SOMO 1: Isa. 43:16-21
Bwana asema hivi, yeye afanyaye njia katika bahari, na mahali pa kupita katika maji yenye nguvu; atoaye gari na farasi, jeshi la askari na uwezo; wamelala, hawataondoka; wametoweka, wamezimwa mfano wa utambi. Msiyakumbuke mambo ya kwanza, wala msiyatafakari mambo ya zamani. Tazama, nitatenda neno jipya; sasa litachipuka; je! Hamtalijua sasa? Nitafanya njia hata jangwani, na mito ya maji nyikani. Wanyama wa kondeni wataniheshimu, mbweha pia na mbuni; kwa sababu nimewapa maji jangwani, na mito nyikani, ili kuwanywesha watu wangu, wateule wangu; watu wale niliojiumbia nafsi yangu, ili wazitangaze sifa zangu.
WIMBO WA KATIKATI: Zab. 126, (K) 3
(K) Bwana alitutendea mambo makuu, tulikuwa tukifurahi.
Bwana alipowarejeza mateka wa Sayuni,
Tulikuwa kama waotao ndoto.
Ndipo kinywa chetu kilipojaa kicheko.
Na ulimi wetu kelele za furaha. (K)
Ndipo waliposema katika mataifa,
Bwana amewatendea mambo makuu.
Bwana alitutendea mambo makuu,
Tulikuwa tukifurahi. (K)
Ee Bwana, uwarejeze watu wetu waliofungwa,
Kama vijito vya Kusini.
Wapandao kwa machozi,
Watavuna kwa kelele za furaha. (K)
Ingawa mtu anakwenda zake akilia,
Azichukuapo mbegu za kupanda.
Hakika atarudi kwa kelele za furaha,
Aichukuapo miganda yake. (K)
SOMO 2: Flp. 3:8-14
Nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nipate Kristo; tena nionekane katika yeye, nisiwe na haki yangu mwenyewe ipatikanayo kwa sheria, bali ile ipatikanayo kwa Imani iliyo katika Kristo, haki ile itokayo kwa Mungu, kwa Imani; ili nimjue yeye, na uweza wa kufufuka kwake, na ushirika wa mateso yake, nikifananishwa na kufa kwake; ili nipate kwa njia yoyote kuifikia kiyama ya wafu. Si kwamba nimekwisha kufika, au nimekwisha kuwa mkamilifu; la! Bali nakaza mwendo ili nipate kulishika lile ambalo kwa ajili yake nimeshikwa na Kristo Yesu. Ndugu, sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kushika; ila natenda neno moja tu; nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele; nakaza mwendo, niifikilie mede ya thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu.
SHANGILIO: Yoe. 2:12, 13
Lakini hata sasa, asema Bwana, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, kwa maana ni mwenye neema na huruma.
INJILI: Yn. 8:1-11
Yesu akaenda mpaka mlima wa Mizeituni. Hata asubuhi kulipokucha akaingia tena hekaluni, na watu wote wakamwendea; naye akaketi, akawa akiwafundisha.
Waandishi na Mafarisayo wakamletea mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, wakamweka katikati. Wakamwambia, Mwalimu, mwanamke huyu amefumaniwa alipokuwa akizini. Basi katika torati, Musa alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake namna hii; nawe wasemaje? Nao wakasema neno hili wakimjaribu, ili wapate sababu ya kumshitaki.
Lakini Yesu akainama, akaandika kwa kidole chake katika nchi. Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe. Akainama tena, akaandika kwa kidole chake katika nchi. Nao waliposikia, wakashitakiwa na dhamiri zao, wakatoka mmoja mmoja, wakianzia tangu wazee hata wa mwisho wao; akabaki Yesu peke yake, na yule mwanamke amesimama katikati.
Yesu akajiinua asimwone mtu ila yule mwanamke, akamwambia, Mwanamke, wako wapi wale washitaki wako? Hakuna aliyekuhukumu kuwa na hatia? Akamwambia, Hakuna, Bwana. Yesu akamwambia, Wala mimi sikuhukumu. Enenda zako; wala usitende dhambi tena.
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Tumaini ni nanga ya roho
Sifa kwa Bwana!
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Dumu katika Bwana.
Katika imani, yote yanawezekana
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Rehema hushinda hukumu
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Imani inaweza kusogeza milima
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Neema ya Mungu inatosha kwako
Mwamini katika mpango wake.
Nakuombea 🙏
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Mungu akubariki!
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Nguvu hutoka kwa Bwana
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Mwamini Bwana; anajua njia
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Mungu ni mwema, wakati wote!
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Neema na amani iwe nawe.
Endelea kuwa na imani!
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Rehema zake hudumu milele
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Baraka kwako na familia yako.
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini