SOMO 1
Yer. 17:5-10
Bwana asema hivi: Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake, na moyoni mwake amemwacha Bwana. Maana atakuwa kama fukara nyikani, hataona yatakapotokea mema; bali atakaa jangwani palipo na ukame, katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.
Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, ambaye Bwana ni tumaini lake. Maana atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji, uenezao mizizi yake karibu na mto; hautaona hofu wakati wa hari ujapo, bali jani lake litakuwa bichi; wala hautahangaika mwaka wa uchache wa mvua, wala hautaacha kuzaa matunda.
Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua? Mimi, Bwana, nauchunguza moyo, navijaribu viuno, hata kumpa kila mtu kiasi cha njia zake, kiasi cha matunda ya matendo yake.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 1:1-4, 6 (K) 40:4
(K) Heri aliyemfanya Bwana kuwa tumaini lake.
Heri mtu yule asiyekwenda
Katika shauri la wasio haki;
Wala hakusimama katika njia ya wakosaji;
Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.
Bali sheria ya Bwana ndiyo impendezayo,
Na sheria yake huitafakari mchana na usiku. (K)
Naye atakuwa kama mti uliopandwa
Kandokando ya vijito vya maji,
Uzaao matunda yake kwa majira yake,
Wala jani lake halinyauki;
Na kila alitendalo litafanikiwa. (K)
Sivyo walivyo wasio haki;
Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
Kw akuwa Bwana anaijua njia ya wenye haki,
Bali njia ya wasio haki itapotea. (K)
SHANGILIO
Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako.
INJILI
Lk. 16:19-31
Yesu aliwaambia Mafarisayo: Palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula sikuzote kwa anasa. Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, huwekwa mlangoni pake, ana vidonda vingi, naye alikuwa akitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka katika meza ya yule tajiri; hata mbwa wakaja wakamramba vidonda vyake. Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa.
Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake. Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu. Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa. Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu.
Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu, kwa kuwaninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao piawakafika mahali hapa pa mateso. Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao. Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea atokaye kwa wafu, watatubu. Akamwambia wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishwa hata mtu akifufuka katika wafu.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Baraka kwako na familia yako.
Mwamini Bwana; anajua njia
Nguvu hutoka kwa Bwana
Mungu akubariki!
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Neema na amani iwe nawe.
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Katika imani, yote yanawezekana
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Rehema zake hudumu milele
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Rehema hushinda hukumu
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Sifa kwa Bwana!
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Endelea kuwa na imani!
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Imani inaweza kusogeza milima
Tumaini ni nanga ya roho
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Mungu ni mwema, wakati wote!
Mwamini katika mpango wake.
Neema ya Mungu inatosha kwako
Dumu katika Bwana.
Nakuombea 🙏