Ujana na Makuzi | Mapenzi na Ngono Salama

Kwa nini watu wasio na ualbino wanaogopa kuoa Albino kwa imani kuwa watawazalia watoto Albino?

Ualbino ni hali ya
kurithi, hii inamaanisha
kuwa unapata ualbino
kutoka kwa wazazi
wako. Watu wawili
weusi wanaweza kupata
Albino endapo kila
mmoja wao atakuwa
na kinasaba cha ualbino.
Hali hii huwezi kuiona
au kuijua. Unaweza tu
kuitambua baada ya
kujifungua. Takribani
mtu mmoja katika watu
70 ana kinasaba cha
ualbino lakini si rahisi
kujua ni nani anacho.
Endapo Albino ataoa
mwanamke mweusi,
uwezekano wa kuzaa
Albino ni mdogo sana.
Albino wengi waliooa au
kuolewa na watu weusi
wamepata watoto
ambao ni weusi.

Kwa upande mwingine, wanandoa ambao wamekwisha
pata mtoto Albino kuna uwezekano wa kupata mtoto mwingine
Albino katika uzazi wa pili.
Kuzaliwa Albino ni lazima mtoto huyo arithi vinasaba vya
ualbino kutoka kwa wazazi wote wawili, yaani mama na baba.

Watu wanaamini kuwa Albino wana joto katika mapenzi kuliko watu weusi, Je, hiyo ni kweli?

Hii siyo kweli,
tofauti
baina ya Albino
na mtu a s i
ekuwa na ualbino
i m e e l e z w a
hapo mwanzoni
ambapo tofauti
ipo tu kwenye
muonekano wa
rangi ya ngozi,
nywele n a macho. Mifumo yao yote mingine ya mwili iko sawa na watu
wasio na ualbino.
Watu wanaweza tu kuanzisha uvumi kama huo popote pale.
Ipo pia mifano kama: Wajerumani wanaamini kuwa Wafaransa
wana joto katika mapenzi, Wazungu pia huamini kuwa Waafrika
wana joto n.k. Hizo ni hisia tu na siyo ukweli. Katika jamii wapo
watu ambao wanapenda kufanya ngono sana, wapo wa wastani
na wapo wale ambao hawajisikii msukumo wa kujamiiana. Uvumi
huu unatokana na mawazo ya kifikra na siyo ukweli halisi.

Kwa nini Albino wanatengwa katika masuala ya mapenzi na wale watu ambao siyo Albino?

Watu huogopa kujaribu vitu au mambo ambayo hawajayazoea
au yale ambayo yapo tofauti. Jinsi unavyozidi kujua ukweli
kuhusu sababu za ualbino ndipo unavyoweza kujenga mtazamo
chanya ikiwemo kuwapenda.
Wapo pia watu wengi katika jamii yetu ambao wana mahusiano
ya kimapenzi na Albino na ambao wapo katika ndoa. Watu
wengine katika jamii wanapoona mifano hiyo inasaidia katika
kuondoa wasiwasi na kuondoa imani potofu.

Kama Albino akiathirika na VVU anaweza kutumia ARVs kama watu wengine?

Katika suala hili la UKIMWI hakuna tofauti yoyote kati ya
Albino na watu wengine katika jamii. Albino wanaweza kupata
maambukizo kama watu
wengine, na mahitaji yao ni yaleyale, kijamii, kisakolojia na kiafya.
Albino watapewa ARVs kama watu wengine kwa kufuata
utaratibu uleule wa matibabu ya UKIMWI kama wanavyofanyiwa
watu wasio Albino. Kwa hiyo kama Albino anakataliwa kupewa
huduma za dawa za kufubaza VVU (ARVs) basi atoe taarifa
kwa vyombo husika ukiwemo uongozi katika jamii au kwenye
Chama cha Albino ili waweze kuwasaidia kufuatilia haki zao.

Watu wanasema kuwa unaweza kupona UKIMWI kwa kujamiiana na Albino. Hii ni kweli?

Watu wanaweza kuvumisha uongo wowote ili kupotosha
ukweli na kufanya mambo yao maovu wanayoyapenda. Wapo
wanaosema kuwa unaweza kupona UKIMWI kwa kujamiiana na
bikira, mtu mlemavu au Albino, hizi ni imani potofu na hazina
msingi wowote.

Imani hii kuwa kwa kujamiiana na Albino mtu anaweza kupona
VVU / UKIMWI siyo kweli kabisa. Mpaka sasa hakuna tiba
ya UKIMWI ingawa kuna maendeleo makubwa yanayotokana
na dawa za kufubaza VVU (Anti-retrovirals kwa kifupi ARVs).
ARVs zimesaidia watu wengi wanaoishi na VVU kuishi maisha
bora kiafya lakini ARVs haziponyi UKIMWI. Mtu akisha athirika
na VVU ataendelea kuwa na maambukizo kwa maisha yake yote
na hakuna uponyaji wowote unapatikana kwa kujamiiana na
Albino.
Imani hizi potofu pia zinaathiri makundi mengine katika jamii
yetu, kwa mfano; kujamiiana na bikira kunaweza kuponya
UKIMWI, hii imepelekea kuongezeka kwa vitendo vya ubakaji
wa watoto. Ni muhimu kwa vijana Albino kufahamu ukweli
kuhusu VVU/UKIMWI na pia mila hizi potofu ili waweze
kujikinga.

Shopping Cart