Hapo Mwanzo Mungu aliumba Malaika katika hali ya njema na Heri kubwa. Kisha aliumba mbingu na nchi, na viumbe vyote vinavyoonekana na visivyoonekena. (Kol, 1;16, Mwa, 1;31)
Malaika ni viumbe vilivyo Roho tuu vyenye akili na utashi. (Zab 91:11, Ebr 1:7, Uf, 12:7-9).
Malaika wengine walikosa kwa kumkaidi Mungu, wakatupwa motoni na ndio Mashetani ambao Mkubwa wao ni Lusiferi. (Yn, 8:44: Uf 12:7-9,).
Mungu aliumba Malaika ili Wamtukuze, Wafurahi nae Mbinguni na wawe Matarishi/wajumbe wake kwa Wanadamu. (Tob 12:12, Lk. 16:22).
Malaika wema kazi yao ni kutuombea, kutumwa na Mungu kwetu, na wanatulinda kama Malaika walinzi. (Ebr, 13:2). Ambapo kila Mwanadamu ana Malaika wake wa kumlinda na kumuongoza Roho na Mwili, ndie Malaika wake mlinzi, (Zab, 91:11, Mt. 18:10).
Malaika wote sio sawa, wapo Malaika Wakuu, Malaika wanaomtumikia Mungu Mbinguni kwa mfano Makerubi na Maserafi, na pia wapo Malaika walinzi.
Malaika wakuu ni Mikaeli, Gabrieli na Raphaeli (Dn, 10:13, Tobiti 12:15, Lk 1:26).
Mashetani kazi yao ni kuteswa Motoni na hutaka kudhuru Roho na Miili ya wanadamuna kutupoteza milele. (1 Petro, 5:8, Yoh, 8:44).
Neema ya Mungu inatosha kwako
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Tumaini ni nanga ya roho
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Nakuombea 🙏
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Dumu katika Bwana.
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Baraka kwako na familia yako.
Sifa kwa Bwana!
Endelea kuwa na imani!
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Neema na amani iwe nawe.
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mwamini katika mpango wake.
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Nguvu hutoka kwa Bwana
Katika imani, yote yanawezekana
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Mungu ni mwema, wakati wote!
Imani inaweza kusogeza milima
Mungu akubariki!
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Rehema zake hudumu milele
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Rehema hushinda hukumu
Mwamini Bwana; anajua njia