Kisa cha kusisimua cha mama mjane

Mimi ni mwanamke mjane ninaishi mjini Arusha. Huu ni ushuhuda wangu wa maisha yangu.

Miaka 21 iliyopita nilifunga ndoa na mume wangu mpendwa kanisani, baadaye tukajaliwa kuwa na watoto wa2 mmoja wa kiume Alfred na mwingine wa kike Minza. Mimi nimesomea mambo ya uuguzi MD, nimefanya kazi muda mrefu ktk hospitali za wilayani karatu na Arusha mjini mpk nilipolazimika kuacha kutokana na udhaifu wa mwili na mambo yaliyonipata katika maisha. Mume wangu alikua ni askari polisi mpk baadaye alipojiunga na ajira zingine mpaka alipokutwa na mauti kama nitakavyoeleza baadaye hapo chini.

Tulipooana na mume wangu,maisha yalikua ya furaha sana na tulikua na mipango mingi mizuri ya kujiendeleza kiuchumi na kihuduma kwani tulikua tunampenda Mungu na tulikua waimbaji na waombaji kanisani. Baada ya muda mrefu katika maisha ya ndoa na familia, baadaye maisha yalianza kuwa magumu kutokana na mishahara yetu kuwa midogo ukilinganisha na mahitaji. Mume wangu alijisikia vibaya sana zaidi yangu hasa pale alipoona wengine hasa marafiki zake wanafanikiwa lkn yeye hafanikiwi. Kuna maaskari walikua wakipandishwa vyeo haraka na kuhamishiwa mijini ikiwemo Daressalaam na Arusha- hali hiyo ilimpa shida sana akawa anaomba na kufunga kwa muda mrefu lkn hakuona mafanikio.

Wakati fulani ilitokea akakutana na rafiki yake askari mwenzie, akamualika nyumbani kwake. Mume wangu aliporudi akaja akiwa mwenye mawazo makubwa sana, sikujua ni kwanini na hukuniambia hata nilipomuuliza.

Baada ya siku kadhaa mume wangu akaacha kwenda kanisani wala huduma hakufurahia tena. Akawa ni mkimya na mwenye mawazo mengi sana. Siku moja akaniambia atasafiri kikazi kwa muda wa siku tatu. Baada ya siku tatu akarudi akiwa hoi sana na mgonjwa km mtu mwenye malaria. Nikajaribu kumshawishi twende hospitali hakukubali kbs akaniambia ni uchuvo tu wa safari na kazi na atakuwa salama. Kesho yake, kweli akaamka vzr na kwenda kazini bila kuugua km hapo jana. Ikapita muda mrefu bila kujua hasa nini kinachoendelea kwa mume wangu kwani hakuniambia chochote hata nilipomuuliza.

Baada ya muda, mume wangu akapata nafasi ya kwenda masomoni Moshi. Alipomaliza masomo hayo,haikuchukua muda mrefu tukapata barua ya uhamisho wa mume wangu kikaz kuelekea Arusha mjini.

Binafsi nilifurahi sana, nikajua Mungu ameanza kujibu maombi yetu ya siku nyingi. Kwa hiyo na mimi nikaanza mipango ya uhamisho. Tulipofika Arusha tukapata makazi mapya na kanisa zuri la kuabudia. Baada ya muda niligundua mume wangu hakupenda mambo ya Mungu km siku za zamani. Wakati huu mimi nilikua mjamzito nikijandaa kupata mtoto wa pili.

Tulizungumza sana na mwenzangu lkn sikujua hasa kitu gani kulikua kinamsumbua. Baada ya muda niligundua mume wangu alikua mlevi wa pombe na tabia yake ilibadilika sana hasa kuhusu mambo ya kiimani na kushirikishana mipango. Aligeuka kuwa mtu wa mambo mengi,kuamrisha na msiri sana- kutokana na aina ya kazi zao nikajua ni kawaida.

Nilipojifungua mtoto wetu wa pili akaniletea zawadi ya gari mark2-mimi nilikua miongoni mwa wanawake wachache kuendesha mark2 wakati miaka ya90 mwishoni. Tulijisikia vzr sana na mambo ni kama yalikua yananyooka.

Mwaka 2001 mume wangu alipata nafasi ya kwenda tena chuoni kusoma kwa muda mfupi huko Dar, nikabaki na familia na nikawa naendelea vzr na kazi zangu. Alipomaliza masomo akarudi na maisha yakaendelea kwa muda km kawaida. Baada ya miezi km sita kutoka chuo ni, mume wangu akaniambia anataka kuacha kazi- nilishangaa sana nikamuuliza maswali mengi lkn hukunijibu vzr. Wiki moja baadaye akaniambia ameacha kazi na ameajiriwa shirika moja kubwa la UN hapa Arusha.

Kweli akaanza kuvaa sare mpya za kazi hiyo mpya. Kazi hiyo mpya ilituletea mafanikio makubwa sana ya kifedha na kujieneza kwa mali. Wakati huo pia mimi nilipata nafasi ya kwenda kusoma chuoni muhimbili Dar kwa muda wa miaka mitano. Nikaenda Dar nikaiacha familia ikiendelea vzr kbs.

Nikiwa Dar chuoni nilipata nafasi ya kwenda nje ya nchi kufanya seminar ya health exhibitions (mafunzo ya maonesho)- nikiwa huko nilipigiwa simu kuwa mtoto wetu mdogo amefariki dunia. Nilichanganyikiwa nikarudi nyumbani kwa kuchelewa, nikakuta wameshamzika Alfred mwanangu sikumuona tena. Ilisemekana alifariki ghafla sana bila kujua hasa ni ugonjwa gani au alipatwa na nini mwanangu. Niliongea na madaktari, wakanieleza kuwa mwanangu alitokwa na damu nyingi sana mpk ndani ya jeneza. Uchungu mkubwa na kuchanganyikiwa vilinipata bila kujua hasa nini cha kufanya.

Niliporudi msibani nilishangaa kumkuta mume wangu akiwa na pete kubwa ya dhahabu yenye kinakshi cha tanzanite katikati mkono wa kuume. Nilipomuuliza akaniambia amenunua mjini bei ghali sana na pia ameninulia na mimi aina km hiyo ya pete. Sikujua chochote nikaipokea ile pete km zawadi nikawa naivaa. Pia akaniambia kuna kanisa jipya limeanzishwa hapa mjini ndio tutakua tunasali. Huko tulikutana na watu mbalimbali wa mataifa mengine na ibada zilikua ni za kiingereza. Tulienda kutambulishwa na mume wangu kwa mchungaji ambaye nayepia alikua amevaa pete km ya mume wangu-sikujali sana kwa siku hiyo. Nilijisikia vzr sana kwani huko nilimuona mume wangu akifurahia na kujitoa km zamani. Pia tulipata marafiki wengi akiwemo familia moja ya wakameruni waliokua karibu sana sisi. Tukahamia huko.

Baada ya muda baada ya kuipata ile pete na kurudi chuoni na kujiunga kanisa jipya huku Arusha, sikupenda tena kwenda kanisani wala kujishughulisha na mambo ya huduma kama awali. Nilijiona mwenye majukumu mengi sana na sina muda wa mambo ya kanisani na huduma. Wenzangu waliponiuliza, niliwajibu kuwa niko bize sana na masomo na shughuli za kikazi. Nikawa mzembe sana ktk mambo ya imani na huduma.

Lkn siku moja Nikiwa Dar wakati wa fellowship za chuoni, ndugu mmoja alitutembelea akahubiri kwa nguvu sana akatuambia kuna mtu amezingirwa na roho mbaya za kichawi zinazotafuta kumuangamiza na familia yake-sikuelewa hata kidogo wala hakupita mtu yeyote mbele siku hiyo. Yule muhuburi alilia sana kwa uchungu mpk mwisho wa ibada.

Baada ya kumaliza masomo mwaka 2007 nilirudi Arusha. Nikapata marafiki wengi na mitandao mbalimbali ya kibiashara ndani na nje ya nchi. Pesa ilikuwa nyingi mpk nikashangaa kuwa ni baraka za namna gani.

Mwaka 2009 siku moja nilishtuka na kitu kimoja pale mume wangu aliposahau pete yake (ile nyingine anayovaa mkono wa kuume sio ya ndoa) nyumbn. Mimi bila kujua nilipoiona niliihifadhi kwenye mkoba wangu nikaondoka nayo. Kumbe nyuma yangu, mume wangu alirudi nyumbn ghafla na kuitafuta sana pete akanipigia simu nikamwambia ninayo kwenye mkoba aje nilipo aichukue. Cha ajabu alipokuja ili nimpe ile pete haikuwepo tena kwenye mkoba. Nilijikagua na kuwauliza wafanyakzi wenzangu lkn pete haikuonekana. Mume wangu alichanganyikiwa na kunishambulia kwa makofi na matusi akiwa mwenye hasira kubwa- sikuwahi kumuona mume wangu akiwa mwenye hasira na ghadhabu kubwa kiasi kile. Alinidhalilisha hadharani mbele ya wafanyakazi wenzangu na kuniamrisha twende nyumbn haraka. Ofisi yao ilikua nikaribu na ofisi kwangu lkn alinipandisha gari yake na tukaelekea nyumbn bila kupitia ofisini kwao. Kwenye gari tulikua tunagombezana kwani nilijisikia kudhalilishwa kwa hali ya juu sana.

Tulipofika nyumbani, ugomvi ulikua mkubwa sana na sana mume wangu alinipiga kweli. Baadaye watu walikuja lkn hawakuweza kuingia ndani kwani kulikua kumefungwa. Mume wangu alinifungia kwenye chumba kimoja na nikamsikia akiwapigia simu watu kadhaa huku akilia km mtoto. Sikuelewa kwa kweli. Mchungaji wa kule kwenye kanisa letu alikuja na mtu mmoja ambaye alikua ni rafiki wa karibu wa familia yetu lkn foreigner.

Walipofika waliongea na mume wangu kwa muda afu wakaondoka. Mume wangu akaja akanifungulia mlango akaniambia tuongee- wakati huo alikua mpole na mkimya asiyelia tena.

Akaniambia kuwa ile pete iliyopotea ilikua ndio pete ya maisha yetu. Alipewa na huyo mchungaji na ilikua inamasharti makubwa kuwa lazima aivae yeye tu na isikae muda mrefu nje ya kidole chake. Kwa ufupi pete hiyo haikuwa ya kawaida na ile pete ilikua ni yule mtoto wetu (Alfred) aliyekufa miaka kadhaa iliyopita. Nilishtuka kujua hata ile pete niliopewa mimi haikuwepo mkononi mwangu wakati huo. Ilikua imetoweka, nikazimia kusikia maneno hayo. Nilipozinduka nilijikuta nyumbn kwa mchungaji nikiwa nimelazwa kitandani. Kumbe nilipozimia nilipelekwa hospitali na pia mume wangu akakamatwa na polisi akawekwa lokap lkn akaachiwa bady kutokana na ushawishi wake pale polisi na alipowaelezea anavyojua yeye. Alipotoka akaja hospitali wakanichukua mpk nyumbn kwa mchungaji. Nilipozinduka nikamuona mchungaji na yule rafiki yetu mkameruni walikua wamevaa pete km ile ya mume wangu iliyopotea. Hawakunisemesha kitu wala hawa kuomba lkn waliondoka kule chumbani wakiniacha na mume wangu mara baada ya kupata ufahamu.

Mume wangu alinichukua mpk nyumbn, tulipofika hatukuongea kitu mpk asbh. Yeye alienda mjini baadaye akarudi akiwa bado mwenye mawazo na wasiwasi mkubwa. Siku hiyo ikapita na kesho yake. Marafiki zangu walikuja kunitembelea ili kunipa pole lkn hawakuruhusiwa. Kumbe mume wangu aliwaambia watu pamoja na ndugu zangu kuwa nimemuibia mali nyingi sana nimeficha kusikojulikana. Ndugu zangu walipokuja aliwaruhusu kwa masharti kuwa nisiwaambie ukweli. Akanitisha kuwa nikisema ukweli tutakufa wote.

Maisha yaliendelea kwa siku kadhaa, nikaendelea na kazi lkn nikiwa mwenye mawazo makubwa. Nikaomba off kazini kwa muda ili nipate ahueni. Mume wangu naye akaomba off pia tukawa tunashinda ndani tu. Nyakati za usiku nikiwa nimelala mara nyingi niliota ndoto kuwa Alfred mwanangu ananiita yuko barabarani anahangaika akiwa analia. Nikimwambia mume wangu ananiuliza ni wapi eneo gani hasa, nikimtajia eneo nilipoota ananiambia hapo ndipo pete ilipo kwa hiyo ataifuata- nakweli mara nyingi alikua anaamka anaondoka eti kuifuata hilo eneo nilipomuona mtoto wangu kwenye ndoto.

Pete ile haikuwahi kuonekana na maisha yetu yalianza kuporomoka siku hadi siku. Mume wangu hakufurahi tena. Alikua ni mtu mwenye majonzi na wasiwasi sana juu ya maisha yetu siku zijazo. Wakati huo aliwafukuza wafanyakazi wote wa nyumbn na alininyanganya simu zote na alifungia ndani nisitoke nje

Siku moja ikitokea mjini katika mizunguko yake alinijia na habari mpya akidai kuwa ndio suluhisho la tatizo letu. Aliniambia kuwa ili turejee ktk maisha yetu ya kawaida inabidi tumuue mtoto wetu Minza pia kwa siku zote za maisha yetu kuanzia siku hiyo itakua ni marufuku kufanya mapenzi kwa njia ya kawaida ila tu kinyume na maumbile (yaani awe ananiingilia kinyume na maumbile ya mwanamke). Akaniambia hakuna namna nyingine ya kurejesha maisha yetu zaidi ya hivyo. Nilishtuka sana nikaogopa mno. Nilimlaumu sana mume wangu kwanini alijiingiza ktk maisha hayo- ndipo akanieleza hbr kamili kuwa mafanikio yetu yote yametokana na mfumo huo wa maisha tangu siku ile aliporudi ile safari tukiwa Karatu. Kumbe siku ile alikua ametoka kwa mganga aliyepelekwa na yule rafiki yake.

Nilimshauri mume wangu twende kwa mchungaji tukaombewe lkn akasema kuwa tukisema tu kwa watu tutakufa wote. Pia akasisitiza kuwa sisi wote tuko katika mtandao huo kwa hiyo sio rahisi kujiokoa tena. Kesho yake mume wangu alinikumbushia tena akasema ni lazima tufanye hivyo na pia sio kwa kulazimisha inatakiwa iwe kwa hiari ili tupate faida kwa haraka. Bado nilikataa, sikuwa tyr kufanya hivyo. Nilimuomba mungu usiku na mchana atusaidie. Lkn mume wangu Alinitisha sana na kunifinya mwili ili nikubali kwani alikua mwenye hasira na ghadhabu kubwa. Pia alinifungia ndani ili nisitoke nje. Pia alisisitiza nisiombe kbs. Maisha yaligeuka kuwa jehanam.

Siku km mbili zililizofuata tulipigiwa simu kutoka shuleni kwao na mtoto wetu kuwa Minza ametoweka shuleni hajulikani alipo. Tulikwenda haraka kujua hatma ya mtoto wetu. Niliogopa zaidi kwani nilijua labda ndio keshapatikana- japo mume wangu alionekana kuwa si mwenye wasiwasi ht kidogo. Nilianza kukumbuka kukemea na kuomba Mungu atusaidie lkn mume wangu alinikataza nisiombe kbs. Akanizabua kibao kikubwa mdomoni tukiwa kwenye gari mpk damu ikatoka mdomoni. Nikisikia uchungu mkubwa zaidi kwanini maisha yalikua yanaenda hivyo ghafla au nini faida ya kuishi basi.

Tulisafiri siku nzima mpk kufika shuleni kwa Minza mwanangu. Kitu cha ajabu ni kwamba tulimkuta mtoto akiwa hospitali amelzwa haongei wala hajitambui- na taarifa zinasema alikutwa chumbani(hostel) kwao mchana huo akiwa anatokwa na damu nyingi.

Siku kadhaa bdye tulipewa mtoto wetu baada ya kupata nafuu tukarudi naye nyumbn kwa matibabu zaidi. Minza aliendelea kuugua sana bila nafuu na hakuweza kuzungumza kitu alikua ni mtu wa kulala kitandani na kutazama tu.

Ilipita miezi kadhaa maisha hayo yakawa yamechukua sura ya familia yangu. Miradi kadhaa tuliyoifungua mjini ilikua imefungwa, pia kazini kwangu nilikua nakwenda kwa shida sana. Uwezo wangu wa akili na kiutendaji ulipooza sana. Nilijiingiza kwenye chama cha ulevi wa pombe km mume wangu ili kupoteza machungu na kupunguza mawazo. Lkn hai kusaidia. Lkn kule kanisani tuliendelea kwenda na mume wangu aliendelea na kazi kule UN.

Siku moja mume wangu aliniambia tunakwenda shambani kwa siku kadhaa twende wote- tulijiandaa tulikwenda pamoja. Tulipofika huko, tulijumuika pamoja na mchungaji na yule rafiki yetu mkameruni. Tulifurahi na kunywa na kula mpk usiku kwa siku hiyo ya kwanza. Kesho yake asubuhi na mapema niliitwa na mume wangu kuwa kuna kikao- Cha ajabu ni kwamba asbhu hiyo mchungaji na yule mkameruni walikua wamevalia mavazi ya kitamaduni kupitiliza kawaida yao. Tulikwenda mpk vichakani zaidi kwani walisema kuna maongezi muhimu sana.

Tukiwa huko yule mchungaji alitueleza waziwazi kuwa yeye ni mtu mwenye nguvu nyingi sana na amewasaidia wengi sana. Na pia hata zile mali za kwanza na kufanikiwa kwetu ni yeye ndiye aliyetusaidia kwa nguvu zake. Na nguvu hizo ni zilitokana pete yake. Pete yake ndio inayompa nguvu na kumletea bahati na mvuto kwa watu.

Kwa kuwa tulikua tumeshindwa kutekeleza sharti la kwanza la kumuua Minza na muda ulikua umepita basi, kuna sharti lingine la mwisho

Kwa hiyo, akasema anao uwezo wa kutupatia pete nyingine lkn ndio kwa masharti. Na leo hapo yuko tyr kutusaidia tena ili tufanikiwe na tusife- kwani tulikua tumefanya makosa makubwa sana kupoteza ile pete ya awali.

Akatoa masharti ili tupate pete nyingine inabidi mimi nikubali pale niingiliwe kimwili nao wote watatu. (yaani nifanye mapenzi na wote watatu pale kichakani hadharani na mmoja baada ya mwingine akianza mume wangu). Vinginevyo mume wangu atapoteza maisha pale pale na mimi pia ningekufa siku zijazo au ningekua kichaa. Nilishtuka nikaogopa sana, nikaanza kupiga mayowe huku nilikimbia kuelekea kwa mume wangu- nililia sana kwa uchungu huku nikitaja jina la mume wangu kwa kumlaumu kwanini alijiingiza kwenye mambo hayo. Mume wangu alinisihi nikubali ili tusife kwani hakukua na namna nyingine.

Sikukubali. Nilianza kukimbia kuelekea barabarani kuhofia usalama wangu kwani niligundua mume wangu hakuwa na uwezo tena wa kunisaidia au kujiokoa. Nilpofika mahala tulipopark magari yetu sikuona gari ht moja. Nikiwa ktk hali ya kukimbia na kujiokoa huku nikipiga mayowe niliwaona yule mchungaji na yule mkameruni wamenitokea nyuma na mbele yangu. Ghafla yule mchungaji aliniwekea mkono kichwani nikaanguka chini nikapoteza fahamu.

Niliporejea fahamu zangu ni siku nilipojikuta niko katikati ya kundi la watu walinisimamia na kuniangalia kwaumakini mkubwa sana. Kumbe ilikua ni kwenye maombezi. Fahamu zangu zilinirejea na kujitambua japo nilikua nimeharibika mwili na mavazi machakavu pia nikiwa nimefungwa kwa kamba ngumu sana. Nikifanikiwa kuwatambua baadhi ya ndugu jamaa na marafiki waliokuwepo pale.

Kwa masaa kadhaa nilijisikia kupumbaa kama mjinga bila kujua nifanye nini. Alitokea mtu mmoja akaniambia pole. Akaniuliza kama ninajisikiaje kwa wakati huo. Nikamuelezea. Kisha nikamuhoji kuwa hapo ni wapi- akaniambia kuwa ni kituo cha maombezi na yeye ndiye mchungaji.

Inasemekana kuwa siku hiyo nilikua nimefunguliwa kutoka katika ukichaa ulionisumbua kama miaka mitatu na nusu. Katika muda wote huo niliishi msituni km mnyama. Nilitafutwa na ndugu zangu kwa muda mrefu sana bila mafanikio. Hakuna mtu alijua mimi au mume wangu tulikua wapi.

Baadaye Nilipouliza kuhusu mwanangu Minza na mume wangu, nijibiwa kuwa waliokufa miaka mitatu na nusu iliyopita. Ndipo nikakumbuka mambo magumu ya maisha yaliyonipata. Nilitunga msiba mkubwa upya kabisa. Nililia sana na kujionea huruma kama yatima asiye na msaada. Sina cha kusema zaidi ya kumshukuru Mungu kwa yote. Hata uhai nilionao leo ni Mungu tu amenisaidia.

If you have any question or need more information, ask/search it here

More results...

Generic selectors
Exact matches only
Search in title
Search in content
Post Type Selectors
Filter by Categories
1000+ Best Jokes That You Will Find Absolutely Hilarious
1000+ Best Quotes to Brighten your Day
1000+ Inspiring Real Stories
1000+ Riddles with Answers
Afya na Ustawi wa Wanaume
Afya na Ustawi wa Wanawake
Afya ya Akili na Ustawi
Afya ya Mwili na Mazoezi
All you need to Know About Virgin Mary Mother of God Jesus Christ
Amazing Real African Stories
Best Christian Quotes to Support your Faith
Best Health and Wellness Improvement Tips
Business and Entrepreneurship Secrets
Business Innovations Development Secrets
Business Planning and Strategic Management Tips
Career Development and Success Techniques
Chemsha Bongo: Maswali na Majibu
Christian Articles to Build your Faith
Christian Reflections to Build your Faith
Christian Teachings to Strengthen Your Faith
Climate and Environment
Communication and Interpersonal Skills Techniques
Community and Social Development
Decision Making and Problem Solving Strategies
Detailed Elaboration of Global Contemporary Issues
Dhana ya Muungano wa Mataifa ya Afrika: Mikakati ya Kuunda "United States of Africa"
Digital Marketing Tips
Disease Prevention and Management
Dondoo za Mapishi na Lishe
Dondoo za Urembo na Mitindo
Emotional Well-being Techniques
Entrepreneurship Development: Secrets of Becoming a Successful Entrepreneur
Fahamu kwa Undani Kuhusu Bikira Maria: Mama wa Yesu Kristo na Mama wa Mungu
Family/Parenting, Love and Relationship Techniques
Finance and Money Matters Techniques
Financial Management and Wealth Creation Tips
Financial Management Tips for Your Business
Fitness and Exercise
Funny Questions with answers
Global Cooperation for Peace and Unity
Global Poverty Alleviation and Sustainable Development
Global Sustainable Resources Utilization and Environment Conservation
Hadithi nzuri za Mafundisho kwa Ajili ya Watoto
Hadithi za Kiswahili: Historia, Mapenzi na Maisha
Hadithi za Kusisimua za Matukio ya Kweli ya Kihistoria
Hadithi za Kusisimua: Hadithi za Biblia
Hali ya Hewa na Mazingira
Health and Lifestyle Tips and Techniques
Healthy Aging and Longevity
Healthy Cooking and Meal Preparation
Healthy Habits and Behavior Change
Ifahamu Huruma ya Mungu
Injili na Mafundisho ya Yesu
Inspiring Historical Stories From all Over the World
Inspiring Stories From All Over the World
International Relations and Cooperation
Intimacy and Connection Building Tips
Jinsi ya Kuboresha namna Unavyowasiliana: Ujuzi wa Mawasiliano
Jinsi ya Kujijengea Mtazamo na Fikra Chanya
Kujenga Jamii na MIji Endelevu
Kupunguza Umaskini na Maendeleo Endelevu
Kuvunjika kwa Mahusiano ya Mapenzi: Kuvunjika na Uponyaji
Kuzuia na Usimamizi wa Magonjwa
Lishe na Ulaji wa Afya
Maendeleo ya Jamii na Kijami
Mafundisho Makuu ya Dini: Makala za Dini
Mafundisho Makuu ya Upendo Wa Kipekee Wa Mungu
Mafundisho ya Katekisimu
Mafundisho ya Msingi ya Kanisa Katoliki: Makala za Katoliki
Mafundisho ya Nguvu ya Damu ya Yesu
Mahusiano ya Kimataifa na Ushirikiano
Maintenance of Spirituality and Inner Peace
Makala za Tafakari Kwa Wakatoliki
Malezi na Afya ya Familia
Mambo Muhimu ya Msingi Unayopaswa Kufahamu Kuhusu Afrika
Mambo ya Sasa ya Amerika ya Kaskazini na Kusini
Management of African Natural Resources for African Economic Development
Masomo ya Misa ya Kanisa Katoliki
Mastering Leadership and Human Resources Management
Matumizi Endelevu ya Rasilimali na Uhifadhi wa Mazingira
Mbinu za Kilimo na Ufugaji Kukuongezea Mapato
Mbinu za Kubadilisha Mfumo wa Mawazo na Kujenga Tabia Chanya ya Waafrika
Mbinu za Kuboresha Afya na Ustawi wako Binafsi
Mbinu za Kuboresha Afya ya Kihisia Katika Mahusiano
Mbinu za Kufanya Maamuzi na Kutatua Matatizo: Uamuzi na Ushughulikiaji wa Matatizo
Mbinu za Kujengea Afrika na Waafrika Uhuru na Uwezo wa Kujitegemea
Mbinu za Kukufanya Uwe Mjasiriamali Mwenye Mafanikio: Maendeleo ya Ujasiriamali
Mbinu za kukuza Ujasiri wa Kibinafsi na Heshima ya Kujiamini
Mbinu za Kuongeza Ukaribu na Ushirikiano
Mbinu za Kupangilia Biashara na Usimamizi Mkakati
Mbinu za Kusimamia Pesa na Mambo ya Kifedha kwenye Mahusiano
Mbinu za Kutunza Familia na Malezi ya Watoto
Mbinu za Kuwa na Maendeleo ya Kazi na Mafanikio
Mbinu za kuwa na Maisha Mazuri ya Kikristo
Mbinu za kuwa na Misingi imara ya Upendo na Mapenzi
Mbinu za Mauzo na Masoko Kuboresha Biashara Yako
Mbinu za Mawasiliano na Ujuzi wa Mahusiano
Mbinu za Ubunifu Katika Biashara na Maisha: Maendeleo ya Ubunifu
Mbinu za Ujasiriamali na Biashara Kufanya tofauti
Mbinu za Uongozi na Ushawishi
Mbinu za Uongozi na Usimamizi wa Rasilimali Watu
Mbinu za Usimamizi wa Fedha Katika Biashara
Mbinu za Utatuzi wa Migogoro
Mbinu za Uwezo wa Kihisia na Ujuzi wa Kujitambua
Meditation and Yoga
Men’s Health and Wellness
Mental Health and Well-being
Methali za Kiswahili na Maana zake
Mikakati ya Uhifadhi wa Utamaduni na Urithi wa Kiafrika
Mipango na Mikakati ya Usimamizi wa Maliasili za Afrika
Misemo ya AckySHINE
Misingi ya Ndoa Yenye Mafanikio: Ndoa na Kujitolea
Nguvu na Uwezo wa Roho Mtakatifu
Njia za Kujenga Udini na Amani Yako ya Ndani
North and South America Contemporary Issues
Nukuu ya Mistari ya Biblia
Nukuu za Dini
Nutrition and Healthy Eating
Parenting and Family Health
Pembejeo Bora za Kilimo: Bidhaa za Kilimo
Personal Development Strategies and Tips
Promotion of Good Governance and Management of Social Services
Promotion of Sustainable Cities and Communities
Recommended African Development Strategies for Building Independent and Self Reliance Africa Community
Recommended Beauty and Fashion Tips
Recommended Christian Daily Readings
Recommended Conflict Resolution Tips
Recommended Emotional Intelligence and Self-Awareness Tips
Recommended Family and Parenting Techniques
Recommended Leadership and Influence Techniques
Recommended Relationships and Social Skills Techniques
Recommended Strategies for Preservation of African Culture and Heritage
Recommended Technique to Build Self-Confidence and Self-Esteem
Relationship Breakups and Healing Tips
Sala za Katoliki: Sala Muhimu Kwa Mkristu Mkatoliki
Sales and Marketing Tips for Your Business
Sayansi, Teknolojia, na Ubunifu
Science, Technology and Innovation
Selected Christian Prayers to Support your Prayer Life
Shine Ads
Siri ya kuwa na Familia Nzuri ya Kikristo
Siri za Familia, Mapenzi na Mahusiano
Siri za Kuwa na Afya Bora na Utimamu
Siri za Mahusiano Bora na Ujuzi wa Mambo ya Kijamii
Siri za Nguvu ya Jina la Yesu
Siri za Usimamizi wa Fedha na Utengenezaji wa Utajiri
SMS za AckySHINE: SMS Nzuri za Mapenzi na Mahaba Kwa Mpenzi Wako
Special Dedications: 1000+ SMS Messages to Build your Love Life
Stadi za Maisha: Mbinu za Maisha ya Kipekee
Strategies on Changing Mentality and Building Positive Mindset
Strategies to Strengthen your Marriage and Build Commitment
Strategies to Unite Africa: Building a Better World for African Community
Strategies Towards Formation Of The United States Of Africa
sw-picha
Tabia Njema za Afya na Badiliko la Mwenendo
Tafakari ya Kina na Yoga
The Best Love and Romance Techniques
Tips to Develop Positive Mindset and Positive Thinking
Ujana na Makuzi | Mapenzi na Ngono Salama
Ukombozi kutoka Utumwa Wa Dhambi na Shetani
Umoja na Ushirikiano wa Jumuiya ya Kanisa
Umoja wa Afrika: Mikakati ya Kuunganisha nchi na Watu wa Afrika
Understanding African Development: All You Need to Know About Africa
Understanding Communication Skills and Technics
Upishi na Maandalizi ya Milo yenye Afya
Usawa wa Kazi na Maisha
Ushirikiano wa Kimataifa kwa Amani na Umoja
Usimamizi wa Uzito na Taswira ya Mwili
Utawala Bora na Usimamizi wa Huduma za Kijamii
Uzee Mwema na Maisha Marefu
Vichekesho vipya 1000+: Vichekesho vya AckySHINE
Videos in English
Videos za Kiswahili
Weight Management and Body Image
Women’s Health and Wellness
Work-Life Balance
Yafahamu kwa Undani Mambo ya Sasa ya Kimataifa
Melkisedeck Leon Shine

Editor: Melkisedeck Leon Shine. About Me | Contact Me | LinkedIn | TikTok | WhatsApp

Read and Write Comments

Views: 3

Shopping Cart