Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
☰
AckyShine

Angalia nilivyoingizwa mjini na ujanja wangu wote

Featured Image

Ndio nilikuwa nimeshuka kwenye basi la SAI BABA pale Ubungo, nina Begi kubwa Mgongoni na begi Dogo la Lap Top mkononi, sura inatazama Mbele Very Serious kama nipo kwenye Gwaride la Uhuru!..Mabega juu yanafanya Cheers na Mawingu!, natembea kwa madoido…..leo nimetoka Likizo Moshi,

"Brother Simu ya ukweli hii..kitu cha Tecno C9 bei poa" hii ilikuwa sauti ya Teja mmoja hivi!

Yaani huyu Teja Bwege kweli,anataka kumuuzia nani sabuni? mimi sio wa kuja!…kamwe Siwezi kuibiwa hapa Town,hakuna wizi au utapeli nisioujua!, Mimi nimezaliwa Mwananyamala kwa Manjunju, nikalelewa Tandale kwa Mtogole, Shule ya msingi nimesoma Turiani Magomeni, Hivi Mbwa gani aniibie?…kwa Style ipi?

Sipendi kabisa Upuuzi!, Wajinga ndio wataibiwa, sio Mimi!…sasa Kwa mwendo wa haraka nikatoka nje kabisa ya Stendi ya Ubungo straight mpaka Stendi ya dala dala za Kariakoo, hapo ndipo nikakutana na Vijana wawili wadogo wakiwa na mzani wa kupimia uzito,…hakika napenda sana vijana wanaojituma kama hawa na sio ile Mijizi ya kule ndani Stendi!!,….hapa sasa nikapata wazo!

"Dogo mnapima uzito kwa shilingi ngapi?''

"Mia mbili tu Kaka!"

''Ok"

Kwa mwendo wa kikakamavu nikapanda juu ya mzani,lengo hapa ni kujua uzito wangu, Mtori niliokula mwezi mzima kule kwa Mshekuu sio mchezo, hapa nahisi nacheza kwenye kg za John Cena,

"Mama wee! Dogo mzani mzima huu kweli? Mbona nina kilo 134?" (Nilihamaki)

"Aaah! Brother huoni umepanda na Mabegi juu ya mzani?'''

Hahaha! kweli nimechanganyikiwa!…Sasa nikatoa mabegi yote mawili na kurudi juu ya Mzani, hapa ndipo Uzito ukashuka kutoka kg 134 mpaka kg 56!…My God kweli Body la "One Pack " haliongopi! thats means mabegi yaliniongezea kg 78! duh hii ni hatari!

"Yaani we Dogo kitambi chote hiki kg 56? huu Mzani Mzima kweli?"

Kimya…

"Dogo huu Mzani vipi?"

Kimya…

Dogo ana dharau huyu!…Sasa ndio nikabandua macho yangu toka kwenye kioo cha mzani ili nimtazame huyu dogo asiyejibu!….ndipo macho yangu yakakutana na Kigoda tupu kilichochongwa Mvomero!…Dogo hakuwepo!….na Mabegi pia hayapo!…lap top haipo!….NIMEPIGWA!

Ni dhahiri watoto wa Mjini walikuwa wameniacha juu ya Mzani, wamechukua Lap top ya Milioni na wameniachia Mzani chakavu wa elfu 40, what a stress!….sasa nilirudisha macho kwenye kioo cha uzito na sasa kilisoma KG 38!…yaani dakika hii hii nimepungua kilo zingine 18, Hakiyamama nahisi hata utumbo wangu wamebeba!…niitieni Ambulance!

πŸ™†πŸΌπŸ™†πŸΌπŸ™†πŸΌπŸ™†πŸΌπŸ™†πŸΌπŸ™†πŸΌπŸ™†πŸΌπŸ™†πŸΌπŸ™†πŸΌπŸ™†πŸΌπŸ™†πŸΌ

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Nahida (Guest) on July 10, 2022

Hii ni kichekesho kali sana, ninashiriki na kila mtu! πŸ˜‚

Lucy Wangui (Guest) on June 25, 2022

πŸ˜‚πŸ‘πŸ˜…πŸ€£

Rashid (Guest) on May 16, 2022

Hii ni dhahabu ya vichekesho! πŸ˜„

Charles Mchome (Guest) on May 7, 2022

Asante Ackyshine

Agnes Lowassa (Guest) on May 2, 2022

Brilliant! Muda wake ulikuwa kamili! ⏰

Josephine Nekesa (Guest) on April 24, 2022

Hii ni joke ya maana sana! πŸ˜‚πŸ‘Œ

Peter Otieno (Guest) on March 29, 2022

Hizi jokes ni za ukweli! πŸ˜†πŸ‘

Richard Mulwa (Guest) on March 16, 2022

Kila siku napenda jokes zenu! πŸ˜†πŸ˜‚

Margaret Anyango (Guest) on March 16, 2022

Hii imenichekesha sana! πŸ˜„πŸ˜‚

Elijah Mutua (Guest) on March 10, 2022

Kweli mna kipaji cha ucheshi! πŸ‘πŸ€£

Samson Mahiga (Guest) on January 5, 2022

🀣πŸ”₯😊

Lydia Mzindakaya (Guest) on December 31, 2021

Hizi jokes zinabamba sana! πŸ˜†πŸ˜‚

Lydia Mahiga (Guest) on December 22, 2021

Hii ni joke ya kipekee sana! πŸ˜‚πŸ‘

George Mallya (Guest) on December 15, 2021

πŸ˜‚πŸ€£πŸ˜†πŸ˜…

Joy Wacera (Guest) on November 23, 2021

Ucheshi wenu unanifurahisha kila siku! πŸ˜ŠπŸ˜‚

Dorothy Mwakalindile (Guest) on October 17, 2021

Hii ni joke ya ukweli kabisa! πŸ˜‚πŸ€£

Nancy Kawawa (Guest) on July 24, 2021

Ucheshi wenu ni wa hali ya juu! πŸ‘πŸ€£

Paul Kamau (Guest) on July 23, 2021

Hii ni kali sana! πŸ˜‚πŸ€£

Joyce Aoko (Guest) on July 21, 2021

πŸ˜ŠπŸ˜‚πŸ˜…πŸ‘

Samuel Were (Guest) on July 20, 2021

Hii kichekesho imenifurahisha sanaβ€”imebamba! 🀣

Lydia Wanyama (Guest) on June 28, 2021

Bado nacheka, hiyo ilikuwa nzuri sana! 🀣

Faith Kariuki (Guest) on June 27, 2021

πŸ€£πŸ€£πŸ‘πŸ˜†

Agnes Njeri (Guest) on June 10, 2021

Hii imenibamba sana! πŸ˜…πŸ€£

Salum (Guest) on May 28, 2021

πŸ˜‚ Sijacheka hivi kwa muda mrefu sana!

Edwin Ndambuki (Guest) on May 27, 2021

πŸ˜„ Hii ni ubunifu wa hali ya juu!

Linda Karimi (Guest) on April 5, 2021

Hii imenifurahisha sana! 🀣😊

Simon Kiprono (Guest) on March 26, 2021

Hii ni aina ya kichekesho usichosahau! πŸ˜‚

Grace Njuguna (Guest) on March 17, 2021

πŸ€£πŸ˜„πŸ˜Š

John Kamande (Guest) on March 14, 2021

Hii ndio nilihitaji leo! Asante! 😜

Lydia Wanyama (Guest) on March 11, 2021

πŸ˜… Bado ninacheka!

Esther Nyambura (Guest) on February 17, 2021

Hii ni joke ya kipekee! πŸ€£πŸ‘Œ

Elizabeth Mrope (Guest) on February 13, 2021

πŸ˜‚πŸ€£πŸ˜‚πŸ˜…

Anna Mahiga (Guest) on February 10, 2021

Hii imenipa kicheko cha siku! πŸ˜‚πŸ˜†

Joseph Kiwanga (Guest) on January 20, 2021

Huyu alikuwa na point! πŸ˜‚πŸ‘Œ

Arifa (Guest) on January 17, 2021

Hii kichekesho imebadilisha kabisa hali yangu! πŸ˜ƒ

Jane Muthui (Guest) on January 10, 2021

Napenda jokes zenu! πŸ˜ŠπŸ˜…

Michael Mboya (Guest) on December 4, 2020

Nimecheka hadi nimesahau shida zangu! πŸ€£πŸ˜†

Lucy Kimotho (Guest) on December 3, 2020

Umetisha! πŸ‘ŒπŸ˜‚

Daudi (Guest) on November 26, 2020

πŸ˜„ Umenishika vizuri!

Patrick Kidata (Guest) on November 19, 2020

πŸ˜†πŸ˜‚πŸ˜Š

Mary Sokoine (Guest) on November 8, 2020

πŸ˜…πŸ˜ŠπŸ˜‚πŸ‘

Mwanais (Guest) on November 5, 2020

πŸ˜„ Kichekesho gani!

Sarafina (Guest) on October 30, 2020

πŸ˜… Nilihitaji kicheko hiki, asante!

Michael Mboya (Guest) on October 29, 2020

Huu ucheshi hauna kifani! 🀣πŸ”₯

Moses Kipkemboi (Guest) on October 25, 2020

Hii imenifurahisha sana! πŸ˜ŠπŸ˜…

Mwakisu (Guest) on October 13, 2020

🀣 Sikutarajia hiyo!

John Lissu (Guest) on September 12, 2020

Hii imenikuna sana! πŸ˜†πŸ˜…

John Mwangi (Guest) on July 9, 2020

Nimecheka hadi nimesahau shida! πŸ€£πŸ˜†

Peter Mugendi (Guest) on June 29, 2020

Nimeipenda hii joke! πŸ˜„πŸ˜‚

Alice Mwikali (Guest) on May 25, 2020

Lazima niihifadhi hii, ni kichekesho kali sana! πŸ˜†

John Mushi (Guest) on May 9, 2020

Kweli mnajua kuchekesha watu! πŸ€£πŸ˜‚

Michael Onyango (Guest) on May 2, 2020

πŸ˜† Ninaihifadhi kwa baadaye!

Anthony Kariuki (Guest) on April 28, 2020

πŸ˜„ Umeshinda mtandao leo!

Alice Mwikali (Guest) on April 20, 2020

Nimefurahia sana hii! πŸ˜…πŸ˜Š

Nancy Komba (Guest) on March 25, 2020

😁 Kicheko bora ya siku!

David Sokoine (Guest) on March 22, 2020

Nimecheka hadi machozi yanatoka! 🀣😭

Diana Mallya (Guest) on February 5, 2020

😁 Hii ni dhahabu!

Esther Nyambura (Guest) on February 2, 2020

Kweli mna ucheshi! πŸ˜‚πŸ€£

Sharifa (Guest) on January 4, 2020

πŸ˜… Nilihitaji kicheko hicho!

Rose Kiwanga (Guest) on December 19, 2019

Hii imenipa kicheko cha siku! πŸ˜‚πŸ€£

Related Posts

Mzee wa kichaga na hela zake. Angalia anachofanya

Mzee wa kichaga na hela zake. Angalia anachofanya

Mzee moja alikuwa kila usiku anapita mbele ya bank anasimama,kisha anapiga honi,akitoka askari ml... Read More

Angalia huyu jamaa anavyojiona msomi, huyu kamuotea, hapa amekwama

Angalia huyu jamaa anavyojiona msomi, huyu kamuotea, hapa amekwama

USIJIONE MJUAJI SAAAA…NA.
Jamaa kamaliza chuo anarudi nyumbani kwa wazee, kufika
nyum... Read More

Cheki huyu mzee alichomfanyia muuzaji wa pharmacy

Cheki huyu mzee alichomfanyia muuzaji wa pharmacy

Mzee kaingia pharmacy, MZEE: Mambo mwanangu, kuna kitu naomba uonje nitakulipa MFAMASIA: Kitu gani?β... Read More
Cheki tulichokifanya jana

Cheki tulichokifanya jana

JANA APA HOME

JENERETA LILIWASHWA

ACHA TUHANGAIKE KULIKUNA

πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚... Read More

Huyu jamaa kawaweza polisi watatu, cheki alichowaambia

Huyu jamaa kawaweza polisi watatu, cheki alichowaambia

Polisi::: hodi, hodi
Jamaa::: kimya
Polisi::: hodi, hodi
Jamaa::: ... Read More

Cheki huyu jamaa anavyoungama kwa padri sasa

Cheki huyu jamaa anavyoungama kwa padri sasa

JAMAA: Baba Padri nimekuja kuungama
PADRI: Haya
JAMAA: Niliiba kamba
PADRI: Kamba?... Read More

Hii ndiyo maana ya matatizo

Hii ndiyo maana ya matatizo

SWALI: Nini maana ya matatizo..?

JIBU: matatizo ni pale unapopewa adhabu na mwanajeshi t... Read More

Ukata wa January

Ukata wa January

Boss;-Β kwa nini umechelewa kazini
Juma;-Β kuna mtu njiani alidondo... Read More

Angalia nilichomjibu huyu kuhusu kabila langu

Angalia nilichomjibu huyu kuhusu kabila langu

Kuna mtu kanikeraΒ et nmemkubalia urafiki Leo tuΒ Faceb... Read More

Kilichotokea baada ya kuzamia sherehe

Kilichotokea baada ya kuzamia sherehe

Pale unapozamia kwenye Dinner Party ya Jumuiya Fulani, sasa Lengo la Jumuiya hiyo ni kupata Fedha... Read More

Vichekesho vya kukuondoa mawazo leo

Vichekesho vya kukuondoa mawazo leo

Soma vichekesho hivi;

Mwizi wa atm

Jamaa aliibiwa kadi yake ya benk akaulizwa kama ... Read More

Sitasahau mwaka huu

Sitasahau mwaka huu

Sitasahau mwaka ule ambapo nilipeleka barua ya maombi yangu ya kazi kwenye kampuni moja ... Read More