Ee Mt. Yosefu, ambaye ulinzi wako ni mkubwa, wenye nguvu na wa haraka mbele ya Kiti cha Enzi cha Mungu, ninakukabidhi nia na haja zangu zote. Ee Mt. Yosefu, unisaidie kwa maombezi yako yenye nguvu, na unipatie kutoka kwa Mwanao Mungu, baraka zote za kiroho, kwa njia ya Kristu Bwana wetu, ili nikishapata msaada wako wa mbinguni ningali bado hapa duniani, niweze nami kumsifu, kumwabudu na kumshukuru Mungu aliye Baba mwema kabisa kushinda wote. Ee Mt. Yosefu, sichoki kamwe kufikiri moyoni kwa upendo, jinsi Mtoto Yesu alivyokuwa amesinzia mikononi mwako. Akiwa amepumzika hivyo karibu na moyo wako, sithubutu kujongea, nisije nikamsumbua, bali nakuomba wewe umkumbatie na kumbusu kwa niaba yangu na kumwambia anipe busu lake nitakapovuta pumzi yangu ya mwisho.
Mtakatifu Yosefu Msimamizi wa wanaozimia roho; Utuombee.
Amina.
Sala hii ilipatikana katika mwaka wa hamsini wa Bwana na Mwokozi Wetu Yesu Kristu. Mnamo mwaka 1505 Baba Mtakatifu alimtumia sala hii Mfalme Charles wakati alipokuwa anaenda vitani. Yeyote atakayeisoma sala hii, au kuisikia ikisomwa, au kuibeba, hatakufa kifo cha ghafla,hatazama majini, hatadhurika kwa sumu, wala hataanguka katika mikono ya adui zake, au kuunguzwa katika moto wowote ule, au kushindwa katika vita.
Sali sala hii kwa siku tisa mfululizo, kwa kuomba jambo lolote unalolihitaji. Haijawahi kusikika kuwa sala hii imeshindwa jambo.
Sarah Karani (Guest) on December 27, 2017
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Samuel Were (Guest) on December 27, 2017
πβ¨ Mungu atakuinua
Peter Tibaijuka (Guest) on December 19, 2017
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Benjamin Masanja (Guest) on October 11, 2017
Mwamini Bwana; anajua njia
Joseph Njoroge (Guest) on August 10, 2017
Sifa kwa Bwana!
Stephen Kikwete (Guest) on June 15, 2017
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Nora Lowassa (Guest) on May 7, 2017
πππ
Chris Okello (Guest) on May 2, 2017
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Ruth Wanjiku (Guest) on December 10, 2016
πβ€οΈπ Baraka za Mungu ziwe nawe
Alex Nyamweya (Guest) on November 14, 2016
πβ€οΈβ¨ Mungu akujalie furaha
Peter Mbise (Guest) on October 15, 2016
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
James Kimani (Guest) on September 26, 2016
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Monica Nyalandu (Guest) on August 20, 2016
Endelea kuwa na imani!
Joseph Kawawa (Guest) on June 29, 2016
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Andrew Odhiambo (Guest) on May 20, 2016
Imani inaweza kusogeza milima
Chris Okello (Guest) on May 20, 2016
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Violet Mumo (Guest) on May 6, 2016
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Victor Kimario (Guest) on November 22, 2015
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Lydia Mzindakaya (Guest) on October 28, 2015
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Joseph Kawawa (Guest) on October 13, 2015
Neema ya Mungu inatosha kwako
Nancy Komba (Guest) on August 18, 2015
ππ Mungu akujalie amani
Rose Lowassa (Guest) on August 14, 2015
πβ€οΈ Mungu ni mwaminifu
Charles Mchome (Guest) on July 11, 2015
Nakuombea π
John Lissu (Guest) on June 18, 2015
ππ Neema za Mungu zisikose
Ruth Wanjiku (Guest) on June 13, 2015
ππ Asante kwa neema zako Mungu