SHEREHE YA MT. YOSEFU, MUME WA BIKIRA MARIA
SOMO 1
2Sam. 7: 4 – 5, 12 – 14, 16
Ikawa usiku uo huo, neno la Bwana likamfikia Nathani kusema, Enenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, Bwana asema hivi, siku zako zitakapo timia, ukalala na Baba zako, nitainua mzao wako nyuma yako, atakayetoka viunoni mwako, nami nitaufanya imara ufalme wake.
Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa jina langu, nacho kiti cha enzi cha ufalme wake nitakifanya imara milele. Mimi nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu, akitenda maovu nitamwadhibu kwa fimbo yako, na ufalme wako, vitathibitishwa milele mbele yako. Nacho kiti chako kitafanywa imara milele.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 89:1 – 4, 26, 28 (K) 36(K)
Wazao wake watadumu milele.
Fadhili za Bwana nitaziimba milele;Kwa kinywa changu nitavijulisha vizazi vyote uaminifu wako.
Maana nimesema, Fadhili zitajengwa milele;Katika mbingu utauthibitisha uaminifu wako. (K)
Nimefanya agano na mteule wangu,Nimemwapia Daudi, mtumishi wangu.Wazao wako nitawafanya imara milele,Nitakijenga kiti chako cha enzi hata milele. (K)
Yeye ataniita, Wewe baba yangu,Mungu wangu na mwamba wa wokovu wangu.
Hata milele nitamwekea fadhili zangu,Na agano langu litafanyika amini kwake. (K)
SOMO 2
Rum. 4:13, 16 – 18, 22
Ahadi ile ya kwamba atakuwa mrithi wa ulimwengu alipewa Ibrahimu na uzao wake, si kwa sheria bali kwa haki aliyohesabiwa kwa Imani. Kwa hiyo ilitoka katika Imani, iwe njia ya neema, ili kwamba ile ahadi iwe imara kwa wazao wote; si kwa wale wa torati tu, ila kwa wale wa Imani ya Ibrahimu; aliye baba yetu sisi sote; (kama ilivyoandikwa, Nimekuweka kuwa baba wa mataifa mengi); mbele zake yeye aliyemwamini, yaani Mungu, mwenye kuwahuisha wafu, ayatajaye yale yasiyokuwako kana kwamba yamekuwako.Naye aliamini kwa kutarajia yasiyoweza kutarajiwa, ilia pate kuwa baba wa mataifa mengi, kama ilivyonenwa, Ndivyo utakavyokuwa uzao wako. Kwa hiyo ilihesabiwa kwake kuwa ni haki.Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
SHANGILIO
Zab. 84:5
Heri wakaao nyumbani mwako, Ee Bwana.
Nakuombea 🙏
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Sifa kwa Bwana!
Endelea kuwa na imani!
Mungu akubariki!
Dumu katika Bwana.
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Mwamini katika mpango wake.
Baraka kwako na familia yako.
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Neema na amani iwe nawe.
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Rehema zake hudumu milele
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Neema ya Mungu inatosha kwako
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Nguvu hutoka kwa Bwana
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Rehema hushinda hukumu
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Mwamini Bwana; anajua njia
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Katika imani, yote yanawezekana
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Imani inaweza kusogeza milima
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Tumaini ni nanga ya roho
Mungu ni mwema, wakati wote!