SOMO 1
Kut. 24:3-8
Musa aliwambia watu maneno yote ya Bwana, na hukumu zake zote; watu wote wakajibu kwa sauti moja, wakasema, Maneno yote aliyoyanena Bwana tutayatenda. Basi Musa akayaandika maneno yote ya Bwana, akaondoka asubuhi na mapema, akajenga madhabahu chini ya mlima, na nguzo kumi na mbili, kwa hesabu ya kabila kumi na mbili za Israeli, akapeleka vijana wa wana wa Israeli, waliotoa sadaka za kuteketezwa, wakamchinjia Bwana sadaka za amani za ng’ombe. Musa akatwaa nusu ya ile damu, akaitia katika mabakuli; na nusu ya ile damu akainyunyiza juu ya madhabahu. Kisha akakitwaa kitabu cha agano akakisoma masikioni mwa watu; wakasema, Hayo yote aliyoyanena Bwana tutayatenda, nasi tutatii. Musa akaitwaa ile damu, akawanyunyizia watu, akasema, Hii ndiyo damu ya agano alilolifanya Bwana pamoja nanyi katika maneno haya yote.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 50:1-2, 5-6, 14-15 (K) 14 (K)
Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru. Mungu, Mungu Bwana, amenena, ameiita nchi, Toka maawio ya jua hata machweo yake. Tokea Sayuni,, ukamilifu wa uzuri, Mungu amemulika. (K)
Nikusanyieni wacha Mungu wangu, Waliofanya agano nami kwa dhabihu. Na mbingu zitatangaza haki yake, Kwa maana Mungu ndiye aliye hakimu. (K)
Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru; Mtimizie Aliye juu nadhiri zako. Ukaniite siku ya mateso; Nitakuokoa, na wewe utanitukuza. (K)
SHANGILIO
Zab. 8:15
Aleluya, aleluya,
Wanabarikiwa wale ambao kwa unyofu na wema wa mioyo yao, hulisikia neno la Mungu na kulishika.
Aleluya.
INJILI
Mt. 13:24 – 30
Yesu aliwatolea makutano mfano akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake; lakini watu walipolala akaja adui yake akapanda magugu katikati ya agano, akaenda zake. Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu. Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu? Akawaambia, Adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, Basi, wataka twende tukayakusanye? Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo. Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Neema na amani iwe nawe.
Endelea kuwa na imani!
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Mungu akubariki!
Mwamini katika mpango wake.
Rehema zake hudumu milele
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Katika imani, yote yanawezekana
Mungu ni mwema, wakati wote!
Nguvu hutoka kwa Bwana
Tumaini ni nanga ya roho
Baraka kwako na familia yako.
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Dumu katika Bwana.
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Mwamini Bwana; anajua njia
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Neema ya Mungu inatosha kwako
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Nakuombea 🙏
Imani inaweza kusogeza milima
Sifa kwa Bwana!
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Rehema hushinda hukumu
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia