Author name: SW - Melkisedeck Shine

Utani wa wahindi, cheka kidogo

Mhindi afaulu mtihani wa Kiswahili

(1) Mfa maji ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆ.. Tampa life jacket.
(2) Mwenda pole?โ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆ Tachelewa fika.
(3) Usipoziba ufa ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆ.. Mizi taona mpaka dani.
(4) Usilolijua ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆ Uliza google.
(5) Mbio za utelezini ?โ€ฆโ€ฆ. Chafua guo yako.
(6) Ukipenda boga ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆ Ngoja mezi ya ramzani tapata.
(7) Ukiona vinaelea ?โ€ฆโ€ฆ.. iko nyepesi hiyo.
(8) Maji yakimwagika ?โ€ฆโ€ฆ Mambie dada tapiga deki.
(9) Chelewa chelewa ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆ Takosa guo ya sikukuuโ€ฆ
(10) Kila ndege ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆ.. โ€ฆHutua Airport
(11) Bandu bandu ?โ€ฆ.. โ€ฆโ€ฆ.Rafiki yake Jecha
(12) Mtaka cha Mvunguni ?โ€ฆ Ondoa tanda
(13) Simba mwenda kimya?โ€ฆ.Kama sio gonjwa basi haina njaa.
(14) Aisifuye mvua ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆ. Najua iko Mkulima hiyo
(15) Barabara ndefu ?โ€ฆโ€ฆ.. Ongeza mwendo au tachelewa fika.
(16) Mlanawe hafi nawe ila?โ€ฆ. Takimbia
(17) Asie sikia la mkuu ? โ€ฆโ€ฆ.. Tapeleka jela
(18) Hasira za mkizi ? โ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆ..Tatafuna veve
(19) Mchamba wima ?โ€ฆโ€ฆ.. Karibu ya Hurumzi
(20) Akumurikae mchana ?โ€ฆ.Kipofu hiyo
(21) Mficha maradhi ?โ€ฆโ€ฆ.. Taenda Loliondo
(22) Mkataa wingi ? โ€ฆโ€ฆโ€ฆ.Taenda Chadema
(23) Bendera ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆ. Kama sio ya CCM, ya CUF
(24) Baniani mbaya ?โ€ฆโ€ฆ. Peleka Bombay Lakini sio HB kweli, naonea tu
(25) Akili nyingi ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆ. Tapasi mtihani yote
(26) Penye kuku wengi ? โ€ฆโ€ฆ.. Chija bili tatu ivi, hapana mtu najua.

Cheka kidogo, angalia anachosema huyu mchaga

Mchaga baada ya kufa akaulizwa na malaika anayetoa roho: Mangi hapa ni njiapanda kulia ni Mbinguni na kushoto ni Jehanamu, Je unachagua kwenda wapi?

MANGI: Bwashee, mi nabaki hapa hapa njiapanda aisee.
MALAIKA: Kwa nini?
MANGI: Aisee, nikifungua duka hapa si nitapata wateja wa Mbinguni na Jehanam. Yani patakuwa senta ya hatari, supu na nyama choma muda wote. Hata we utafaidi, unavyoenda kuchukua roho unaniletea stock nakupa hela yako cash mkononi. Na kila ukipita hapa unapiga mchemsho wako wa ulimi na bia mbili chap kabla ya kuingia mbinguni.
Kwanza nashangaa Shirima alipitaje hapa bila kushika ploti, au alikufa amelewa sana?

Safari ni safari

FUNDISHO : SAFARI NI SAFARI

Maisha ni ya ajabu sana, wakati mwingine maisha ni mazuri na mwingine ni mabaya, katika maisha yetu tumeshapitia safari nyingi sana na za aina mbalimbali kwa nyakati mbalimbali. Lakin kiukweli kila safari ni safari tuu.

Japokua kila safari ina changamoto zake lakini mwisho wake ni ule ule , kila safari ina uzuri na upekee wake.

Vile vile kila safari ina ubaya wake, kwa mfano kila safari ina gharama yake kulingana na upekee wake.

Usiwe na wasiwasi na mashaka na aina ya safari ulionayo, jipe moyo utaimaliza na kupata ulichokitarajia. Haya ndio maisha na wote tunatakiwa tuyafurahie.

Ingawa kila mtu ana safari yake bado wote tunatakiwa tufurahie pamoja kwa safari tuliyo nayo. Hata Uwe Na safar ya aina gani wewe furahi tuu. Hii ni kwa sababu safari mwisho wake ni mmoja kwa wote burudani ni ile ile

Safari๐Ÿบ ni safari ๐Ÿบhata kama ni ya chupa au ya kopo mwisho wake ๐Ÿ’ค๐Ÿ’ค

๐Ÿ˜‹๐Ÿ˜œ๐Ÿ˜œ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚
Ulijua ni nn??

Ndege ya Tanzania

Kuna maprofesa 40 walipanda AIR TANZANIA ili wasafari. Kabla ndege haijaanza kuondoka, Lilipita tangazo kama ifuatavyo:

Ndugu wasafiri wote, ndege unayotarajia kusafiri nayo imetengenezwa na wanafunzi wa Kitanzania.
Baada ya tangazo maprofesa wote waliteremka isipokuwa mmoja alibaki kwenye kiti chake
Walipomuuliza ni kwanini hakuondoka akajibu kwa haraka na furaha kuwa:
Kama ndege hii imetengenezwa na watanzania, hata kuwaka haitawaka!

Shopping Cart