Kwanza Mungu aliumba nini?
Kwanza Mungu aliumba Malaika (Kol 1:16)
Malaika ni viumbe gani?
Malaika ni viumbe vya Mungu vilivyo roho tu wenye akili na utashi. (Zab 91:11, Ebr 1:7, Ufu 12:7-9)
Mungu aliumba Malaika katika hali gani?
Mungu aliumba Malaika katika hali njema na heri kubwa.
Malaika wote walidumu katika hali njema na ya heri?
Siyo, Malaika wengine walikosa kwa kumkaidi Mungu, Wakatupwa Motoni.
Ndio Mashetani ambao Mkubwa wao ni Lusiferi. (Yoh 8:44, Uf 12:7-9)
Kwa nini Mungu ameumba Malaika?
Mungu ameumba Malaika ili wamtukuze, wafurahi naye Mbinguni, na wawe matarishi wake kwa wanadamu. (Tob 12:12, Lk 16:22)
Malaika wema kazi yao ni nini?
Malaika wema kazi yao ni kutuombea, kutumwa na Mungu kwetu, na wanatulinda kama Malaika wetu Walinzi. (Ebr 13:2)
Kila Mwanadamu anaye Malaika wake wa kumlinda?
Ndiyo, Kila Mwanadamu anaye Malaika wake wa kumlinda ndiye Malaika Mlinzi. (Mt. 18:10)
Malaika Walinzi wanatutendea nini?
Malaika walinzi hutupenda, hutuongoza, na kutulinda roho na mwilini (Zab 90:11)
Je Malaika wote ni sawa?
Hapana. Malaika wote sio sawa, maana kuna;
1. Malaika wakuu
2. Malaika wanaomtumikia Mungu Mbinguni yaani Makerubi na Maserafi
3. Malaika Walinzi
2. Malaika wanaomtumikia Mungu Mbinguni yaani Makerubi na Maserafi
3. Malaika Walinzi
Malaika wakuu wako watatu ambao ni?
Malaika wakuu wako watatu: Mikaeli, Raphaeli na Gabrieli (Dn 10:13, Tobiti 12:15, Lk 1:26)
Makao ya shetani ni wapi na anatamani nini?
1. Mashetani kazi yao ni kuteswa Motoni
2. Hutaka kutudhuru roho na mwili na kutupoteza milele (1 Petro 5:8, Yoh 8:44)
2. Hutaka kutudhuru roho na mwili na kutupoteza milele (1 Petro 5:8, Yoh 8:44)
Kisha kuumba Malaika Mungu aliumba nini?
Kisha kuumba Malaika Mungu aliumba Mbingu na dunia, na viumbe vingine vingi vyenye kuonekana mimea na watu. (Mwanzo 1;31)
Viumbe vyenye hiari ni vipi?
Malaika na watu ndio viumbe pekee vyenye hiari ya kuchagua wenyewe wachangie mpango wa Mungu au la.
“Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi, chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako; kumpenda Bwana, Mungu wako, kuitii sauti yake, na kushikamana naye; kwani hiyo ndiyo uzima wako” (Kumb 30:19-20).
Malaika na watu wanaweza kuchagua hata nini?
Malaika na watu wanaweza kuchagua hata wawe wema au wabaya milele.
“Kulikuwa na vita mbinguni: Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni” (Ufu 12:7-8).
Chaguo letu binadamu linafanyika siku kwa siku kwa kuchukua misimamo mizuri au mipotovu kuhusu dini na maadili.
“Mwayachunguza Maandiko, kwa sababu mnadhani kwamba ninyi mna uzima wa milele ndani yake; na hayo ndiyo yanayonishuhudia. Wala hamtaki kuja kwangu mpate kuwa na uzima” (Yoh 5:39-40).
Malaika wakoje?
Malaika ni roho tupu walioumbwa na Mungu ili wamtukuze milele, wamlinde kila mtu na kumtumikia Bwana Yesu katika kutuokoa.
“Angalieni, msidharau mmojawapo wadogo hawa, kwa maana nawaambia ya kwamba malaika zao mbinguni sikuzote huutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni” (Math 18:10).
Je, toka mwanzo sisi watu tunaasi mpango wa Mungu peke yetu?
Hapana, toka mwanzo sisi watu tunaasi mpango wa Mungu kwa kuvutwa na mashetani, yaani malaika waliokataa moja kwa moja kumtumikia; baada ya dhambi ya asili hao wanatutumia sisi pia tuangushane na wenzetu.
Lakini Mungu aliwahi kumuambia Shetani:
“Nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako, na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino” (Mwa 3:15).
“Hata ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke” (Gal 4:4).
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Rehema hushinda hukumu
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Dumu katika Bwana.
Nakuombea 🙏
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Katika imani, yote yanawezekana
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Endelea kuwa na imani!
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Neema na amani iwe nawe.
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Mungu akubariki!
Rehema zake hudumu milele
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Neema ya Mungu inatosha kwako
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Nguvu hutoka kwa Bwana
Tumaini ni nanga ya roho
Mungu ni mwema, wakati wote!
Imani inaweza kusogeza milima
Mwamini Bwana; anajua njia
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Mwamini katika mpango wake.
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Baraka kwako na familia yako.
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Sifa kwa Bwana!
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia