Siku moja jioni katika mji flani, kulikuwa na basi likisafiri kutoka mji huo kuelekea mji mwingine. Lilikuwa ni basi kubwa na limejaa abiria. Wakati wakiendelea na safari, ghafla, mvua kubwa iliyoambatana na radi ikaanza kunyesha. Dereva hakuogopa, wala abiria, wakaendelea na safari. Mara wakati wanaenda, radi ikaanza kufuatilia gari. Kila wakienda, radi inapiga karibu na basi kana kwamba inalifuata basi. Likisimama, radi inapiga pembezoni mwa basi.
Dereva kuona hivyo, akasimamisha gari mita 5 kutoka kwenye mti… Akawaambia abiria, “Humu ndani ya basi, kuna mtu ambaye leo ni siku yake ya kufa, tena kufa kwa radi. Ili tusife wote, nataka kila abiria ashuke akaguse mti ili anayepigwa na radi, apigwe wengine wasife kwa ajili yake. “Abiria wakitetemeka, wakaanza kushuka mmoja mmoja. Unaenda unagusa mti , kisha unarudi kwenye basi. Abiria wote pamoja na dereva mmoja mmoja, wakaenda, wakagusa mti na kurudi bila dhara lolote! Akawa kabaki abiria mmoja tu, ambaye alikuwa hajagusa mti. Abiria wote kwa macho ya hasira wakamwambia akaguse mti. Akawa anaogopa kufa. Akagoma. Wakamlazimisha kwa nguvu sana na kumtoa nje……. …….. Yule abiria akiwa amefumba macho, akaenda akagusa mti. Hamadi bin Vuu! Radi kali sana ikalipiga basi, abiria na wote waliokuwamo, wakafa palepale. Kumbe uwepo wake ndio ulikuwa unazuia abiria wengine wasidhurike na radi.
MAFUNZO
1. Unapofanikiwa, huwezi jua uwepo wa nani umefanikisha mafanikio yako, usichukue sifa zote peke yako. Wapatie na wengine bila kumsahau MUNGU.
2. Unaweza kujiona huna thamani sehemu ulipo, iwe kwenye kundi la WhatsApp, darasani, kazini, kwenye basi, barabarani bila kujua kama uwepo wako ni wa muhimu sana kwa ustawi wa wengine.
3. Usimtenge wala kumnyanyasa mtu au jirani yako, huwezi jua uwepo wake ni kwa ajili gani.
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Dumu katika Bwana.
Endelea kuwa na imani!
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Neema ya Mungu inatosha kwako
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Mungu akubariki!
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Rehema zake hudumu milele
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Tumaini ni nanga ya roho
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Imani inaweza kusogeza milima
Neema na amani iwe nawe.
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Nguvu hutoka kwa Bwana
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Mwamini Bwana; anajua njia
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Mungu ni mwema, wakati wote!
Baraka kwako na familia yako.
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Rehema hushinda hukumu
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Katika imani, yote yanawezekana
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Nakuombea 🙏
Sifa kwa Bwana!
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Mwamini katika mpango wake.
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu