VIPIMO
Mchele – 3 Vikombe
Mchicha
Mafuta – 1/2 kikombe
Vitunguu maji – 2 vikubwa
Nyanya – 1
Viazi – 3
Kitunguu saumu(thomu/galic) iliyosagwa – 3 vijiko vya supu
Vidonge vya supu (Stock cubes) – 3
Jiyrah (cummin powder) – 1 kijiko cha chai
Pilipili manga ya unga – 1 kijiko cha chai
Hiliki ya unga – 1/2 kijiko cha chai
Mdalasini – 1 kijiti
Maji (inategemea mchele) – 5 vikombe
Chumvi
NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA
1. Osha na roweka mchele.
2. Osha mchicha, chuja maji na katakata.
3. Katakata vitunguu maji, nyanya.
4. Menya na kata viazi vipande ukaange pekee vitoe weka kando.
5. Katika sufuria tia mafuta na kaanga vitunguu hadi viwe rangi ya hudhurungi.
6. Tia thomu, bizari zote, kaanga kidogo kisha nyanya.
7. Tia mchicha kaanga kidogo kisha tia mchele, maji na vidonge vya supu, chumvi.
8. Koroga kidogo kisha tia viazi ulivyovikaanga, funika na acha uchemke kidogo katika moto mdogo mdogo.
9. Kabla ya kukauka maji, mimina katika chombo cha kupikia ndani ya oven (oven proof) au katika treya za foil, funika vizuri na upike ndani ya oven moto wa 400ΒΊ kwa dakika 15-20 upikike hadi uive.
10. Ukishaiva epua na tayari kuliwa na kitoweo chochote upendacho.
Editor: Melkisedeck Leon Shine. About Me | Contact Me | LinkedIn | TikTok | WhatsApp
Read and Write Comments
Recommended Posts
Mapishi ya samaki aina ya salmon
Mapishi ya Biriani la nyama ya ng’ombe
Jinsi ya kupika Slesi Za Chokoleti Na Karameli
Jinsi ya kupika Biskuti Za Njugu/Matunda Makavu (Rock Cakes)
Mapishi ya Haliym Ya Nyama Mbuzi -Bokoboko La Pakistan
Nguvu ya Nafaka Zote: Chaguzi za Upishi Zenye Afya
Jinsi ya kupika Viazi Vya Nazi Kwa Nyama
LISHE BORA KWA WATU WENYE AFYA NZURI