SOMO 1
Kut. 32:15-24, 30-34
Musa aligeuka akashuka katika mlima, na zile mbao mbili za mawe mikononi mwake; mbao ziliandikwa pande zote mbili, upande huu na upande huu ziliandikwa. Na zile mbao zilikuwa kazi ya Mungu, nayo maandiko yalikuwa maandiko ya Mungu, yaliyochorwa katika zile mbao.
Na Yoshua aliposikia kelele za watu walipokuwa wakipiga kelele, akamwambia Musa, Kuna kelele ya vita maragoni. Akasema, Hiyo si sauti ya watu wapigao kelele kwa sababu ya kushinda vitani, wala si sauti ya watu wapigao kelele kwa sababu ya kushindwa; bali kelele za watu waimbao nizo ninazozisikia mimi.
Hata alipyakaribia marago akaiona ile ndama, na ile michezo. Hasira ya Musa ikawaka, akazitupa zile mbao mikononi mwake, akazivunja chini ya mlima. Akaitwaa ile ndama walioifanya, akaichoma moto, akaisaga hata ikawa mavumbi, akainyunyiza juu ya maji, akawanywesha wana wa Israeli. Musa akamwambia Haruni; Watu hawa wamekufanyani hata ukaleta dhambi hii kuu juu yao? Haruni akasema, Hasira ya bwana wangu isiwake; wewe unawajua watu hawa, ya kuwa wamejielekeza kwa mabaya. Maana waliniambia, Katufanyie miungu itakayokwenda mbele yetu, kwa maana mtu huyo Musa, aliyetutoa katika nchi ya Misri, hatujui yaliyompata. Nikawaambia, Mtu yeyote aliye na dhahabu na aivunje; basi wakanipa, nami nikaitupa ndani ya moto, akatoka ndama huyu.
Basi asubuhi yake Musa akawaambia watu, Mmetenda dhambi kuu; na sasa nitakwenda juu kwa Bwana, labda nitafanya upatanisho kwa ajili ya dhambi yenu. Musa akarejea kwa Bwana akasema, Aa! Watu hawa wametenda dhambi kuu, wamejifanyia miungu ya dhahabu. Walakini sasa ikiwa utawasamehe dhambi yao – na kama sivyo, unifute, nakusihi, katika kitabu chako ulichokiandika. Bwana akamwambia Musa, Mtu yoyote aliyenitenda dhambi, ndiye nitakayemfuta katika kitabu changu. Basi sasa uende ukawaongoze watu hawa mpaka mahali pale ambapo nimekuambia habari zake; tazama, malaika wangu atakutangulia; pamoja na hayo siku nitakayowajilia nitawapatiliza kwa ajili ya dhambi yao.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 106:19-23 (K) 1
(K) Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema.
Walifanya ndama huko Horebu,
Wakaisujudia sanamu ya kuyeyuka.
Wakaubadili utukufu wao,
Kuwa mfano wa ng’ombe mla majani. (K)
Wakamsahau Mungu, mwokozi wao,
Aliyetenda makuu katika Misri.
Matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu,
Mambo ya kutisha penye bahari ya Shamu. (K)
Akasema ya kuwa atawaangamiza,
Kama Musa, mteule wake, asingalisimama,
Mbele zake kama mahali palipobomoka,
Ili aigeuze hasira yake asije akawaharibu. (K)
SHANGILIO
Efe. 1:17, 18
Aleluya, aleluya,
Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristu, awape roho ya hekima mjue tumaini la mwito wake.
Aleluya.
INJILI
Mt. 13:31 – 35
Yesu aliwatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na punje ya haradali, aliyoitwaa mtu akaipanda katika shamba lake; nayo ni ndogo kuliko mbegu zote; lakini ikiisha kumea, huwa kubwa kuliko mboga zote, ikawa mti, hata nyuni wa angani huja na kukaa katika matawi yake.
Akawaambia mfano mwingine; Ufalme wa mbinguni umefanana na chachu aliyoitwaa mwanamke, akaisitiri ndani ya pishi tatu za unga, hata ukachachwa wote pia.
Hayo yote Yesu aliwaambia makutano kwa mifano; wala pasipo mfano hakuwaambia neno; ili litimie neno lililonenwa na nabii, akisema, Nitafumbua kinywa changu kwa mifano, Nitayatamka yaliyositirika tangu awali.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Nguvu hutoka kwa Bwana
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Katika imani, yote yanawezekana
Tumaini ni nanga ya roho
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Mwamini katika mpango wake.
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Neema na amani iwe nawe.
Nakuombea 🙏
Endelea kuwa na imani!
Sifa kwa Bwana!
Rehema hushinda hukumu
Neema ya Mungu inatosha kwako
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Dumu katika Bwana.
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Mungu akubariki!
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Imani inaweza kusogeza milima
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Rehema zake hudumu milele
Mwamini Bwana; anajua njia
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Baraka kwako na familia yako.
Mungu ni mwema, wakati wote!
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha