Kulikuwa na vijana wawili walioamua kwenda kwa padri kumwelezea shida zao.
Basi walipofika kwa yule padre, wakamwambia padre, ” samahani padre tuko hapa mbele yako kwa kuwa tumejisikia kuwa ni wadhambi ha hivyo tunahitaji kuungama.
Basi wakwanza akamwambia padre, ” Mimi dhambi zangu ni kubwa sana hata ninaona aibu kuziungama”, wa pili akamwambia padre, ” sahamani padre mimi nimetenda dhambi ila siyo kubwa sana kama za mwenzangu, bali ni dhambi ndogondogo.” Baada ya kusikia hayo padre aliwaambia basi kila mmoja aende akaokote mawe kadiri ya dhambi alizozitenda na akamletee. Hao vijana walienda kuokota mawe kadiri ya dhambi za kila mmoja wao. Mmoja wao alileta jiwe moja kubwa ambalo alikuja akilivilingisha hadi pale alipokuwepo padre, na mwingine alileta mawe madogomadogo mengi kwenye mfuko. Baada ya padre kuone kuwa walifanya alivyowaagiza, basi aliwaambia kuwa kila mmoja arudishe mawe yake sehemu ile ile alipoyaokota. Yule aliyebeba jiwe kubwa ilikuwa rahisi kujua alipolitoa hivyo alilivilingisha mara moja na kulirudisha mahali pake, wakati yule aliyekuwa na mawe madogomadogo alishindwa kukumbuka mahali alipoyatoa, hivyo akaishia kuhangaika na kumwambia padre kuwa hawezi kumbuka mahali alipotoa kila jiwe, na kwake ni vigumu.
Baada ya hayo padre aliwaambia wote kuwa yule mwenye dhambi kubwa daima ni rahisi kuiungama maana huwa inashika nafasi kubwa katika nafsi yake na inamfanya asiwe na amani daima, kwa hivyo ni rahisi kukumbuka kuiungama dhambi yake, vilevile padre akamgeukia yule mwingine aliyebeba mfuko wa mawe madogomadogo na akamwambia kuwa, jinsi ulivyoshindwa kurudisha hayo mawe katika nafasi yake kila moja, ndivyo ilivyo kwa dhambi ndogondogo ulizotenda. Dhambi zionekanazo kuwa ni ndogo zaweza sahulika na kukufanya utende dhambi nyingine ya kutokukumbuka wajibu wako wa kuungama ukidhani kuwa hujatenda dhambi.
Daima tunakumbushwa kuungama dhambi zetu hata kama ni ndogo au hata kama tumesahau, kwa maana kuna zile dhambi ambazo ni nyepesi na rahisi kusahulika na hivyo kutufanya daima tujihisi kuwa sisi hatuna haja ya kuungama.
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Mwamini Bwana; anajua njia
Neema na amani iwe nawe.
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Nakuombea 🙏
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Rehema hushinda hukumu
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Neema ya Mungu inatosha kwako
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Mungu akubariki!
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Sifa kwa Bwana!
Rehema zake hudumu milele
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Tumaini ni nanga ya roho
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Baraka kwako na familia yako.
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Mungu ni mwema, wakati wote!
Mwamini katika mpango wake.
Imani inaweza kusogeza milima
Dumu katika Bwana.
Endelea kuwa na imani!
Nguvu hutoka kwa Bwana
Katika imani, yote yanawezekana
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe