Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMS💌💕
AckyShine

SALA YA NOVENA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Featured Image

Ee Moyo Mtakatifu sana wa Yesu, chemchemi ya kila baraka, ninakuabudu, ninakupenda, na kwa majuto halisi ya dhambi zangu, nakutolea moyo wangu dhaifu. Nifanye mnyenyekevu, mvumilivu na safi, nikikubali na kuyatii kabisa mapenzi yako. Ee Yesu mwema, unijalie niishi nawe na kwa ajili yako. Unilinde niwapo katikati ya hatari, unifariji katika mateso, unipe afya ya mwili na msaada katika mahitaji ya mwili, Baraka yako juu ya kila nilifanyalo, na neema ya kifo chema. Amina.

Ee Yesu uliyesema “Kweli nawaambieni, ombeni nanyi mtapewa, tafuteni nanyi mtapata, gongeni nanyi mtafunguliwa”, tazama ninagonga, ninatafuta na kuomba …….. (Taja ombi lako)
Baba Yetu….., Salamu Maria …….., Atukuzwe Baba……..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!

Ee Yesu uliyesema “Kweli nawaambieni, chochote mtakachomwomba Baba kwa jina langu mtapewa”, tazama kwa jina lako ninaomba ……. (Taja ombi lako)
Baba Yetu….., Salamu Maria …….., Atukuzwe Baba……..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!

Ee Yesu uliyesema “Kweli nawaambieni, mbingu na dunia zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe”, tazama, nikitiwa nguvu na maneno yako ya kweli ninaomba …….. (Taja ombi lako)
Baba Yetu….., Salamu Maria …….., Atukuzwe Baba……..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!

Ee Moyo Mtakatifu wa Yesu, ambaye kwako ni kitu kimoja tu kisichowezekana, ambacho ni kutoacha kutowaonea huruma wenye huzuni, utuhurumie sisi wakosefu maskini na utujalie neema tukuombayo kwa njia ya Moyo Imakulata wa Maria, Mama yetu mpole.

Sali ‘Salamu Malkia’ na kuongezea, ‘Mtakatifu Yosefu Baba Mlishi wa Yesu, utuombee’.

P.S. – Sala hii ya Novena ilisaliwa kila siku na PADRE PIO kwa ajili ya kuwaombea wale wote waliomwomba msaada wa sala zake. Unaweza kuisali kwa namna tofauti tofauti. Mfano, kama Novena ya siku tisa, ambapo unasali sala hii mara moja au zaidi kila siku kwa siku tisa, au unaweza kuifanya kama Novena ya masaa, ambapo unasali sala hii kila baada ya saa moja kwa masaa tisa kwa siku hiyo hiyo, hasa kama kitu unachokiomba ni cha haraka au umesongwa moyoni. Vilevile unaweza kuifanya sala hii kama sehemu ya sala zako za kila siku katika mwezi Juni ambao ni mwezi uliotengwa na Kanisa kwa ajili ya kuuheshimu Moyo Mtakatifu wa Yesu, na hapo utaitumia kuwaombea watu waliokuomba msaada wa sala zako kama alivyofanya Mtakatifu Padre Pio. Pia unaweza kuitumia kama sala yako ya siku zote au ya mara kwa mara kwa ajili ya mahitaji mbalimbali.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Lucy Kimotho (Guest) on September 20, 2017

🙏💖🙏 Mungu akufunike na upendo

Tabitha Okumu (Guest) on August 24, 2017

🙏💖💫 Mungu ni mwema

Isaac Kiptoo (Guest) on August 13, 2017

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Miriam Mchome (Guest) on July 16, 2017

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Rose Kiwanga (Guest) on June 30, 2017

🙏❤️ Mungu ni mwaminifu

James Mduma (Guest) on June 3, 2017

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Rose Kiwanga (Guest) on May 29, 2017

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Christopher Oloo (Guest) on April 30, 2017

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Anna Malela (Guest) on December 5, 2016

🙏✨ Mungu asikie maombi yetu

Lydia Mahiga (Guest) on November 14, 2016

🙏✨❤️ Tumwombe Mungu kila siku

Frank Macha (Guest) on September 8, 2016

🙏💖 Nakushukuru Mungu

Sarah Karani (Guest) on August 11, 2016

Rehema hushinda hukumu

Charles Mchome (Guest) on August 11, 2016

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Joyce Aoko (Guest) on July 11, 2016

🙏🌟 Namuomba Mungu akupiganie

Diana Mallya (Guest) on April 11, 2016

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Joseph Mallya (Guest) on December 4, 2015

🙏🙏🙏

Hellen Nduta (Guest) on November 5, 2015

Nakuombea 🙏

Peter Mbise (Guest) on October 23, 2015

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Peter Mbise (Guest) on September 23, 2015

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Esther Cheruiyot (Guest) on August 25, 2015

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Francis Mrope (Guest) on May 23, 2015

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Nancy Kawawa (Guest) on May 7, 2015

Dumu katika Bwana.

Esther Nyambura (Guest) on April 3, 2015

🙏🌟 Mbarikiwe sana

Related Posts

SALAMU MARIA

SALAMU MARIA

Salamu Maria
Umejaa neema
Bwana yu nawe
Umebarikiwa kuliko wanawake wote
Na Y... Read More

Sala fupi ya Asubuhi

Sala fupi ya Asubuhi

Tuusifu Utatu Mtakatifu wa Mungu Mwenyezi, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, milele na milele, Amina... Read More

Sala za kuheshimu Damu Takatifu ya Yesu

Sala za kuheshimu Damu Takatifu ya Yesu

Tusali kila siku sala hizi, angalau kwa mwezi wa saba (Julai) kila mwaka, mwezi wa kuhesh... Read More

AMRI ZA MUNGU

AMRI ZA MUNGU

1. NDIMI BWANA MUNGU WAKO, USIABUDU MIUNGU WENGINE.
2. USILITAJE BURE JINA LA MUNGU WAKO.Read More

SALA YA KUOMBEA FAMILIA

SALA YA KUOMBEA FAMILIA

Ewe Mungu Mwenyezi, sisi kama familia tunakushukuru kwa zawadi ya Mama Kanisa Katoliki ambaye sik... Read More

Sala ya Usiku kabla ya kulala

Sala ya Usiku kabla ya kulala

Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.

SALA YA KUSHUKURU

Tunakus... Read More

SALA ZA IBADA KWA BIKIRA MARIA WA MATESO

SALA ZA IBADA KWA BIKIRA MARIA WA MATESO

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

Tumia Rozari ya Mateso Saba ya Bikira Maria iliyo ... Read More

SALA MBELE YA KITI CHA ENZI CHA MUNGU

SALA MBELE YA KITI CHA ENZI CHA MUNGU

Sali Atukuzwe 7 kwa heshima ya Malaika 7 wateule ujipatie neema ya kuepa dhambi mbaya saba na kut... Read More

SALA YA KUMWOMBA MT. YOSEFU MSAADA (SALA KUU KWA MTAKATIFU YOSEFU)

SALA YA KUMWOMBA MT. YOSEFU MSAADA (SALA KUU KWA MTAKATIFU YOSEFU)

Ee Mt. Yosefu mwenye heri, tunakimbilia kwako katika masumbuko yetu, na kisha omba shime ya Mchum... Read More

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

Tumia Rozari ya Mateso Saba ya Bikira Maria iliyo na mafungu 7 yaani mateso 7 yenye Salamu Maria... Read More

Sala ya Saa Tisa

Sala ya Saa Tisa

✝⌚✝

Sala ya saa tisa🙏🏾

Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu.... Read More

SALA ZA KUMWABUDU YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA ZA KUMWABUDU YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA YA KUMWABUDU BWANA YESU KATIKA SAKRAMENTI TAKATIFU

Ee Yesu Kristu,/ Bwana wangu na M... Read More