Katika amri ya tatu ya Mungu tumeamriwa nini?
Tumeamriwa kuheshimu siku ya Mungu:-
1. Kushiriki Misa Takatifu siku ya Jumapili na Sikukuu zote za Amri
2. Kuacha kazi nzito na
3. Kutenda matendo mema
Siku ya Mungu kwa Mkristo ni lini?
Siku ya Mungu kwa Mkristo ni siku ya Dominika, ndio siku aliyofufuka Bwana na huitwa pia Siku ya Bwana
Nani analazima kuhudhuria Misa Takatifu, Dominika na Sikukuu zilizoamriwa?
Kila Mkatoliki aliyetimiza umri wa Miaka saba na kuendelea ana lazima kuhudhuria Misa Takatifu, Dominika na Sikukuu zilizoamriwa.
Katika amri ya tatu ya Mungu tumekatazwa nini?
Katika Amri ya tatu ya Mungu tumekatazwa kufanya kazi nzito siku ya Dominika/Jumapili.
Kazi nzito zilizokatazwa kufanyika siku ya Bwana ni zipi?
Kazi nzito ni zile za kuchosha mwili na zisizo za lazima kama vile kulima, kujenga, kubeba mizigo mizito, biashara n.k.
Je ni dhambi kukosa Misa Jumapili?
NDIYO. Ni dhambi kubwa kukosa Misa kwa Makusudi siku ya Jumapili/Dominika na Sikukuu zilizoamriwa.
Nani atenda dhambi dhidi ya Amri ya tatu ya Mungu?
Anayetenda dhambi dhidi ya amri ya tatu ya Mungu ni yule:-
1. Asiyeshiriki Misa Takatifu Dominika na sikukuu zilizoamriwa kwa uvivu au uzembe
2. Anayefanya kazi ngumu Dominika na sikukuu zilizoamriwa
3. Anayechelewa sehemu kuu ya Misa Takatifu
4. Anayekaa nje ya kanisa bila sababu wakati wa Misa Takatifu na Ibada. (Neh 13:15-22, Kut 20:8-11)
Anayevunja Amri ya Tatu ya Mungu yampasa nini?
Yampasa atubu na aungame kabla ya kushiriki Sakramenti nyingine
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Mungu akubariki!
Dumu katika Bwana.
Neema ya Mungu inatosha kwako
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Nakuombea 🙏
Imani inaweza kusogeza milima
Tumaini ni nanga ya roho
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Nguvu hutoka kwa Bwana
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Baraka kwako na familia yako.
Mungu ni mwema, wakati wote!
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Rehema hushinda hukumu
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Neema na amani iwe nawe.
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Mwamini Bwana; anajua njia
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Sifa kwa Bwana!
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Katika imani, yote yanawezekana
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Rehema zake hudumu milele
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Mwamini katika mpango wake.
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Endelea kuwa na imani!