MASOMO YA MISA, MACHI 25, 2022
IJUMAA, JUMA LA 3 LA KWARESIMA
SHEREHE YA KUPASHWA HABARI YA KUZALIWA BWANA
SOMO 1
Isa. 7:10 – 14
Bwana alisema na Ahazi akinena, Jitakie ishara ya Bwana, Mungu wako; itake katika mahali palipo chini sana, au katika mahali palipo juu sana. Lakini Ahazi akasema, Sitaitaka, wala sitamjaribu Bwana. Naye akasema, Sikilizeni sana, enyi nyumba ya Daudi; Je! Ni neno dogo kwenu kuwachosha wanadamu, hata mkataka kumchosha Mungu wangu pia? Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, Bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 40:6 – 10 (K) 7 , 8
(K) Tazama, nimekuja, Ee Bwana, kuyafanya mapenzi yako.
Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo,
Masikio yangu umeyazibua,
Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka.
Ndipo niliposema, Tazama nimekuja. (K)
Katika gombo la chuo nimeandikiwa
Kuyafanya mapenzi yako,
Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu;
Naam, sheria yako imo moyoni mwangu. (K)
Nimehubiri habari za haki katika kusanyiko kubwa,
Sikuizuia midomo yangu; Ee Bwana, unajua. (K)
Sikusitiri haki yako moyoni mwangu;
Nimetangaza uaminifu wako na wokovu wako.
Sikuficha fadhili zako wala kweli yako
Katika kusanyiko kubwa. (K)
SOMO 2
Ebr. 10:4 – 10
Haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi. Kwa hiyo ajapo ulimwenguni, asema, Dhabihu na toleo hukutaka, Lakini mwili uliniwekea tayari; Sadaka za kuteketezwa na sadaka za dhambi hukupendezwa nazo; Ndipo niliposema, Tazama nimekuja (katika gombo la chuo nimeandikiwa) niyafanye mapenzi yako, Mungu.
Hapo juu asemapo, Dhabihu na matoleo na sadaka za kuteketezwa na hizo za dhambi hukuzitaka, wala hukupendezwa nazo (zitolewazo kama ilivyoamuru torati), ndipo aliposema, Tazama, nimekuja niyafanye mapenzi yako. Aondoa la kwanza, ili kusudi alisimamishe la pili. Katika mapenzi hayo tumepata utakaso, kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu.
Neno la Bwana…
Tumshukuru Mungu.
SHANGILIO
Yn. 1:14
Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu, nasi tukaona utukufu wake.
INJILI
Mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti, kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu, jina lake Yusufu, wa mbari ya Daudi; na jina lake bikira huyo ni Mariamu. Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema. Bwana yu pamoja nawe. Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani? Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu. Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye ju, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake. Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho. Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume? Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu. Tena, tazama, jamaa yako Elisabeti naye amechukua mimba ya mtoto mwanamume katika uzee wake; na mwezi huu ni wa sita kwake yeye aliyeitwa tasa; kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu. Mariamu akasema, Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema. Kisha malaika akaondoka akaenda zake.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Katika imani, yote yanawezekana
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Imani inaweza kusogeza milima
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Endelea kuwa na imani!
Mwamini Bwana; anajua njia
Nakuombea 🙏
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Baraka kwako na familia yako.
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Mungu ni mwema, wakati wote!
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Neema ya Mungu inatosha kwako
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Dumu katika Bwana.
Tumaini ni nanga ya roho
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Neema na amani iwe nawe.
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Rehema hushinda hukumu
Mwamini katika mpango wake.
Mungu akubariki!
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Sifa kwa Bwana!
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Nguvu hutoka kwa Bwana
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Rehema zake hudumu milele