SOMO 1
Yer. 7:23-28
Naliwaamuru neno hili, nikisema, Sikilizeni sauti yangu, nami nitakuwa Mungu wenu, nanyi mtakuwa watu wangu; mkaende katika njia ile yote nitakayowaamuru, mpate kufanikiwa. Lakini hawakusikiliza, wala kutega sikio lao, bali walikwenda kw amashauri yao wenyewe, na kwa ushupavu wa mioyo yao mibaya, wakaenda nyuma wala si mbele. Tokea siku ile baba zenu walipotoka katika nchi ya Misri hata leo, nimewatuma watumishi wangu wote manabii kwenu ninyi, nikiamka mapema kila siku na kuwatuma. Lakini hawakunisikiliza, wala kutega sikio lao; bali walifanya shingo yao kuwa ngumu; walitenda mabaya kuliko baba zao. Nawe utawaambia maneno hayo yote; lakini hawatakusikiliza; nawe utawaita; lakini hawatakuitikia. Nawe utawaambia, Taifa hili ndilo lisilosikiliza sauti ya Bwana, Mungu wao, wala kupokea mafundisho; uaminifu umepotea, umekatiliwa mbali vinywa vyao.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 95:1-2, 6-9 (K) 7
(K) Ingekuwa heri leo msikie sauti yake! Msifanye migumu mioyo yenu.
Njoni, tumwimbie Bwana,
Tumfanyie shangwe mwamba wa wokovu wetu.
Tuje mbele zake kwa shukrani,
Tumfanyie shangwe kwa zaburi. (K)
Njoni, tuabudu, tusujudu,
Tupige magoti mbele za Bwana aliyetuumba.
Kwa maana ndiye Mungu wetu,
Na sisi tu watu wa malisho yake,
Na kondoo za mkono wake. (K)
Ingekuwa heri leo msikie sauti yake!
Msifanye migumu mioyo yenu;
Kama vile huko Meriba,
Kama siku ya Masa jangwani.
Hapo waliponijaribu baba zenu,
Wakanipima, wakayaona matendo yangu. (K)
SHANGILIO
Zab. 51:10, 12
Ee Mungu, uniumbie moyo safi,
Unirudishie furaha ya wokovu wako.
INJILI
Lk. 11:14-23
Yesu alikuwa akitoa pepo bubu; ikawa pepo alipotoka, yule bubu akanena, makutano wakastaajabu. Wengine wao wakasema, Atoa pepo kwa Beelzebuli, mkuu wa pepo. Wengine walimjaribu, wakitaka ishara itokayo mbinguni. Naye akajua mawazo yao, akawaambia, Kila ufalme uliofitinika wenyewe kwa wenyewe hufanyika ukiwa; na nyumba juu ya nyumba huanguka. Basi, ikiwa Shetani naye amefitinika juu ya nafsi yake, ufalme wake utasimamaje? Kwa kuwa ninyi mnasema kwamba mimi natoa pepo kwa Beelzebuli, wana wenu je! Huwatoa kwa nani? Kwa sababu hiyo, hao ndio watakaowahukumu. Lakini, ikiwa mimi natoa pepo kwa kidole cha Mungu, basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajilia. Mtu mwenye nguvu aliyejifunga silaha zake, alindapo nyumba yake, vitu vyake vi salama; lakini mtu mwenye nguvu kuliko yeye atakapomwendea na kumshinda, amnyang’anya silaha zake zote alizokuwa akizitegemea, na kuyagawanya mateka yake.
Mtu ambaye si pamoja nami yu kinyume changu; na mtu asiyekusanya pamoja nami hutapanya.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Neema na amani iwe nawe.
Imani inaweza kusogeza milima
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Mungu ni mwema, wakati wote!
Baraka kwako na familia yako.
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Katika imani, yote yanawezekana
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Nguvu hutoka kwa Bwana
Sifa kwa Bwana!
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Tumaini ni nanga ya roho
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Rehema zake hudumu milele
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Neema ya Mungu inatosha kwako
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Mwamini Bwana; anajua njia
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Rehema hushinda hukumu
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mwamini katika mpango wake.
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Endelea kuwa na imani!
Nakuombea 🙏
Mungu akubariki!
Dumu katika Bwana.
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni