Updated at: 2024-05-27 07:11:27 (1 year ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Sala ni Hazina. Kusali ni muhimu sana. Sala unayosali leo inaweza kukusaidia hata miaka kumi ijayo au ikasaidia watoto wa watoto wako. Mungu ni mwenye fadhila na anakumbuka yote. Mwombe Mungu akulinde ukiwa mzima ili uwapo hatarini akukumbuke hata kabla hujamwomba.
Updated at: 2024-05-27 07:11:40 (1 year ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Mungu ni mwenye Hekima, anajibu Sala zetu kwa kutupa kile tunachohitaji na chenye kutufaa na Sio kutupa kile tunachokitaka na kukitamani kwa kuwa anatupenda na kututakia mema.
Updated at: 2024-05-27 07:11:45 (1 year ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Kama yalivyo maisha ya kimwili, maisha ya kiroho pia yanahitaji mipango. Kila siku panga utafanya nini kiroho, mfano unaweza kupanga sala, kusaidia masikini, kuwa mpole au mwema. Vivyo hivyo kila wiki, kila mwezi na kila mwaka mpya panga cha kufanya kiroho naye Mungu atakubariki na kukupangia zaidi. Huwezi kufanikiwa kiroho kama hujui unafanya nini kiroho.
Updated at: 2024-05-27 07:12:09 (1 year ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Mungu ni mwenye Huruma na Upendo na Anataka watu wote waokolewe naye. Mungu hayupo kwa ajili ya kukuhukumu bali kwa ajili ya kukuhurumia na kukurehemu.
Updated at: 2024-05-27 07:11:55 (1 year ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Hakuna sala yeyote itolewayo kwa unyenyekevu wa kweli katika imani, matumaini na mapendo inayopita bure mbele ya Mungu. Mungu hamtupi mwenye unyoofu wa moyo.
Updated at: 2024-05-27 07:11:34 (1 year ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Kufanya Mambo mema ndipo kunaleta furaha ya kweli kwa Binadamu yeyote yule. Hakuna Binadamu anayefurahia kufanya maovu. Mema hayaambatani na majuto lakini uovu wowote unamajuto. Hata waovu wanafanyiana mema ili wapate furaha.
Mungu ni zaidi ya Mzazi na upendo wake ni zaidi ya wa Wazazi
Updated at: 2024-05-27 07:11:51 (1 year ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Wakati wazazi waliweza kuaamua kuzaa mtoto tuu, Mungu yeye alikuchagua wewe utungwe mimba na kukulinda ungali tumboni mwa mama yako….Wakati wazazi wanasubiri kwa shauku kuona muonekano wako wewe, Mungu anawaweka wajukuu wa wazazi wako/ watoto wako ndani mwako…. Wakati wazazi wakitafuta chakula kwa ajili yako, Mungu yeye aliwawezesha kukipata…. Wakati wazazi wakingoja kuona unavyoendelea kukua huku wakiwaza hatima ya maisha yako Mungu anakuendeleza na alishapanga maisha yako tangu alipokuchagua uwe mtu ukiwa tumboni mwa mama yako…. Wazazi wanaweza kukuombea kwa Mungu lakini Mungu ndiye anayeamua akufanyie nini maana Wewe ni wa kwake….Wewe na wazazi wako ni watoto wa Baba mmoja ambaye ndiye Mungu.