MWANZO:
Asifiwe Mungu Baba na Mwana na Roho Mtakatifu; kwasababu ametufanyizia huruma yake.
SOMO 1
Kut. 34 : 4-6, 8-9
Musa aliinuka na mapema asubuhi, naye akakwea katika mlima wa Sinai, kama Bwana alivyomwamuru, akazichukua hizo mbao mbili za mawe mkononi mwake.
Bwana akashuka ndani ya lile wingu, akasimama pamoja naye huko, akalitangaza jina la Bwana. Bwana akapita mbele yake, akatangaza, Bwana, Bwana, Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli; Musa akafanya haraka, akainamisha kichwa chake hata nchi, akasujudu. Akasema, Ikiwa sasa nimepata neema mbele zako, Bwana, nakuomba, Bwana, uende kati yetu maana ni watu wenye shingo ngumu; ukasamehe uovu wetu na dhambi yetu, ukatutwae tuwe urithi wako.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu
WIMBO WA KATIKATI
Dan. 3:52-56. (K) 52
(K) Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele.
Umehimidiwa, Ee Bwana, Mungu wa baba zetu:
Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele.
Limehimidiwa jina lako takatifu, tukufu;
Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele. (K)
Umehimidiwa katika hekalu la fahari yako takatifu;
Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele.
Umehimidiwa juu ya kiti cha ufalme wako;
Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele. (K)
Umehimidiwa utazamaye vilindi, uketiye juu ya makerubi;
Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele.
Umehimidiwa katika anga la mbinguni
Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele. (K)
SOMO 2
2 Kor. 13 :11-14
Hatimaye, ndugu, kwaherini; mtimilike, mfariji- ke, nieni mamoja, mkae katika amani; na Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi. Sali- mianeni kwa busu takatifu. Watakatifu wote wawasalimu. Neema ya Bwana Yesu Kristo, na pendo la Mungu. na ushirika wa Roho Mtakatifu ukae nanyi nyote.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
SHANG1LIO
Ufu. 1 :8
Aleluya, Aleluya,
Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu, Mungu ambaye yupo, aliyekuwako, na atakayekuja.
Aleluya.
INJILI
Yn. 3:16-18
Yesu alimwambia Nikodemu: Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhu- kumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye. Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Mungu akubariki!
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Neema na amani iwe nawe.
Nakuombea 🙏
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Sifa kwa Bwana!
Nguvu hutoka kwa Bwana
Mwamini Bwana; anajua njia
Rehema hushinda hukumu
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Endelea kuwa na imani!
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Baraka kwako na familia yako.
Dumu katika Bwana.
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Tumaini ni nanga ya roho
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Mungu ni mwema, wakati wote!
Rehema zake hudumu milele
Mwamini katika mpango wake.
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Katika imani, yote yanawezekana
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Imani inaweza kusogeza milima
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Neema ya Mungu inatosha kwako
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Tembea kwa imani, si kwa kuona