
Anza kusali Rozari kwa kuibusu miguu ya Bwana Yesu katika taswira (picha) yake Msalabani kisha fanya Ishara ya Msalaba ukiwa unasema “Kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Amina”.
Taja kwa ufupi nia za Rozari hii. Tangaza nia hizo kwa sauti kama mnasali wengi kwa pamoja, Mfano, “Tusali kuombea amani katika nchi yetu na ulimwenguni kote, na tuunganishe nia hizo na nia zetu sisi wenyewe, nk).
Baada ya Sala ya Nasadiki pamoja na ya Baba Yetu, tunamwomba Mungu (Utatu Mtakatifu) fadhila za Imani, Matumaini na Mapendo, zikiambatana na Salamu Maria tatu.
Mojawapo ya maneno yafuatayo huweza kutumika:
“Mungu Baba utuongezee Imani. Salamu Maria, …… Mungu Mwana utuongezee matumaini, Salamu Maria, …… Mungu Roho Mtakatifu washa nyoyo zetu kwa mapendo yako, Salamu Maria, …..”
Au;
“Utuongezee Imani ee Bwana, Salamu Maria,…. Utuongezee matumaini ee Bwana, Salamu Maria,…. Uwashe nyoyo zetu kwa mapendo yako ee Bwana, Salamu Maria, …..” Au;
“Salamu e uliyechaguliwa na Mungu Baba, Salamu Maria,….. Salamu e Mama wa Mungu Mwana, Salamu Maria,….. Salamu e Mchumba wa Mungu Roho Mtakatifu, Salamu Maria,……”
Atukuzwe Baba, na Mwana na Roho Mtakatifu, kama mwanzo na sasa na siku zote, na milele, Amina.
Ee Yesu wangu, utusamehe dhambi zetu, utuepushe na moto wa milele, ongoza roho zote mbinguni, hasa za wale wanaohitaji huruma yako zaidi.
Tuwasifu milele, Yesu, Maria na Yosef.
Kisha endelea na sala zinazofuata kama mpangilio unavyoonyesha hapo juu.
Kila baada ya Tendo moja na makumi ya Salamu Maria…, “Atukuzwe..”, “Ee Yesu wangu…” na “Tuwasifu milele…” kama muda unatosha wimbo ufaao wa Bikira Maria uimbwe (kama muda ni mfupi basi angalau ubeti mmoja mmoja uimbwe kila baada ya makumi hayo). Baada ya Wimbo, Tendo linalofuata litangazwe kwa sauti pamoja na tafakari fupi au ombi linaloambatana na Tendo husika kama inavyoonyeshwa hapa chini.
MATENDO YA ROZARI TAKATIFU
MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)
Tendo la kwanza; Malaika Gabrieli anampasha habari Maria kuwa atakuwa Mama wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie unyenyekevu.
Tendo la pili; Maria Mtakatifu anakwenda kumtembelea Elizabeti. Tumwombe Mungu atujalie mapendo ya jirani.
Tendo la tatu; Yesu anazaliwa Betlehemu. Tumwombe Mungu atujalie moyo wa ufukara
Tendo la nne; Yesu anatolewa hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie usafi wa moyo.
Tendo la tano; Maria anamkuta Yesu hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie kuwatii wakubwa wetu.
MATENDO YA UCHUNGU (Jumanne na Ijumaa)
Tendo la kwanza; Yesu anatoka jasho la damu kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie sikitiko la dhambi.
Tendo la pili; Yesu anapigwa kwa mijeledi kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuacha dhambi za uchafu.
Tendo la tatu; Yesu anatiwa miiba kichwani kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kushinda kiburi.
Tendo la nne; Yesu anachukua Msalaba kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuvumilia taabu.
Tendo la tano; Yesu anakufa Msalabani. Tumwombe Mungu atujalie kuwapenda Yesu na Maria.
MATENDO YA UTUKUFU (Jumatano na Jumapili)
Tendo la kwanza; Yesu anafufuka. Tumwombe Mungu atujalie kugeuka watakatifu.
Tendo la pili; Yesu anapaa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kwenda mbinguni.
Tendo la tatu; Roho Mtakatifu anawashukia Mitume. Tumwombe Mungu atujalie bidii katika dini yetu.
Tendo la nne; Bikira Maria anapalizwa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kufa vizuri.
Tendo la tano; Bikira Maria anawekwa Malkia mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kudumu katika njia njema.
MATENDO YA MWANGA (Alhamisi)
Tendo la kwanza; Yesu anabatizwa Mto Jordani. Tumwombe Mungu atujalie uaminifu kwa ahadi zetu za ubatizo.
Tendo la pili; Yesu anageuza maji kuwa divai huko Kana. Tumwombe Mungu atujalie kuukoleza ulimwengu kwa chachu ya enjili.
Tendo la tatu; Yesu anatangaza Ufalme wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie kupokea Ufalme wake kwa toba ya kweli.
Tendo la nne; Yesu anageuka sura. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kuung’arisha ulimwengu kwa uso wa Yesu.
Tendo la tano; Yesu anaweka Sakramenti ya Ekaristia. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kujitoa sadaka kwa ajili ya wengine.
LITANIA YA BIKIRA MARIA
- Bwana utuhurumie
- Bwana utuhurumie
- Kristo utuhurumie
- Bwana utuhurumie
- Bwana utuhurumie
- Kristo utusikie
- Kristo utusikilize
- Mungu Baba wa Mbinguni,…… Utuhurumie
- Mungu Mwana Mkombozi wa dunia ……… Utuhurumie
- Mungu Roho Mtakatifu …….. Utuhurumie
- Utatu Mtakatifu Mungu Mmoja …….. Utuhurumie
- Maria Mtakatifu ………. utuombee
- Mzazi Mtakatifu wa Mungu …….. utuombee
- Bikira Mtakatifu Mkuu wa Mabikira …….. utuombee
- Mama wa Kristo ……… utuombee
- Mama wa Neema ya Mungu ………….. utuombee
- Mama Mtakatifu sana ……… utuombee
- Mama mwenye usafi wa Moyo ……….. utuombee
- Mama mwenye ubikira ……….. utuombee
- Mama usiye na doa ……….. utuombee
- Mama mpendelevu ………. utuombee
- Mama mstajabivu ………. utuombee
- Mama wa Muumba ………. utuombee
- Mama wa Mkombozi ………….. utuombee
- Mama wa Kanisa……….. utuombee
- Bikira mwenye utaratibu ………….. utuombee
- Bikira mwenye heshima ………….. utuombee
- Bikira mwenye sifa ………….. utuombee
- Bikira mwenye uwezo ………….. utuombee
- Bikra mweye huruma ………….. utuombee
- Bikra mwaminifu………….. utuombee
- Kioo cha haki ………….. utuombee
- Kikao cha hekima ………….. utuombee
- Sababu ya furaha yetu ………….. utuombee
- Chombo cha neema ………….. utuombee
- Chombo cha kuheshimiwa ………….. utuombee
- Chombo bora cha ibada ………….. utuombee
- Waridi lenye fumbo ………….. utuombee
- Mnara wa Daudi ………….. utuombee
- Mnara wa pembe ………….. utuombee
- Nyumba ya dhahabu ………….. utuombee
- Sanduku la Agano ………….. utuombee
- Mlango wa Mbingu ………….. utuombee
- Nyota ya asubuhi ………….. utuombee
- Afya ya wagonjwa ………….. utuombee
- Kimbilio la wakosefu ………….. utuombee
- Mtuliza wenye huzuni ………….. utuombee
- Msaada wa waKristo ………….. utuombee
- Malkia wa Malaika ………….. utuombee
- Malkia wa Mababu ………….. utuombee
- Malkia wa Manabii ………….. utuombee
- Malkia wa Mitume ………….. utuombee
- Malkia wa Mashahidi ………….. utuombee
- Malkia wa Waungama dini ………….. utuombee
- Malkia wa Mabikira ………….. utuombee
- Malkia wa Watakatifu wote ………….. utuombee
- Malkia uliyepalizwa Mbinguni ………….. utuombee
- Malkia wa Rozari takatifu ………….. utuombee
- Malkia wa amani ………….. utuombee
- Mwanakodoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,…………..Utusamehe ee Bwana.
- Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,…………..Utusikilize ee Bwana
- Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,…………..Utuhurumie.
- Utuombee, Mzazi Mtakatifu wa Mungu,…………..Tujaliwe ahadi za Kristo.
Tuombe
Ee Bwana Mungu, utujalie sisi watumishi wako afya ya roho na mwili siku zote; na kwa maombezi matukufu ya Maria Mtakaatifu Bikira daima, tuopolewe na mashaka ya saa, tupate na furaha za milele. Kwa Kristo Bwana wetu, Amina.
Karibu Vitatabu vya Kikatoliki
[products orderby="rand" columns="4" category="vitabu-vya-dini" limit="20"]
Stephen Mushi (Guest) on July 25, 2018
🙏💖 Asante kwa neema zako Mungu
Esther Cheruiyot (Guest) on May 27, 2018
Amina
Lucy Mahiga (Guest) on April 9, 2018
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Maimuna (Guest) on February 12, 2018
🙏🙏🙏
Frank Sokoine (Guest) on December 22, 2017
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
David Nyerere (Guest) on July 19, 2017
🙏❤️✨ Asante Mungu kwa kila kitu
Irene Makena (Guest) on June 5, 2017
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Catherine Mkumbo (Guest) on April 29, 2017
🙏✨ Mungu asikie maombi yetu
Lydia Mutheu (Guest) on March 4, 2017
🙏✨❤️ Neema za Mungu zikufunike
Daniel Obura (Guest) on October 3, 2016
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Jane Muthoni (Guest) on October 1, 2016
🙏🌟 Neema za Mungu zisikose
Raphael Okoth (Guest) on September 22, 2016
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Lydia Wanyama (Guest) on September 20, 2016
Tembea kwa imani, si kwa kuona
James Kimani (Guest) on July 11, 2016
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Esther Nyambura (Guest) on April 18, 2016
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Violet Mumo (Guest) on February 27, 2016
Neema ya Mungu inatosha kwako
James Malima (Guest) on January 27, 2016
🙏✨ Mungu atupe nguvu
Alice Wanjiru (Guest) on December 29, 2015
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Anna Malela (Guest) on December 22, 2015
🙏✨❤️ Tumwombe Mungu kila siku
Fredrick Mutiso (Guest) on November 1, 2015
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Thomas Mwakalindile (Guest) on October 21, 2015
🙏💖 Mungu wetu asifiwe
Joy Wacera (Guest) on September 30, 2015
🙏❤️💖 Baraka za Mungu ziwe nawe
Paul Ndomba (Guest) on April 11, 2015
🙏🌟 Namuomba Mungu akupiganie