Je, tunaweza kuhakikisha neema ya utakaso?
Hapana, hatuwezi kuhakikisha neema ya utakaso kwa kuwa ni tukio ambalo linapita maumbile na kufanyika rohoni, hivyo halifikiwi na hisi zetu. Pengine Mungu anatokeza dalili fulani za badiliko hilo kama vile furaha ya ndani au karama ya nje, lakini hizo hazihitajiki wala hazitoshi kuthibitishia mtu amepata neema hiyo.
“Wengi wataniambia siku ile: Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri: Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu” (Math 7:22-23).
“Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao. Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi. Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu” (1Kor 13:1-3).
Neema ni nini?
Neema ni kipaji cha roho kinachopita nguvu za viumbe vyote; ndicho kipaji tupewacho na Roho Mtakatifu ili tupate uzima wa milele. (Lk 1:30, Rum 5:2)
Kuna aina ngapi za neema?
Kuna aina mbili za neema
1. Neema ya utakaso
2. Neema ya msaada
2. Neema ya msaada
Neema ya Utakaso ni nini?
Neema ya Utakaso ni uzima wa Kimungu unaomiminwa na Roho Mtakatifu mioyoni mwetu. (Yoh 1:16, Yoh 3:3-5)
Neema ya Utakaso yapatikanaje?
Neema ya Utakaso yapatikana kwa;
1. Kwanza kwa Sakramenti ya Ubatizo
2. Sakramenti ya Kitubio
3. Kwa majuto kamili (majuto ya mapendo)
1. Kwanza kwa Sakramenti ya Ubatizo
2. Sakramenti ya Kitubio
3. Kwa majuto kamili (majuto ya mapendo)
4. Yaongezwa kwa kupokea Sakramenti nyingine
5. Kwa Sala
6. Kwa Ibada Takatifu
7. Kwa matendo mema
5. Kwa Sala
6. Kwa Ibada Takatifu
7. Kwa matendo mema
Neema ya Utakaso yapoteaje?
Neema ya Utakaso yapotea kwa kutenda dhambi kubwa (dhambi ya mauti)
Kuna Faida ya kuwa na Neema ya Utakaso?
Faida ya kuwa na Neema ya Utakaso ni;-
1. Kupendwa na Mungu hapa duniani
2. Na kupokelewa kwake mbinguni baada ya kufa
2. Na kupokelewa kwake mbinguni baada ya kufa
Neema ya Msaada ni nini?
Neema ya Msaada ni msaada tupatao kwa Roho Mtakatifu kutuongezea nguvu Rohoni tutende mambo mema na tuepuke Mabaya
Neema ya Msaada yapatikanaje?
Neema ya Msaada yapatikana kwa kupokea Sakramenti, kusali, na kutenda mambo ya Ibada (Yoh 15:5, 1Tim 2:4)
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Mwamini katika mpango wake.
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Nakuombea 🙏
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Neema ya Mungu inatosha kwako
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Neema na amani iwe nawe.
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Mungu ni mwema, wakati wote!
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Rehema hushinda hukumu
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Baraka kwako na familia yako.
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Rehema zake hudumu milele
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Mwamini Bwana; anajua njia
Nguvu hutoka kwa Bwana
Mungu akubariki!
Sifa kwa Bwana!
Endelea kuwa na imani!
Imani inaweza kusogeza milima
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Katika imani, yote yanawezekana
Dumu katika Bwana.
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Tumaini ni nanga ya roho