MASOMO YA MISA, MACHI 23, 2022: JUMATANO JUMA LA 3 LA KWARESI
SOMO 1 – Kumb. 4:1, 5-9
Musa aliwaambia makutano: Ee Israeli, zisikilizeni amri na hukumu niwafundishazo, ili mmzitende; mpate kuishi na kuingia na kuimiliki nchi awapayo Bwana, Mungu wa baba zenu.
Angalieni nimewafundisha amri na hukumu, vile vile kama Bwana, Mungu wangu, alivyoniamuru, ili mzitende katika nchi mwmingiayo ili kuimiliki. Zishikeni basi, mkazitende, maana hii ndiyo hekima yenu na akili zenu, machoni pa mataifa watakaozisikia amri hizi zote, nao watasema, Hakika taifa hili kubwa ni watu wenye hekima na akili. Kwa maana liko taifa gani kubwa, lililo na Mungu aliye karibu nao, kama Bwana, Mungu wetu, alivyo, kila tumwitapo? Tena liko taifa gani kubwa, lililo na amri na hukumu zenye haki kama torati hii yote, ninayoiweka mbele yenu leo.
Lakini, jihadhari nafsi yako, ukailinde roho yako kwa bidii, usije ukayasahau mambo yale uliyoyaona kwa macho yako, yakaondoka moyoni mwako siku zote za maisha yako; bali uwajulishe watoto wako na watoto wa watoto wako.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI – Zab. 147:12-13, 15-16, 19-20 (K) 12
(K) Msifu Bwana, Ee Yerusalemu.
Msifu Bwana, Ee Yerusalemu;
Msifu Mungu wako, Ee Sayuni.
Maana ameyakaza mapingo ya malango yako,
Amewabariki wanao ndani yako. (K)
Huipeleka amri yake juu ya nchi,
Neno lake lapiga mbio sana.
Ndiye atoaye theluji kama sufu,
Huimwaga barafu yake kama majivu. (K)
Humhubiri Yakobo neno lake,
Na Israeli amri zake na hukumu zake.
Hakulitendea taifa lolote mambo kama hayo,
Wala hukumu zake hawakuzijua. (K)
SHANGILIO
Mbegu neno la Mungu, mpanzi lakini ni Kristu; Yeyote ampataye, ataishi milele.
INJILI – Mt. 5:17-19
Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Msidhani kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza. Kwa maana, amin, nawaambia, Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya torati haitaondoka hata yote yatimie. Basi mtu yeyote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme mbinguni.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Nguvu hutoka kwa Bwana
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Mungu ni mwema, wakati wote!
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Imani inaweza kusogeza milima
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Endelea kuwa na imani!
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Baraka kwako na familia yako.
Neema ya Mungu inatosha kwako
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Mwamini Bwana; anajua njia
Rehema hushinda hukumu
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Katika imani, yote yanawezekana
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Dumu katika Bwana.
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Mungu akubariki!
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Nakuombea 🙏
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Neema na amani iwe nawe.
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Sifa kwa Bwana!
Tumaini ni nanga ya roho
Mwamini katika mpango wake.
Rehema zake hudumu milele
Tembea kwa imani, si kwa kuona