Upungufu wa damu ni tatizo linalosababishwa na kupoteza damu nyingi, kupungua kwa uzalishaji wa chembe hai za da damu na uharibifu wa chembe za damu kutokana na matatizo na magonjwa mbali mbali seli mundu, ujauzito, hedhi nzito, kurithi, magonjwa sugu na Lishe duni yenye ukosefu wa madini ya folic, chuma na vitamini B12.
Dalili
Dalili zifuatazo zinakuwezesha kutambua kama una tatizo la upungufu wa damu hivyo kukusaidia kuwahi hospitali au kubadili mfumo wa chakula ili kuepuka madhara makubwa ya baadae.
ยท Kushindwa kupumua vizuri
ยท Vidonda kwenye ulimi au mdomoni
ยท Sehemu nyeupe ya jicho kuwa bluu
ยท Ngozi kuwa na rangi ya kijivu
ยท Kucha kuwa dhaifu
ยท Kusikia hasira na kuhamasika haraka
ยท Kuchoka sana kuliko kawaida
ยท Maumivu makali ya kichwa
ยท Kupungua kwa uwezo wa kufikiria
ยท Kusikia kichwa chepesi pale unaposimama
ยท Miguu na mikono kuwa ya baridi sana
ยท Uchovu wa mara kwa mara
Matibabu.
Upungufu wa damu hutibiwa mapema kwa kubadili lishe pamoja na kuongeza lishe yenye vitamini C na B12 pamoja na madini ya Chuma kutokana na visababishi vya tatizo. Mara nyingine vidonge na sindano zenye lishe hizi huweza kutumika hosipitali na matibabu ya tatizo linalosababisha na iwapo mgonjwa yuko katika hali mahututi huweza kuongezewa damu.
References:
Google ScholarResearchGate
Semantic Scholar
AckySHINE