Toharani ni mahali gani?
Toharani ni mahali pa mateso zinakosafishwa roho ambazo hazikutimiza kitubio vizuri baada ya kuungama dhambi. (1Kor 3:15, 1Pet 1:7).
Je, hatuwezi kupunguza mateso ya roho za marehemu waliokwenda toharani?
Ndiyo: twaweza kupunguza hata kuyamaliza kwa kuwasalia na kuwapatia rehema na hasa kwa kuadhimisha Misa kwa ajili yao. (2Mik 12:38-46)
Toharani maana yake nini?
Toharani maana yake kuna hali ya muda ambayo huruma ya Mungu inawatakasa marehemu waliofariki dunia katika urafiki naye lakini bila ya usafi kamili unaotakiwa kwa kuingia mbinguni. Sisi tunaweza kuharakisha utakaso wao kwa kumtolea Mungu sala na sadaka, hasa ekaristi. Yuda Mmakabayo “alichanga fedha kwa kila mtu jumla drakma elfu mbili, akazipeleka Yerusalemu kutoa sadaka ya dhambi.
Kwa kufanya hivi alitenda vema na kwa haki, kwa kuwa aliukumbuka ufufuo wa wafu. Maana kama asingalitumaini ya kuwa wale waliokufa watafufuka, ingalikuwa kazi bure isiyo na maana kuwaombea wafu. Lakini kwa kuwa aliufikiri utukufu wa thawabu waliowekewa wale wafao katika utauwa, wazo lake lilikuwa takatifu na la kicho. Ndiyo sababu alifanya upatanisho kwa wafu ili wafunguliwe dhambi zao” (2Mak 12:43-46). Imani hiyohiyo iliongoza Wakristo wa kwanza kuwafanyia marehemu ibada ambayo haieleweki vizuri, lakini hailaumiwi na Mtume Paulo: “Kama wafu hawafufuliwi kamwe, kwa nini kubatizwa kwa ajili yao?” (1Kor 15:29).
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Nguvu hutoka kwa Bwana
Mwamini Bwana; anajua njia
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Sifa kwa Bwana!
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Tumaini ni nanga ya roho
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Rehema zake hudumu milele
Mungu ni mwema, wakati wote!
Rehema hushinda hukumu
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Dumu katika Bwana.
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Imani inaweza kusogeza milima
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Katika imani, yote yanawezekana
Neema ya Mungu inatosha kwako
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Neema na amani iwe nawe.
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Endelea kuwa na imani!
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Nakuombea 🙏
Mungu akubariki!
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Baraka kwako na familia yako.
Mwamini katika mpango wake.
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe