Muumbaji wa penseli alipomaliza kuiumba penseli yake aliiambia mambo muhimu ya kuzingatia ili iweze kuwa penseli bora kabla hajaituma kuingia kazini kwa matumizi.
“Kuna vitu sita unatakiwa uvitambue, “ Aliiambia penseli,
“Kabla sijakutuma kwenda kutumika, unatakiwa uviweke akilini vitu hivyo na usivisahau kamwe. Vitakusaidia siku zote na utakuwa penseli bora maisha yako yote.”
Alisema muumbaji wa penseli.
“Moja,” alianza kuvitaja,”utakuwa na uwezo wa kufanya vitu vingi, lakini kama utakubali na utaruhusu kuongozwa na mkono wa mtumiaji wako”
“Mbili” aliendelea kutoa nasaha, “utapata maumivu makali kutokana na kuchongwa mara kwa mara. Lakini vumilia kwani itakusaidia kuwa penseli bora na kuandika vizuri.”
“Tatu, utakuwa na uwezo wa kusahihisha makosa utakayo yafanya.”
“Nne, kitu pekee cha muhimu katika maisha yako ni kile kilicho ndani yako kwa sababu ndicho chenye uwezo wa kuandika.”
“Tano” alisisitiza mtengenezaji penseli, “kwenye kila sehemu utakayotumika, utaacha alama yako. Hata ikiwa ni kwenye sehemu ngumu au mbaya kiasi gani, ni lazima alama yako ibaki.
“Na sita”, alimalizia muumbaji yule wa penseli, “ipo siku utaisha na kupotea. Hivyo usiwe na hofu wala woga wala hudhuni uikaribiapo siku hiyo na ukaogopa kutimiza wajibu wako kwa kuhofia kuisha. Ukiogopa kuisha hautotumika na umuhimu wako hautonekana kwani hautatimiza wajibu uliombiwa kuufanya”
Penseli ilielewa na kuahidi kukumbuka na ikaingia sokoni ikiwa na dhamira yake moyoni.
Sasa tutumie mfano huo wa penseli katika maisha yetu halisi. Ukivikumbuka vitu hivyo sita ilivyopewa penseli, utaweza kuwa mtu bora kabisa kwenye maisha yako yote.
Moja, una uwezo wa kufanya mambo mengi na makubwa, kama utajiweka kwenye mikono ya Mungu.
Mbili, utakutana na magumu mengi ya kuumiza, lakini hayo ndiyo yatakufanya uwe mtu imara na bora, usiyakimbie.
Tatu, una uwezo wa kurekebisha makosa yote uliyoyafanya. Usijilaumu.
Nne, sehemu yako ya muhimu ni ile iliyo ndani yako kwani ndiyo inayoandika maisha yako. Ilinde.
Tano, kila sehemu utakayopita, acha alama yako kwa kufanya mazuri yatakayokufanya ukumbukwe daima, bila kujali mazingira. Timiza wajibu wako kwa kiwango cha juu.
Sita, tambua kuwa ipo siku utakufa. Usiwe na hofu yoyote juu ya kifo kwani ukiogopa kifo hutafanya lolote hapa duniani.
Tumia mfano huu wa penseli upate ujasiri wa kutambua kuwa wewe ni mtu muhimu hapa duniani na umeumbwa kwa madhumuni maalumu na umepewa uwezo mkubwa sana na Muumba wako! Ni wewe pekee mwenye uwezo wa kutimiza dhamira uliyotumwa na Muumba.
UBARIKIWE SANA.
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Rehema hushinda hukumu
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Nakuombea 🙏
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Mwamini Bwana; anajua njia
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Endelea kuwa na imani!
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Mungu ni mwema, wakati wote!
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Mwamini katika mpango wake.
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Dumu katika Bwana.
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Baraka kwako na familia yako.
Neema na amani iwe nawe.
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Katika imani, yote yanawezekana
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Sifa kwa Bwana!
Rehema zake hudumu milele
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Mungu akubariki!
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Neema ya Mungu inatosha kwako
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Nguvu hutoka kwa Bwana
Tumaini ni nanga ya roho
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Imani inaweza kusogeza milima
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima