SOMO 1
Yer. 20 : 10-13
Nimesikia mashutumu ya watu wengi; hofu ziko pande zote. Rafiki zangu wote wanaonivizia nisite, husema, Mshitaki, nasi tutamshitaki; huenda akahahadaika; nasi tutamshinda, tutajilipiza kisasi kwake. Lakini Bwana yu pamoja nami, mfano wa shujaa mwenye kutisha; kwa hiyo hao wanaonionea watajikwaa, wala hawatashinda; watatahayarika sana. Kwa sababu hawakutenda kwa akili, wataona aibu ya milele, ambayo haitasahauliwa kamwe. Lakini Ee Bwana wa majeshi, wewe wawajaribu wenye haki, waona viuno na mioyo. nijalie kuona kisasi chako juu yao; kwa maana nimekufunulia wewe neno langu.
Mwimbieni Bwana; msifuni Bwana;
Kwa maana ameiponya roho ya mhitaji
Katika mikono ya watu watendao maovu.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 69 : 7-9, 13,16, 32-34 (K) 13
(K) Kwa wingi wa fadhili zako unijibu.
Kwa ajili yako nimestahimili laumu,
Fedheha imenifunika uso wangu.
Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu,
Na msikwao kwa wana wa mama yangu.
Maana wivu wa nyumba yako umenila,
Na laumu yao wanaokulaumu zimenipata. (K)
Nami maombi yangu nakuomba Wewe, Bwana,
Wakati ukupendezao; Ee Mungu,
Kwa wingi wa fadhili zako unijibu,
Katika kweli ya wokovu wako.
Ee Bwana, unijibu, maana fadhili zako ni njema,
Kwa kadiri ya rehema zako unielekee. (K)
Walioonewa watakapoona watafurahi;
Enyi mmtafutao Mungu, mioyo yetu ihuishwe.
Kwa kuwa Bwana huwasikia wahitaji,
Wala hawadharau wafunga wake.
Mbingu na nchi zimsifu
Bahari na vyote viendavyo ndani yake. (K)
SOMO 2
Rum. 5:12-15
Kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia uli mwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi; maana kabla ya sheria dhambi ilikuwamo ulimwenguni, lakini dhambi haihesabiwi isipokuwapo sheria; walakini mauti ilitawala tangu Adamu mpaka Musa, nayo iliwatawala hata wao wasiofanya dhambi ifananayo na kosa la Adamu, alive mfano wake yeye atakayekuja. Lakini karama ile haikuwa kama lile kosa; kwa maana ikiwa kwa kukosa kwake yule mmoja wengi walikufa, zaidi sana neema ya Mungu, na kipawa kilicho katika neema yake mwanadamu mmoja Yesu Kristo kimezidi kwa ajili ya wale wengi.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
SHANG1LIO
Mdo. 16:14
Aleluya, aleluya,
Fungua mioyo yetu, ee Bwana,
Ili tuyatunze maneno ya Mwanao.
Aleluya.
INJILI
Mt. 10:26-33
Yesu aliwaambia mitume wake: Msiwaogope, kwa maana hakuna neno lililositirika, ambalo halitafunuliwa; wala lililofichwa, ambalo halitajulikana. Niwaambialo ninyi katika giza, lisemeni katika nuru; na msikialo kwa siri, lihubirini juu ya nyumba. Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum, Je! mashomoro wawili hawauzwi kwa senti moja? Wala hata mmoja haanguki chini asipojua Baba yenu; lakini ninyi, hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope basi; bora nyinyi kuliko mashomoro wengi. Basi, kila mtu atakayenikiri mbele ya watu, nami nitamkiri mbele za Baba yangu aliye mbinguni. Bali mtu ye yote atakayenikana mbele ya watu, nami nitamkana mbele za Baba yangu aliye mbinguni.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Rehema hushinda hukumu
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Endelea kuwa na imani!
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Tumaini ni nanga ya roho
Sifa kwa Bwana!
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Neema na amani iwe nawe.
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Baraka kwako na familia yako.
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Katika imani, yote yanawezekana
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Nguvu hutoka kwa Bwana
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Mwamini Bwana; anajua njia
Neema ya Mungu inatosha kwako
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Nakuombea 🙏
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Mwamini katika mpango wake.
Mungu akubariki!
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Rehema zake hudumu milele
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Imani inaweza kusogeza milima
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Dumu katika Bwana.
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Mungu ni mwema, wakati wote!