mungu.” (Warumi 14:12)
“Usiwe na hofu, maana mimi nipo nawe; usishike, maana mimi ndimi Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia; naam, nitakushika kwa mkono wangu wa kuume wa haki.” (Isaya 41:10)
“Lakini wewe, unaposali, ingia katika chumba chako, funga mlango na umwombe Baba yako aliye sirini. Na Baba yako aonaye sirini atakupa.” (Mathayo 6:6)

Katika safari ya kumtafuta Mungu, kumbuka kwamba ni jukumu lako binafsi na nafsi yako. Usijaribu kufuata njia ya mwingine, bali tembea katika njia yako binafsi ambayo Mungu ameiweka mbele yako. Kwa kufanya hivyo, utaweza kumfikia Mungu kwa undani na kujenga uhusiano wa kipekee na wa kweli naye. Kumtafuta Mungu si jambo la jumuia au kanisa; ni mwito wa ndani unaohitaji kujitoa na kuwa tayari kusimama peke yako mbele za Mungu.

Shopping Cart