Jinsi ya kutibu chunusi kwa kutumia papai
Dawa nyingine madhubuti ya chunusi ni papai. Tunda hili ni moja ya matunda yanayotumika kwa ajili ya urembo hasa kwa wanawake.
Dawa nyingine madhubuti ya chunusi ni papai. Tunda hili ni moja ya matunda yanayotumika kwa ajili ya urembo hasa kwa wanawake.
Mvuke husaidia kusafisha ngozi. Ni rahisi sana kutumia mvuke kutibu chunusi.
Chemsha maji kwenye sufuria jikoni funika na uache nafasi kidgo ya mvuke uwe unatoka, kisha chukua taulo na ujifunike usoni huku ukisogelea karibu na mvuke unapokea na uruhusu mvuke huo ukupate kwa mbali.
Baki hapo kwa dakika 5 mpaka 10 hivi huku ukiwa umetulia (relaxed). Huu mvuke utakusaidia pia kujisikia mtulivu na kukuondolea mfadhaiko wa akili.
Mwishoni mwa zoezi jisafishe uso wako na maji ya baridi.
Endelea kusoma makala hii kujifunza zaidi dawa nyingine za asili za kutibu chunusi.
Mchele wa basmati – 3 Vikombe
Dengu – 2 vikombe
Viazi – 3 vikubwa
Kitunguu – 2 kubwa
Nyanya – 2
Pilipili mbichi kubwa – 3
Pilipilimanga – ½ kijiko cha chai
Garama Masala (bizari mchanganyiko) -1 kijiko cha chai
Supu ya vidonge (stock cubes) – 2 vidonge
Chumvi – kiasi
Mafuta – ¼ kikombe
Zaafarani – 1 kijiko cha chai
Dengu kama sio za tayari kwenye kopo, roweka na zichemshe hadi ziwive
Zaafarani – iroweke katika maji ya dafu dafu (warm) ya chini ya robo kikombe weka kando.
Osha mchele, roweka.
Menya viazi na vitunguu, katakata vitunguu, na nyanya , weka kando.
Katakata viazi vipande vidogo vidogo kwa umbo la mchemraba (cubes).
Katika sufuria tia mafuta yakipata moto, tia viazi ukaange kidogo kwa moto mdogo mdogo hadi kukaribia kuwiva, toa weka kando.
Kaanga vitunguu hadi vigeuka rangi ya hudhurungi isiyokoza (light brown) kisha tia nyanya ukaange kidogo.
Tia vidonge vya supu (stock cubes) uvivuruge katika mchanganyiko, katakata pilipili mbichi kwa urefu tia, uendelee kukakaanga. Tia bizari, chumvi.
Zima moto, changanya dengu na viazi katika mchanganyiko huo.
Chemsha mchele kama kawaida ya kupika wali mweupe, kiini kiwe kimewiva nusu yake.
Chuja maji kisha changanya katika mchanganyiko wa dengu.
Nyunyizia zaafarani, uchanganye wali na mchanganyiko kidogo tu.
Funika acha uive katika mtoto mdogo mdogo au tia katika oveni hadi uive kama kawaida ya kupika wali.
Pakua katiha sahani na tolea na samaki yoyote wa kukaanga.
Mchele – 4 vikombe
Kuku – 1
Vitunguu – 3
Nyanya/tungule – 4
Zabibu kavu – ½ kikombe
Tangawizi na kitunguu (thomu/galic) – 2 vijiko cha supu
Pilipili mbichi iliyosagwa – 1 kijiko cha supu
Mtindi (yoghurt) – 2 kijiko cha supu
Masala ya tanduri – 2 vijiko vya supu
Pilipili manga – 1 kijiko cha chai
Hiliki – ½ kijiko cha chai
Mdalasini – kijiti kimoja
Ndimu – 3 vijiko vya supu
Chumvi – kiasi
Zaafarani (saffron) – 1 kijiko cha chai
Mafuta – ½ kikombe
Baada ya kumsafisha kuku, mkate vipande vikubwa vikubwa kiasi upendavyo, muoshe mchuje atoke maji.
Katika bakuli, tia tangawizi, kitunguu thomu ilosagawa, pilipili mbichi ilosagwa, chumvi, ndimu, mtindi, masala ya tanduri na uchanganye vizuri, kisha mtie kuku na uchanganye tena na acha arowanike kwa muda wa kiasi saa au zaidi.
Panga kuku katika sinia ya kuchoma ndani ya oveni. Kisha mchome (grill) hadi awive, mtoe acha kando. Mwagia juu yake masala yatakayobakia katika sinia baada ya kumchoma.
Weka mafuta katika karai, tia vitunguu ulivyokatakata, kaanga hadi vianze kugeuka rangi.
Tia nyanya ulizokatakata, tia pilipili manga, hiliki, mdalasini, chumvi, na zabibu. Kaanga kidogo tu yakiwa tayari.
Osha na roweka mchele wa basmati.
Roweka zaafarani kwa maji ya moto kiasi robo kikombe weka kando.
Chemsha maji, tia chumvi, kisha tia mchele uive nusu kiini.
Mwaga maji uchuje mchele kisha rudisha katika sufuria au sinia ya foil. Nyunyizia zaafarini, na rudisha katika moto upike hadi uive kamili.
Epua, kisha pakua wali katika sahani au chombo upendacho, mwagia juu yake masala ya nyanya. Kisha weka vipande vya kuku ulivyochoma, biriani ikiwa tayari
Unga wa mahindi – 4 vikombe
Maji – 6 kiasi
Tia maji kiasi katika sufuria wacha yachemke hasa
Tia unga kidogo kidogo huku ukikoroga mpaka ukamatane
Punguza moto huku ukiendelea kuusonga
Endelea kusonga kwa dakika kadhaa mpaka uanze kuchambuka
Kisha mimina kwenye bakuli au sahani na itakuwa tayari
Samaki:
Samaki wa Nguru – kiasi vipande 5 – 6
Pilipili mbichi – 3
Kitunguu saumu(thomu/galic) – 5 chembe
Tangawizi mbichi – 1 kipande
Bizari ya samaki – 1 kijiko cha supu
Pilipili nyekundu ya unga – 1 kijiko cha chai
Ndimu – 3 kamua
Chumvi – kiasi
Ukipenda mkate samaki vipande kiasi.
Saga vipimo vyote vinginevyo katika mashine. Mchanganyiko ukiwa mzito ongezea ndimu
Changanya pamoja na samaki upake vizuri vipande vya samaki
Acha kwa muda wa nusu saa vikolee mchanganyiko
Panga samaki katika treya ya kupikia ndani ya oveni, kisha mchome (grill) samaki huku ukigeuza hadi viwive.
Epua weka kando.
Nyanya/tungule – 3
Kitunguu – 2
Bizari ya manjano/haldi – ¼ kijiko cha chai
Mafuta – 3 vijiko vya supu
Tui la nazi zito – 3 vikombe
Chumvi – kiasi
Katakata vitunguu na nyanya vidogodogo (chopped) weka kando
Weka mafuta katika karai au sufuria, kaanga vitunguu hadi vianze kugeuka rangi
Tia nyanya kaanga pamoja na tia bizari ya njano/haldi .
Tia tui la nazi, chumvi koroga .
Mwishowe tia vipande vya samaki na rojo lake litakalobakia katika treya, mchuzi uko tayari