SOMO 1
Isa. 65:17-21
Bwana asema: Tazama, mimi naumba mbingu mpya na nchi mpya, na mambo ya kwanza hayatakumbukwa, wala hayataingia moyoni. Lakini furahini, mkashangilie daima, kwa ajili ya hivi niviumbavyo; maana, tazama, naumba Yerusalemu uwe shangwe, na watu wake wawe furaha.
Nami nitaufurahia Yerusalemu, nitawaonea shangwe watu wangu; sauti ya kulia haitasikiwa ndani yake tena, wala sauti ya kuomboleza. Hatakuwapo tena mtoto wa siku chache, wala mzee asiyetimia siku zake; kwa maana mtoto atakufa mwenye umri wa miaka mia; bali mtenda dhambi mwenye umri wa miaka mia atalaaniwa. Nao watajenga nyumba, na kukaa ndani yake; watapanda mizabibu, na kula matunda yake.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 30:1, 3-5, 10-12 (K) 1
(K) Nitakutukuza, ee Bwana, kwa maana umeniinua.
Ee Bwana, nitakutukuza kwa maana umeniinua,
Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu.
Umeniinua nafsi yangu,
Ee Bwana, kutoka kuzimu.
Umenihuisha na kunitoa
Miongoni mwao washukao shimoni. (K)
Mwimbieni Bwana zaburi,
Enyi watauwa wake.
Na kufanya shukrani.
Kwa kumbukumbu la utakatifu wake.
Maana ghadhabu zake ni za kitambo kidogo,
Katika radhi yake mna uhai.
Huenda kilio huja kukaa usiku,
Lakini asubuhi huwa furaha. (K)
Ee Bwana, usikie, unirehemu,
Bwana, uwe msaidizi wangu.
Uligeuza matanga yangu kuwa machezo;
Ulinivua gunia, ukanivika furaha.
Ee Bwana, mungu wangu,
Nitakushukuru milele. (K)
SHANGILIO
Eze. 33:11
Sikufurahii kufa kwake mtu mwovu, asema Bwana, bali aiache njia yake mbaya, akaishi.
INJILI
Yn. 4:43-54
Baada ya siku mbili hizo Yesu aliondoka huko, akaenda Galilaya. Kwa maana Yesu mwenyewe alishuhudia ya kwamba nabii hapati heshima katika nchi yake mwenyewe. Basi alipofika Galilaya, Wagalilaya walimpokea; kwa kuwa wameyaona mambo yote aliyoyatenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu; maana hao nao waliiendea sikukuu.
Basi alifika tena Kana ya Galilaya, hapo alipoyafanya yale maji kuwa divai. Na palikuwa na diwani mmoja ambaye mwanawe hawezi huko Kapernaumu. Huyo aliposikia ya kwamba Yesu amekuja kutoka Uyahudi mpaka Galilaya, alimwendea, akamsihi ashuke na kumponya mwanawe; kwa maana alikuwa kufani. Basi Yesu akamwambia, Msipoona ishara na maajabu hamtaamini kabisa? Yule diwani akamwambia, Bwana, ushuke asijakufa mtoto wangu. Yesu akamwambia, Enenda; mwanao yu hai. Mtu yule akalisadiki lile neno aliloambiwa na Yesu, naye akashika njia. Hata alipokuwa akishuka, watumwa wake walimlaki, wakisema ya kwamba mtoto wake yu hai. Basi akawauliza habari ya saa alipoanza kuwa hajambo; nao wakamwambia, jana, saa saba, homa ilimwacha. Basi babaye akafahamu ya kuwa ni saa ile ile alipoambiwa na Yesu, Mwanao yu hai. Akaamini yeye na wote wa nyumbani mwake.
Hiyo ni ishara ya pili aliyoifanya Yesu, alipokuwa ametoka Uyahudi kufika Galilaya.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Mungu ni mwema, wakati wote!
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Mungu akubariki!
Imani inaweza kusogeza milima
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Nakuombea 🙏
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Katika imani, yote yanawezekana
Rehema zake hudumu milele
Baraka kwako na familia yako.
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Endelea kuwa na imani!
Tumaini ni nanga ya roho
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Mwamini Bwana; anajua njia
Mwamini katika mpango wake.
Dumu katika Bwana.
Rehema hushinda hukumu
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Neema na amani iwe nawe.
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Neema ya Mungu inatosha kwako
Sifa kwa Bwana!
Nguvu hutoka kwa Bwana
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe