SOMO 1
Mdo 20 : 28-38
Paulo aliwaambia wakuu wa kanisa ya Efeso: Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe. Najua mimi ya kuwa baada ya kuondoka kwangu mbwamwitu wakali wataingia kwenu, wasilihurumie kundi; tena katika ninyi wenyewe watainuka watu, wakisema mapotovu, wawavute hao wanafunzi wawaandamie wao. Kwa hiyo kesheni, mkikumbuka ya kwamba miaka mitatu, usiku na mchana, sikuacha kumwonya kila mtu kwa machozi. Basi, sasa nawaweka katika mikono ya Mungu, na kwa neno la neema yake, ambalo laweza kuwajenga na kuwapa urithi pamoja nao wote waliotakaswa. Sikutamani fedha wala dhahabu, wala mavazi ya mtu. Ninyi wenyewe mnajua ya kuwa mikono yangu hii imetumika kwa mahitaji yangu na ya wale waliokuwa pamoja nami. Katika mambo yote nimewaonyesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge, na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu, jinsi alivyosema mwenyewe, Ni heri kutoa kuliko kupokea. Alipokwisha kunena haya akapiga magoti, akaomba pamoja nao wote. Wakalia sana wote, wakamwangukia Paulo shingoni, wakambusu-busu, wakihuzunika zaidi kwa sababu ya neno lile alilosema, ya kwamba hawatamwona uso tena. Wakamsindikiza hata merikebuni.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 68:28-29, 32-35 (K) 32
(K) Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu.
Au: Aleluya.
Ee Mungu, uziamuru nguvu zako;
Ee Mungu, uwe hodari uliyetufanyia makuu.
Kwa ajili ya hekalu lako Yerusalemu
Wafalme watakuletea hedaya. (K)
Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu,
Msifuni Bwana kwa nyimbo.
Apandaye mbingu za mbingu za tangu milele;
Aitoa sauti yake, sauti ya nguvu.
Mhesabieni Mungu nguvu; (K)
Enzi yake i juu ya Israeli;
Na nguvu zake zi mawinguni.
Mungu ni mwenye kutisha Kutoka patakatifu pako.
Ndiye Mungu wa Israeli;
Yeye huwapa watu wake nguvu na uwezo.
Na ahimidiwe Mungu. (K)
SHANGILIO
Yn. 14 : 26
Aleluya, aleluya,
Roho Mtakatifu atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.
Aleluya.
INJILI
Yn. 17:11-19
Siku ile, Yesu alisali akisema: Baba mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo. Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie.
Na sasa naja kwako; na maneno haya nayasema ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu imetimizwa ndani yao. Mimi nimewapa neno lako; na ulimwengu umewachukia; kwa kuwa wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu.
Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu. Wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu. Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli. Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami vivyo hivyo naliwatuma hao ulimwenguni. Na kwa ajili yao najiweka wakfu mwenyewe, ili na hao watakaswe katika kweli.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristu.
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Mungu akubariki!
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Baraka kwako na familia yako.
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Katika imani, yote yanawezekana
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Tumaini ni nanga ya roho
Imani inaweza kusogeza milima
Nguvu hutoka kwa Bwana
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Nakuombea 🙏
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Endelea kuwa na imani!
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Rehema zake hudumu milele
Sifa kwa Bwana!
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Mwamini Bwana; anajua njia
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Neema ya Mungu inatosha kwako
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Rehema hushinda hukumu
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Mwamini katika mpango wake.
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Dumu katika Bwana.
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Neema na amani iwe nawe.
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Mungu ni mwema, wakati wote!