Ujana na Makuzi | Mapenzi na Ngono Salama

Je, gongo na sigara husaidia uyeyushaji wa chakula?

Ni imani na fikra potofu kwamba, ukinywa gongo au kuvuta
sigara kwa kiasi kidogo baada ya chakula itasaidia kuyeyusha
baadhi ya vyakula vya mafuta. Pombe inaweza hata kupunguza
mtiririko wa kawaida wa kimiminika muhimu kwa uyeyushaji wa
chakula (tindikali) na hivyo kuchelewesha kuliko kurahisisha
uyeyushaji wa chakula.
Nikotini ya sigara kwa upande mwingine inaongeza kazi katika
utumbo mpana na hivyo kurahisisha uyeyushaji wa chakula.
Lakini kwa upande mwingine nikotini huchochea utengenezaji
wa tindikali tumboni ambayo husababisha maumivu ya tumbo.

Je, ni kweli kwamba mtu anayekunywa pombe anaishi kwa muda mrefu kuliko yule ambaye hanywi kabisa?

Si kweli. Mpaka sasa wanasayansi hawajathibitisha kwamba
mtu anayekunywa pombe kidogo ndiye anayeishi kwa muda
mrefu. Kwa ujumla, watu wanaoishi katika hali ya usafi, afya
njema na maisha yenye furaha ndio wanaoishi kwa muda
mrefu kuliko wale ambao hawajijali kimwili na kiakili. Kimsingi,
kunywa pombe ni kutojijali. Unywaji wa pombe kwa kiasi hauna
madhara, lakini inakupasa kuwa macho katika unywaji huo ili
usizidishe kupita kiasi.

Je, ukinywa pombe unaongeza damu?

Si kweli.
Pombe haiongezi damu, vitamini wala nguvu. Ukweli ni kwamba unywaji pombe kupita kiasi huvuruga ufyonzaji wa vitamini na madini kutoka kwenye chakula kuingia mwilini.

Vitamini ni muhimu kwa kuimarisha kinga ya mwili ambayo inasaidia kujikinga na magonjwa, pamoja na maradhi kama UKIMWI. Kwa hivyo, unatakiwa uhakikishe unakula matunda na mboga za majani kwa sababu vinakuongezea vitamini.

ATHARI ZA ULEVI KATIKA JAMII

Watu wanokunywa kupitia kiasi huathiri jamii kwa njia
mbalimbali. Madhara mengine hutokea kwa kuwa wanafanya
vitu ambavyo wasingevifanya iwapo wasingekuwa wamelewa.

Watu wakilewa, huweza kuwa na hasira, wagomvi hivyo basi
huwadhuru wengi kiakili na kimwili. Isitoshe, ajali nyingi za
kazini na barabarani hutokea watu wakiwa wamelewa. Mara
nyingi watu wasiokuwa na hatia na vilema hupoteza maisha yao
kutokana na ajali zinazohusiana na ulevi.

Watu wanaokunywa
pombe kupita kiasi hupunguza uangalifu na hivyo basi kuchangia
katika kuenea kwa VVU kwenye jamii. Watu wanaokunywa pombe
wanaweza pia kufanya ujambazi katika jamii. Pia wanaokunywa
kupita kiasi si wafanyakazi wa kutegemewa kwani hutumia
muda mwingi nje ya sehemu zao za kazi.

Watu waliozoea kunywa pombe nyingi hupoteza pesa zao nyingi
kununua pombe na muda wao mwingi kufikiria jinsi ya kupata
pesa za kunywea pombe.

Kutokana na gharama za kununua
pombe familia zao hukosa pesa za vitu muhimu kama kodi ya
nyumba, ada na sare za shule na chakula.

Vijana wanaokunywa pombe huanza kuiba pesa nyumbani kwao
ili kununulia pombe. Matumizi mabaya ya pombe mara nyingi
husababisha matatizo au kuvunjika kwa familia, au urafiki.

Vilevile husababisha matokeo mabaya shuleni au kuacha kabisa
shule, hali ambayo inaweza kusababisha kukosa nafasi za kazi,
kujitegemea wewe mwenyewe na kusaidia famila yako na jamii.

Shopping Cart