SOMO 1
2 Wafalme:4.42
Alikuja mtu kutoka Baal-shalisha, akamletea mtu wa Mungu chakula cha malimbuko, mikate ishirini ya shayiri, na masuke mabichi ya ngano guniani. Akasema, Uwape watu, ili wale. Na mtumishi wake akasema, Je! Niwaandikie hiki watu mia? Lakini akasema, Uwape watu, ili wale; kwa kuwa Bwana asema hivi, Watakula na kusaza. Basi akawaandikia, nao wakala, wakasaza, sawasawa na neno la Bwana.
WIMBO WA KATIKATI
1. Ee Bwana, kazi zako zote zitakushukuru, Na wacha Mungu wako watakuhimidi. Wataunena utukufu wa ufalme wako, Na kuuhadithia uweza wako. (K)
Waufumbua mkono wako, wakishibisha kila kilicho hai matakwa yake.
2. Macho ya watu yakuelekea Wewe, Nawe huwapa chakula chao wakati wake. Waufumbua mkono wako, Wakishibisha kila kilicho hai matakwa yake. (K)
3. Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote, Na mwenye fadhili juu ya kazi zake zote. Bwana yu karibu na wote wamwitao, Wote wamwitao kwa uaminifu.
SOMO 2
Waefeso:4.1 – 6
Nawasihi, mimi niliye mfungwa katika Bwana, mwenende kama inavyoustahili wito wenu mlioitiwa; kwa unyenyekevu wote na upole, kwa uvumilivu, mkichukuliana katika upendo; na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani. Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu. Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja. Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote.
SHANGILIO
Yohana:14.6
Aleluya Aleluya!
Mimi ndimi njia, na ukweli, na uzima, asema Bwana; Mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi. Aleluya
INJILI
Yn. 6:1-15
Yesu alikwenda zake ng’ambo ya Bahari ya Galilaya, nayo ndiyo ya Tiberia. Na mkutano mkuu wakamfuata, kwa sababu waliziona ishara alizowafanyia wagonjwa. Naye Yesu akakwea mlimani, akaketi huko pamoja na wanafunzi wake. Na Pasaka, sikukuu ya Wayahudi, ilikuwa karibu. Basi Yesu alipoinua macho yake akaona mkutano mkuu wanakuja kwake, alimwambia Filipo, Tununue wapi mikate, ili hawa wapate kula? Na hilo alilinena ili kumjaribu; kwa maana alijua mwenyewe atakalotenda. Filipo akamjibu, Mikate ya dinari mia mbili haiwatoshi, kila mmoja apate kidogo tu. Wanafunzi wake mmojawapo, Andrea, nduguye Simoni Petro, akamwambia, Yupo hapa mtoto, yuna mikate mitano ya shayiri na samaki wawili, lakini hivi ni nini kwa watu wengi kama hawa? Yesu akasema, Waketisheni watu. Na mahali pale palikuwa na majani tele. Basi watu waume wakaketi, wapata elfu tano jumla yao. Basi Yesu akaitwaa ile mikate, akashukuru, akawagawia walioketi; na kadhalika katika wale samaki kwa kadiri walivyotaka. Nao waliposhiba, aliwaambia wanafunzi wake, Kusanyeni vipande vilivyobaki, kisipotee cho chote. Basi wakavikusanya, wakajaza vikapu kumi na viwili, vipande vya mikate mitano ya shayiri vilivyowabakia wale waliokula. Basi watu wale, walipoiona ishara aliyoifanya, walisema, Hakika huyu ni nabii yule ajaye ulimwenguni. Kisha Yesu, hali akitambua ya kuwa walitaka kuja kumshika ili wamfanye mfalme, akajitenga, akaenda tena mlimani yeye peke yake.
Neno la Bwana….. Sifa Kwako Ee Kristo.
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Imani inaweza kusogeza milima
Neema ya Mungu inatosha kwako
Baraka kwako na familia yako.
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Katika imani, yote yanawezekana
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Mungu akubariki!
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Mungu ni mwema, wakati wote!
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Sifa kwa Bwana!
Nguvu hutoka kwa Bwana
Endelea kuwa na imani!
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Nakuombea 🙏
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Mwamini katika mpango wake.
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Rehema zake hudumu milele
Dumu katika Bwana.
Mwamini Bwana; anajua njia
Tumaini ni nanga ya roho
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Rehema hushinda hukumu
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Neema na amani iwe nawe.
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake