Wakati wa ujauzito ni kipindi cha kubadili mambo mengi katika mfumo wa maisha wa mjamzito. Mjamzito anapaswa kubadili mambo mbalimbali ili kuhakikisha anakua na afya nzuri katika kipindi chote cha ujauzito na ili kuhakikisha kwamba atajifungua mtoto mwenye afya nzuri. Moja ya mambo makubwa ni pamoja na tabia ya kuvaa viatu vyenye visigino virefu. Mjamzito hashauriwi kuvaa viatu vyenye visigino virefu kutokana na athari zinazoweza kutokana na aina hizi za viatu.
Zifuatazo ni athari za kuvaa viatu vyenye visigino virefu wakati wa ujauzito:
Mimba kutoka.
Mjamzito akivaa viatu vyenye visigino virefu anakua katika hatari kubwa ya kuanguka. Hii huweza kusababisha majeraha makubwa kwa mtoto aliyeko tumboni hali inayoweza kusababisha mimba kutoka.
Maumivu ya misuli ya mapaja.
Wadada hupenda kuvaa “high heels” husababisha misuli ya mapaja kukaza na kuwa na muonekano mzuri. Katika ujauzito, mabadiliko ya homoni huweza kupelekea misuli hii kuwa na maumivu tofauti na ilivyokua kabla ya ujauzito.
Hatari ya kuanguka.
Ni wazi kuwa uzito huongezeka wakati wa ujauzito na mabadiliko ya vichocheo vya mwili huweza kupelekea kizunguzungu cha hapa na pale. Hii huongeza hatari ya kuanguka iwapo utavaa “high heels” na kupelekea majeraha kwako na kwa mtoto aliyeko tumboni.
Uvimbe miguuni.
Ni jambo la kawaida miguu kuvimba wakati wa ujauzito. Kuvaa viatu vyenye visigino virefu na vyenye kubana huweza kuongeza tatizo hilo na kupelekea maumivu.
Maumivu ya mgongo.
Wakati wa ujauzito, uzito mkubwa huhamia mbele na misuli ya nyonga hulegea. Mabadiliko haya ya kimsawazo huweza kusababisha maumivu ya sehemu ya chini ya mgongo na kiuno.
Mambo ya Kuzingatia kama ni lazima kuvaa
Iwapo kuna ulazima sana wa kuvaa viatu hivyo, unapaswa kuzingatia yafuatayo:
- Epuka visigino vyembamba sana.
- Usivae siku nzima. Vitoe mara kwa mara kupumzisha miguu.
- Epuka kutembea au kusimama muda mrefu ukiwa umevivaa.
- Ukihisi maumivu kwenye misuli ya mapaja jaribu kufanya mazoezi ya kujinyoosha na kujikanda.
- Ni salama kuvaa viatu hivi katika muhula wa kwanza wa ujauzito (Miezi mitatu ya mwanzo).
- Viatu visiwe virefu sana na visigino viwe imara.
- Vaa viatu visivyo na bugdha na usivikaze sana.
Editor: Melkisedeck Leon Shine. About Me | Contact Me | LinkedIn | TikTok | WhatsApp
Read and Write Comments
Recommended Posts
Jinsi ya kutibu chunusi kwa kutumia maganda ya ndizi
Umuhimu wa kufanya Masaji
Sababu na madhara ya tatizo la kukosa choo
Soma hii Kabla hujafikiria kula nyama ya nguruwe tena
Ulaji mzuri hupunguza uwezekano wa kupata shinikizo la chini la damu
Madhara ya kutumia dawa za kuzuia mimba wakati wa hatari
Mambo ya msingi kujua kuhusu ugonjwa wa ngiri
Aina ya vyakula vinavyotakiwa kwa wajawazito