Nabii mmoja aliumwa
na Jino, lilimtesa sana…
Akapiga magoti kumlilia
Mungu ili amponye..
Mungu akamuonesha mti
flani ili majani yake
Yapate kumtibu..
Akaenda kwenye mti ule,
Akachukua majani yake
akatumia na kweli
akapona…
Baada ya Muda Mrefu
Kupita, nabii yule aliumwa
na Jino tena…
Safari Hii alienda
moja kwa moja kwenye mti
Na kuchuma majani yake
na kuyatumia,Lakini
hakupona..
Akaja tena Kwa Mungu
na kumwambia…
“Mbona ule mti niliutumia
Haukuniponyesha kama
Wakati ule? “
Mungu akamjibu…
“Mara ya Mwanzo ulipona
Kwa kuwa
ulinitegemea mimi, mara ya
Pili hakupona kwa kuwa
Uliutegemea Mti”..
KILA WAKATI TUNAPASWA
KUMUOMBA NA
KUMTEGEMEA MUNGU,
HATA KAMA KWA JAMBO
AMBALO ALISHATUJIBU..
KWA KUTOKUFANYA HIVYO
NDIYO MAANA MARA
KADHAA
TUNAKOSA MAFANIKIO…
✔Tulipooomba mchumba
Tulipompata
Hatukuombea Ulinzi wa
ndoa zetu, matokeo yake
Ni vilio kwenye ndoa
Karibu zote..
✔ Tuliomba watoto,
Tulipowapata
muda mwingi tukatumia
Akili zetu kuwalea
Na kusahau kumshirikisha
Mungu katika malezi yao,
mwisho wa yote
Tunaishia kusema
Watoto wa siku hizi…
✔ Tuliomba kazi kwa Mungu ,
Tulipopata tukaanza
Kutumia akili zetu katika
Kazi hizo na kuanza
Kudharau wenzetu na
Kuzisaliti ndoa
na familia zetu..
▪ Familia zinalia…
▪ Watoto wanalia
Baraka zitatoka wapi?
▪ Kabla ya Kupata kazi
Tulikuwa Hatukosi
Kanisani,
Hakukosi kwenye
Maombi…
TUMEPATA KAZI
TUMEKUWA BIZE
HAKUNA MAOMBI
WALA KANISANI..
Baraka zitokee wapi?
Mafanikio yatoke wapi?
Mshahara mkubwa
Lakini madeni kila siku,
Tena tunakopeshwa na
Tuliowazidi mshahara…
Wapendwa tustuke..
Tumrudie Mungu…
Tusisingizie uchawi..
Tumejiroga wenyewe..
Tumuweke Mungu mbele..
Tafakari chukua hatua
Imani inaweza kusogeza milima
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Rehema hushinda hukumu
Baraka kwako na familia yako.
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Neema ya Mungu inatosha kwako
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Katika imani, yote yanawezekana
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Mungu akubariki!
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Tumaini ni nanga ya roho
Sifa kwa Bwana!
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Dumu katika Bwana.
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Neema na amani iwe nawe.
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Mungu ni mwema, wakati wote!
Mwamini katika mpango wake.
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Nguvu hutoka kwa Bwana
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Rehema zake hudumu milele
Nakuombea 🙏
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Mwamini Bwana; anajua njia
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Endelea kuwa na imani!
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha