Unafahamu nini kuhusu suala la kumlaza mwanao? Maana Mapokeo tuliyo yapokea enzi na enzi ni kuwa ukitaka mtoto wako alale bila kushtuka basi alalie tumbo. Bado watu wengi wanaendelea kufanya hivyo hata sasa hivi unaposoma makala haya.
Je madaktari wanasemaje kuhusu suala hili?
Sayansi inashauri kuwa ni hatari kumlaza mtoto kwa tumbo. Visa kadhaa vya watoto kupoteza maisha vimehusishwa na watoto kulalia tumbo.
Kuanzia mwaka 1992 Madaktari wa watoto nchini Marekani walipendekeza kuwa watoto wachanga walale chali ( walalie Mgongo) ili kuepuka vifo vya ghafla vya watoto. Kifo cha ghafla hutokea pale ambapo mtoto mchanga anakutwa amefariki akiwa usingizini.
Tangu pendekezo hilo la madaktari idadi ya vifo vya ghafla vya watoto imepungua zaidi ya nusu ya vifo vyote vya watoto vinavyotokea wakiwa usingizini.
Ni vizuri kuhakikisha kuwa kila mtu anayekusaidia kulea mtoto anajua jinsi ya kumlaza mtoto chali.
Muhimu
Hata hivyo kuna baadhi ya watoto unaweza kushauriwa na daktari iwapo mwanao usimlaze chali na alalie tumbo.
Editor: Melkisedeck Leon Shine. About Me | Contact Me | LinkedIn | TikTok | WhatsApp
Read and Write Comments
Recommended Posts
Jinsi ya kutibu chunusi za usoni kwa kutumia Parachichi na asali
Visababishi, dalili, matibabu na kinga ya presha ya kushuka
Lifahamu tatizo la maumivu chini ya kitovu
Mambo ya msingi kufahamu kuhusu uotaji wa meno kwa mtoto
Matumizi ya Lozi na maziwa kutibu shinikizo la chini la damu
Faida ya kunywa maji yenye limao au ndimu kila siku
Jinsi ya kutibu chunusi kwa kutumia maganda ya ndizi
Chanzo, dalili, aina na matibabu ya ugonjwa wa kifafa