Kumuamini Mungu ni kuwa na uhakika na uwepo na uwezo wa Mungu. Ni kutambua na kukubali kwa uhakika kuwa Mungu yupo na anaweza kutenda. Unaweza kuwa na Imani lakini ukakosa kuamini yaani unaamini kwa Mungu lakini huamini kama atakutendea.
Kuamini kunakua na sifa zifuatazo
1. Kutokuwa na mashaka kama Mungu atatenda au hatatenda
2. Kuwa na subira. Kusubiri Mungu atende wakati unaofaa
3. Kuwa na matumaini hata kama hujatendewa.
Mara nyingi watu wanakuwa na imani lakini hawaamini ndio maana wanashindwa kuelewa mapenzi ya Mungu, mipango na matendo yake.
Kuwa na Imani tuu bila Kuamini huwezi kuendelea mbele kiroho. Kukosa Kuamini ndiyo sababu inayokwamisha maendeleo ya kiroho kwa watu wenye imani.
Dalili za kukosa au kupungukiwa Kuamini ni kama ifuatavyo
1. Kutokuwa na uhakika kama sala zako zitajibiwa.
2. Kukosa subira na matumaini.
3. Kuwa na maswali kama, Hivi Mungu yupo na mimi au hayupo na mimi??. Kujiuliza Hivi Mungu amenisikia?, Ananikumbuka?, Atafanya kweli??
Kukosa Kuamini kukizidi kunaleta hali ya kuhisi kuwa Mungu yupo na anaweza kutenda chochote lakini hatendi. Utakua sasa unaanza Kujiuliza kwa nini. Mtu akifika katika hali hii, Imani huporomoka na kupotea Mara nyingine mtu hufikia Kukosa imani kabisa na Mungu japokuwa anajua yupo na anaweza.
Ili kuondokana na hali hii ya kuwa na Imani lakini unakua na Kukosa kuamini, jitahidi kusali /kuomba neema ya kuamini, Jitahidi kusoma Biblia itakujengea kuamini na pia omba ushauri kwa watu wenye imani na wanaoamini.
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Baraka kwako na familia yako.
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Rehema hushinda hukumu
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Mwamini katika mpango wake.
Mungu ni mwema, wakati wote!
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Nakuombea 🙏
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Nguvu hutoka kwa Bwana
Sifa kwa Bwana!
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Dumu katika Bwana.
Endelea kuwa na imani!
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Mwamini Bwana; anajua njia
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Neema na amani iwe nawe.
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Tumaini ni nanga ya roho
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Mungu akubariki!
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Rehema zake hudumu milele
Katika imani, yote yanawezekana
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Neema ya Mungu inatosha kwako
Imani inaweza kusogeza milima
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Wakati wa Mungu ni kamilifu