SOMO 1
Isa. 49:8-15
Bwana asema hivi, Wakati uliokubalika nimekujibu, na siku ya wokovu nimekusaidia; nami nitakuhifadhi, nitakutoa uwe agano la watu hawa, ili kuiinua nchi hii, na kuwarithisha urithi uliokuwa ukiwa; kuwaambia waliofungwa, Haya, tokeni; na hao walio katika giza, Jionyesheni.
Watajilisha katika njia, na juu ya majabali watapata malisho. Hawataona njaa, wala hawataona kiu; hari haitawapiga, wala jua; kwa maana yeye aliyewarehemu atawatangulia, naam, karibu na chemchemi za maji atawaongoza. Nami nitafanya milima yangu yote kuwa njia, na njia kuu zangu zitatukuzwa zote.
Tazama, hawa watakuja kutoka mbali; na tazama, hawa kutoka kaskazini, na kutoka magharibi, na hawa kutoka nchi ya sinimu. Imbeni, enyi mbingu; ufurahi, Ee nchi; pazeni sauti ya kuimba, enyi milima; kwa kuwa Bwana amewafariji watu wake, naye atawahurumia watu wake walioteswa.
Bali Sayuni alisema, Yehova ameniacha, Bwana amenisahau. Je! Mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye, hata asimhurumie mwana wa tumbo lake? Naam, hawa waweza kusahau, lakini mimi sitakusahau wewe.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 145:8-9, 13-14, 17-18 (K)
(K) Bwana ana fadhili, ni mwingi wa huruma.
Bwana ana fadhili, ni mwingi wa huruma,
Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema.
Bwana ni mwema kwa watu wote,
Na rehema zake zi juu ya kazi zake zote. (K)
Ufalme wako ni ufalme wa zamani zote,
Ni mamlaka yako ni ya vizazi vyote.
Bwana huwategemeza wote waangukao,
Huwainua wote walioinama chini. (K)
Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote,
Na mwenye fadhili juu ya kazi zake zote.
Bwana yu karibu na wote wamwitao,
Wote wamwitao kwa uaminifu. (K)
SHANGILIO
Mt. 4:4
Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.
INJILI
Yn. 5:17-30
Yesu aliwajibu Wayahudi: Baba yangu anatenda kazi hata sasa, nami ninatenda kazi. Basi kwa sababu hiyo Wayahudi walizidi kutaka kumwua, kwa kuwa hakuivunja sabato tu, bali pamoja na hayo alimwita Mungu Baba yake, akijifanya sawa na Mungu.
Basi Yesu akajibu, akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Mwana hawezi kutenda neno mwenyewe ila lile ambalo amwona Baba analitenda; kwa maana yote ayatendayo yeye, ndiyo ayatendayo Mwana vile vile. Kwa kuwa Baba ampenda Mwana, naye humwonyesha yote ayatendayo mwenyewe; hata na kazi kubwa zaidi kuliko hizi atamwonyesha ili ninyi mpate kustaajabu. Maana kama Baba awafufuavyo wafu na kuwahuisha, vivyo hivyo na Mwana ahuisha wale awatakao. Tena Baba hamhukumu mtu yeyote, bali amempa Mwana hukumu yote, ili watu wote wamheshimu Mwana kama vile wanavyomheshimu Baba. Asiyemheshimu Mwana hamheshimu Baba aliyempeleka.
Amin, amin, nawaambia, yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani. Amin, amin, nawaambia, Saa inakuja, na sasa ipo, wafu watakapoisikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale waisikiao watakuwa hai.
Maana kam avile Baba alivyo na uzima nafsini mwake, vivyo hivyo alimpa na Mwana kuwa na uzima nafsini mwake. Naye akampa amri ya kufanya hukumu kwa sababu ni Mwana wa Adamu. Msistaajabie maneno hayo; kwa maana sasa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu. Mimi siwezi kufanya neno mwenyewe; kama nisikiavyo ndivyo nihukumuvyo na hukumu yangu ni ya haki, kwa sababu siyatafuti mapenzi yangu mimi, bali mapenzi yake aliyenipeleka.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Baraka kwako na familia yako.
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Mwamini katika mpango wake.
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Neema na amani iwe nawe.
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Imani inaweza kusogeza milima
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Katika imani, yote yanawezekana
Tumaini ni nanga ya roho
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Mungu ni mwema, wakati wote!
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Dumu katika Bwana.
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Nakuombea 🙏
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Rehema zake hudumu milele
Nguvu hutoka kwa Bwana
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Mwamini Bwana; anajua njia
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Mungu akubariki!
Endelea kuwa na imani!
Rehema hushinda hukumu
Neema ya Mungu inatosha kwako
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Sifa kwa Bwana!
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni