Uzinzi na uasherati wakati huu umekuwa ndio sumaku kuu ya kuwanasa watu ili waende jehanamu.
Sumaki hii imewanasa hata ambao hawakutegemewa wala kutarajiwa.
Uzinzi uzinzi uzinzi umekuwa kama perfume ya kujipulizia kila Mara mtu akipenda.
Uasherati umekuwa kama heshima ya kibinadamu kwa vijana wengi.
Mbingu zimenyamaza kwa sababu iko jehanamu inawangoja wazinzi na waasherati.
Dhambi hii imekuwa sumaku kubwa ya shetani ya kukamata wanadamu ili waende jehanamu.
Wanadamu wa Leo ukimwambia kwamba aache uzinifu maana wazinzi na waasherati hawataenda uzima wa milele, mtu huyo anakuambia unamhukumu.
Ni Neno la MUNGU ndile limesema katika maandiko mengi tu kwamba wazinzi na waasherati sehemu yako itakuwa katika ziwa la moto.
Hata makanisani baadhi ya watu wamenasa kwenye sumaku hii.
Dada mmoja ambaye kila wiki anasimama na kushika mic kanisani kwao siku moja aliniambia kwamba hawezi kumaliza wiki bila kufanya ngono, na hajaolewa. Niliumia sana rohoni nikamwambia aache kutumika madhabahuni, yeye akasema itakuaje maana yeye ndiye tegemeo.
Mama mmoja alisema yeye ana mume mema sana na mume wake ni mwaminifu sana katika ndoa yao lakini yeye huyo mama ndio hutoka nje ya ndoa Mara kwa Mara, ni hatari inayohitaji neema ya MUNGU tu ili kutubu na kuacha.
Mama mmoja yeye ana watoto zaidi ya wawili na yuko katika ndoa lakini hana uhakika kama watoto wale ni wa mume wake wa ndoa, ni hatari sana.
Baba mmoja akiwa ndani ya ndoa amezaa watoto zaidi ya watatu nje ya ndoa tena wanawake zaidi ya wanne(4) tofauti tofauti.
Mwanaume moja ambaye husimama madhabahuni yeye kila Mara humdanganya mkewe kwamba anaenda safari kumbe ana mahawara karibia kila mkoa, ni hatari sana.
Watu wengi sasa wanaona uzinzi na uasherati ndio fashion nzuri ya wakati kuu.
Kila kijana ana girlfriend kwa lengo la ngono tu na sio vinginevyo.
Kila binti ana boyfriend kwa ajili ya uasherati.
Ukitaka watu wakuchukie basi kemea uzinzi na uasherati.
Watu wengi wamekuwa vipofu wa kiroho kwa sababu ya uzinzi na uasherati.
Lakini upo mwisho mmoja kwa watenda dhambi wote ambayo ni jehanamu.
Ndugu unahitaji kutubu Leo na kuacha dhambi.
Ndugu mmoja akasema yeye anaishi maisha matakatifu ila dhambi moja tu yaani uzinifu ndio imemshinda, hiyo ni hatari.
Leo hata ndoa takatifu zimeadimika maana wahusika huanza kwanza uzinzi na uasherati ndio baadae ndoa, ndugu mnahitaji kutubu.
Ndugu yangu unayenisikiliza kwa njia ya ujumbe huu nakuomba tubu na acha dhambi hiyo.
Amua kuiacha.
Mwisho wa uzinzi na uasherati ni kifo(Mauti) na baada ya kifo ni hukumu(Waebrania 10:27)
Nimekuonya wewe Leo ili ukishupasa shingo usije ukalaumu siku ile ukiwa katikati ya bahari ya moto huku kifo kimezuiliwa ili uteseke milele.
Mimi naamini utatengeneza ndugu baada ya kuusoma ujumbe huu.
Mimi naamini utaachana na mahawara na kuanza kuiheshimu ndoa yako.
Mimi naamini hutamsaliti tena mkeo/Mumeo.
Mimi naamini utaachana na huyo girlfriend/Boyfriend, wengine wanao zaidi ya mmoja, nakuomba ndugu achana nao.
Kijana au binti kaa tulia hadi wakati wako wa ndoa.
Uliyenisikia na utatubu na kuacha dhambi hiyo, MUNGU akubariki sana.“`
ALIYE NA AKILI AWEKE MOYONI MANENO HAYA. AMINA
Mungu akubariki!
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Tumaini ni nanga ya roho
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Imani inaweza kusogeza milima
Mwamini Bwana; anajua njia
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Neema ya Mungu inatosha kwako
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Nguvu hutoka kwa Bwana
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Sifa kwa Bwana!
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Nakuombea 🙏
Dumu katika Bwana.
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Mungu ni mwema, wakati wote!
Endelea kuwa na imani!
Neema na amani iwe nawe.
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Rehema zake hudumu milele
Mwamini katika mpango wake.
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Rehema hushinda hukumu
Baraka kwako na familia yako.
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Katika imani, yote yanawezekana
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi